Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Josué 1.17
Bible en Swahili de l’est


Conquête du pays promis

Josué à la tête d’Israël

1 Ikawa baada ya kufa kwake Musa, mtumishi wa Bwana, Bwana akamwambia Yoshua, mwana wa Nuni, mtumishi wa Musa, akasema,
Deutéronome 34.5 Deutéronome 34.9 Exode 24.13 Deutéronome 1.38 Josué 12.6
2 Musa mtumishi wangu amekufa; haya basi, ondoka, vuka mto huu wa Yordani; wewe na watu hawa wote, mkaende hata nchi niwapayo wana wa Israeli.
Josué 1.11 Deutéronome 3.28 Esaïe 42.1 Deutéronome 31.7 Josué 1.1
3 Kila mahali zitakapopakanyaga nyayo za miguu yenu, nimewapa ninyi, kama nilivyomwapia Musa.
Deutéronome 11.24 Josué 14.9 Tite 1.2
4 Tangu jangwa hili na mlima huu, Lebanoni, mpaka mto ule mkubwa, mto wa Frati, nchi yote ya Wahiti, tena mpaka bahari ile kubwa upande wa machweo ya jua, hapo ndipo patakapokuwa mpaka wenu.
Exode 23.31 Genèse 15.18-15.21 Deutéronome 3.25 Nombres 34.2-34.18 Deutéronome 1.7
5 Hapatakuwa mtu ye yote atakayeweza kusimama mbele yako siku zote za maisha yako; kama nilivyokuwa pamoja na Musa, ndivyo nitakavyokuwa pamoja na wewe; sitakupungukia wala sitakuacha.
Deutéronome 31.6-31.8 Josué 1.9 Matthieu 28.20 Esaïe 41.10-41.14 Exode 3.12
6 Uwe hodari na moyo wa ushujaa, maana ni wewe utakayewarithisha watu hawa nchi hii niliyowaapia baba zao ya kwamba nitawapa.
Josué 1.9 Josué 1.7 1 Chroniques 22.13 Esaïe 35.3-35.4 Zacharie 8.9
7 Uwe hodari tu na ushujaa mwingi, uangalie kutenda sawasawa na sheria yote aliyokuamuru Musa mtumishi wangu; usiiache, kwenda mkono wa kuume, au wa kushoto, upate kufanikiwa sana kila uendako.
Josué 11.15 Deutéronome 5.32 1 Chroniques 22.13 Deutéronome 28.14 1 Rois 2.3
8 Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana.
Psaumes 119.15 Psaumes 19.14 Colossiens 3.16 Luc 11.28 Jean 14.21
9 Je! Si mimi niliyekuamuru? Uwe hodari na moyo wa ushujaa; usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yu pamoja nawe kila uendako.
Genèse 28.15 Josué 1.6-1.7 Jérémie 1.7-1.8 Psaumes 46.7 Psaumes 27.1-27.2
10 Ndipo Yoshua akawaamuru maakida wa watu, akisema,
11 Piteni katikati ya matuo, mkawaamuru hao watu, mkisema, Fanyeni tayari vyakula; kwa maana baada ya siku tatu mtavuka mto huu wa Yordani, ili kuingia na kuimiliki nchi awapayo Bwana, Mungu wenu, mpate kuimiliki.
Josué 3.2 Deutéronome 9.1 Deutéronome 11.31 Exode 19.11 Osée 6.2
12 Tena Yoshua akawaambia Wareubeni, na Wagadi, na hao wa nusu ya kabila ya Manase, akasema,
Nombres 32.20-32.22
13 Likumbukeni neno lile alilowaamuru Musa mtumishi wa Bwana, akisema, Bwana, Mungu wenu, anawapa ninyi raha, naye atawapa nchi hii.
Nombres 32.20-32.28 Deutéronome 3.18-3.20 Josué 22.1-22.4
14 Wake zenu, na watoto wenu, na makundi yenu, watakaa katika nchi aliyowapa Musa ng’ambo ya Yordani; bali ninyi mtavuka mbele ya ndugu zenu, hali mmevikwa silaha zenu, watu wote wenye nguvu, na ushujaa, ili mpate kuwasaidia;
Deutéronome 20.8 Apocalypse 17.4 Exode 13.18
15 hata Bwana atakapowapa ndugu zenu raha, kama alivyowapa ninyi, na wao pia wamepata kuimiliki nchi awapayo Bwana, Mungu wenu; ndipo mtakapoirudia nchi ya milki yenu na kuimiliki, ambayo Musa mtumishi wa Bwana aliwapeni ng’ambo ya Yordani upande wa maawio ya jua.
1 Corinthiens 12.26 Galates 6.2 Galates 5.13 1 Corinthiens 13.5 Nombres 32.17-32.22
16 Wakamjibu Yoshua, wakasema, Hayo yote uliyotuamuru tutayafanya, na kila mahali utakakotutuma tutakwenda.
1 Pierre 2.13-2.15 Deutéronome 5.27 Nombres 32.25 Tite 3.1 Romains 13.1-13.5
17 Kama vile tulivyomsikiliza Musa katika mambo yote, ndivyo tutakavyokusikiliza wewe; Bwana, Mungu wako, na awe pamoja nawe tu, kama alivyokuwa pamoja na Musa.
Josué 1.5 1 Rois 1.37 1 Timothée 2.1-2.2 Psaumes 20.1 Psaumes 20.9
18 Kila mtu atakayeiasi amri yako, asiyasikilize maneno yako katika mambo yote utakayomwamuru, atauawa. Uwe hodari na moyo wa ushujaa, hilo tu.
Josué 1.9 Josué 1.6-1.7 Luc 19.27 Deutéronome 17.12 1 Corinthiens 16.13

Cette Bible est dans le domaine public.