Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Apocalypse 17
Bible en Swahili de l’est


La chute de Babylone

1 Akaja mmoja wa wale malaika saba, wenye vile vitasa saba, akanena nami, akisema, Njoo huku, nitakuonyesha hukumu ya yule kahaba mkuu aketiye juu ya maji mengi;
Jérémie 51.13 Apocalypse 21.9 Apocalypse 19.2 Apocalypse 15.1 Apocalypse 16.19
2 ambaye wafalme wa nchi wamezini naye, nao wakaao katika nchi wamelevywa kwa mvinyo ya uasherati wake.
Apocalypse 14.8 Apocalypse 18.3 Jérémie 51.7 Apocalypse 18.9 Apocalypse 17.17
3 Akanichukua katika Roho hata jangwani, nikaona mwanamke, ameketi juu ya mnyama mwekundu sana, mwenye kujaa majina ya makufuru, mwenye vichwa saba na pembe kumi.
Apocalypse 12.3 Apocalypse 12.6 Apocalypse 12.14 Daniel 7.20 Daniel 7.8
4 Na mwanamke yule alikuwa amevikwa nguo ya rangi ya zambarau, na nyekundu, amepambwa kwa dhahabu, na kito cha thamani, na lulu, naye alikuwa na kikombe cha dhahabu mkononi mwake, kilichojawa na machukizo, na machafu ya uasherati wake.
Jérémie 51.7 Apocalypse 18.16 Apocalypse 18.12 Daniel 11.38 1 Rois 14.24
5 Na katika kipaji cha uso wake alikuwa na jina limeandikwa, la siri, BABELI MKUU, MAMA WA MAKAHABA NA MACHUKIZO YA NCHI.
Apocalypse 14.8 2 Thessaloniciens 2.7 Apocalypse 17.7 Apocalypse 16.19 Jérémie 51.47-51.48
6 Nikamwona yule mwanamke amelewa kwa damu ya watakatifu, na kwa damu ya mashahidi wa Yesu. Nami nilipomwona nikastaajabu ajabu kuu.
Apocalypse 16.6 Apocalypse 13.15 Apocalypse 2.13 Apocalypse 18.20-18.24 Habakuk 1.13
7 Na yule malaika akaniambia, Kwani kustaajabu? Nitakuambia siri ya mwanamke huyu, na ya mnyama huyu amchukuaye, mwenye vile vichwa saba na zile pembe kumi.
Apocalypse 17.1-17.6 Apocalypse 17.8
8 Yule mnyama uliyemwona alikuwako, naye hayuko, naye yu tayari kupanda kutoka kuzimu na kwenda kwenye uharibifu. Na hao wakaao juu ya nchi, wasioandikwa majina yao katika kitabu cha uzima tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu, watastaajabu wamwonapo yule mnyama, ya kwamba alikuwako, naye hayuko, naye atakuwako.
Apocalypse 11.7 Apocalypse 17.11 Apocalypse 19.15-19.21 Apocalypse 3.5 Apocalypse 3.10
9 Hapo ndipo penye akili zenye hekima. Vile vichwa saba ni milima saba anayokalia mwanamke huyo.
Apocalypse 13.18 Apocalypse 17.3 Matthieu 24.15 Apocalypse 17.7 Matthieu 13.11
10 Navyo ni wafalme saba. Watano wamekwisha kuanguka, na mmoja yupo, na mwingine hajaja bado. Naye atakapokuja imempasa kukaa muda mchache.
11 Na yule mnyama aliyekuwako naye hayuko, yeye ndiye wa nane, naye ni mmoja wa wale saba, naye aenenda kwenye uharibifu.
Apocalypse 17.8
12 Na zile pembe kumi ulizoziona ni wafalme kumi, ambao hawajapokea ufalme bado, lakini wapokea mamlaka kama wafalme muda wa saa moja pamoja na yule mnyama.
Apocalypse 13.1 Daniel 7.24 Apocalypse 12.3 Apocalypse 18.10 Zacharie 1.18-1.21
13 Hawa wana shauri moja, nao wampa yule mnyama nguvu zao na mamlaka yao.
Apocalypse 17.17 Actes 4.28 Philippiens 2.2 Philippiens 1.27 Esaïe 10.5-10.7
14 Hawa watafanya vita na Mwana-Kondoo, na Mwana Kondoo atawashinda, kwa maana Yeye ni Bwana wa Mabwana, na Mfalme wa Wafalme, na hao walio pamoja naye ndio walioitwa, na wateule, na waaminifu.
1 Timothée 6.15 Apocalypse 16.14 Apocalypse 1.5 Apocalypse 2.10 Apocalypse 3.21
15 Kisha akaniambia, Yale maji uliyoyaona, hapo aketipo yule kahaba, ni jamaa na makutano na mataifa na lugha.
Apocalypse 17.1 Jérémie 51.42 Apocalypse 11.9 Apocalypse 10.11 Psaumes 18.4
16 Na zile pembe kumi ulizoziona, na huyo mnyama, hao watamchukia yule kahaba, nao watamfanya kuwa mkiwa na uchi, watamla nyama yake, watamteketeza kabisa kwa moto.
Apocalypse 18.8 Lévitique 21.9 Apocalypse 18.16-18.17 Apocalypse 18.19 Jérémie 50.41-50.42
17 Maana Mungu ametia mioyoni mwao kufanya shauri lake, na kufanya shauri moja, na kumpa yule mnyama ufalme wao hata maneno ya Mungu yatimizwe.
Apocalypse 10.7 2 Thessaloniciens 2.10-2.12 Apocalypse 17.13 Luc 22.22 Luc 22.37
18 Na yule mwanamke uliyemwona, ni mji ule mkubwa, wenye ufalme juu ya wafalme wa nchi.
Apocalypse 16.19 Luc 2.1 Apocalypse 18.2 Daniel 2.40-2.41 Apocalypse 12.4

Cette Bible est dans le domaine public.