Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jacques 1.23
Bible en Swahili de l’est


Adresse et salutation

1 Yakobo, mtumwa wa Mungu, na wa Bwana Yesu Kristo, kwa kabila kumi na mbili waliotawanyika; salamu.
Jude 1.1 1 Pierre 1.1 Galates 2.9 Actes 15.23 Actes 21.18

La mise à l’épreuve de la foi

2 Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali;
1 Pierre 1.6-1.8 Jacques 1.12 Matthieu 5.10-5.12 Luc 6.22-6.23 Actes 5.41
3 mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi.
Romains 5.3-5.4 Hébreux 10.36 1 Pierre 1.7 2 Corinthiens 4.17 2 Pierre 1.6
4 Saburi na iwe na kazi kamilifu, mpate kuwa wakamilifu na watimilifu bila kupungukiwa na neno.
Matthieu 5.48 Habakuk 2.3 Luc 21.19 Colossiens 4.12 2 Timothée 3.17
5 Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa.
Proverbes 2.3-2.6 Jean 15.7 Proverbes 3.5-3.7 1 Rois 3.7-3.12 Jérémie 29.12-29.13
6 Ila na aombe kwa imani, pasipo shaka yo yote; maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari lililochukuliwa na upepo, na kupeperushwa huku na huku.
Matthieu 21.21-21.22 Ephésiens 4.14 Marc 11.22-11.24 Hébreux 11.6 Hébreux 10.23
7 Maana mtu kama yule asidhani ya kuwa atapokea kitu kwa Bwana.
Jacques 4.3 Proverbes 21.27 Esaïe 1.15 Proverbes 15.8 Esaïe 58.3-58.4
8 Mtu wa nia mbili husita-sita katika njia zake zote.
1 Rois 18.21 Jacques 4.8 Matthieu 6.24 2 Pierre 2.14 Esaïe 29.13
9 Lakini ndugu asiye na cheo na afurahi kwa kuwa ametukuzwa;
Jérémie 9.23-9.24 Psaumes 62.9 Jacques 2.5-2.6 Philippiens 3.14 Proverbes 17.5
10 bali tajiri kwa kuwa ameshushwa; kwa maana kama ua la majani atatoweka.
1 Pierre 1.24 1 Jean 2.17 1 Timothée 6.17 1 Corinthiens 7.31 Job 14.2
11 Maana jua huchomoza kwa hari, huyakausha majani; ua lake huanguka, uzuri wa umbo lake hupotea; vivyo hivyo naye tajiri atanyauka katika njia zake.
Esaïe 40.7-40.8 Ecclésiaste 5.15 1 Pierre 1.4 Psaumes 102.11 Psaumes 102.4

Appel à vivre la parole de vérité

12 Heri mtu astahimiliye majaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa ataipokea taji ya uzima, Bwana aliyowaahidia wampendao.
1 Corinthiens 9.25 1 Pierre 5.10 2 Timothée 4.8 1 Pierre 1.6-1.8 Jacques 2.5
13 Mtu ajaribiwapo, asiseme, Ninajaribiwa na Mungu; maana Mungu hawezi kujaribiwa na maovu, wala yeye mwenyewe hamjaribu mtu.
Romains 9.19-9.20 Habakuk 2.12-2.13 Esaïe 63.17 Jacques 1.2 Genèse 3.12
14 Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa.
Ephésiens 4.22 Marc 7.21-7.22 Esaïe 44.20 Hébreux 3.13 Matthieu 15.18
15 Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti.
Psaumes 7.14 Job 15.35 Genèse 2.17 Esaïe 59.4 Genèse 3.6
16 Ndugu zangu wapenzi, msidanganyike.
Jacques 2.5 Galates 6.7 Jacques 1.19 Philippiens 4.1 Colossiens 2.4
17 Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu, hushuka kwa Baba wa mianga; kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeuka-geuka.
Jean 3.27 Matthieu 7.11 Nombres 23.19 1 Jean 1.5 Hébreux 13.8
18 Kwa kupenda kwake mwenyewe alituzaa sisi kwa neno la kweli, tuwe kama limbuko la viumbe vyake.
1 Pierre 1.23 Jean 1.13 Apocalypse 14.4 1 Pierre 1.3 Jérémie 2.3
19 Hayo mnajua, ndugu zangu wapenzi. Basi kila mtu na awe mwepesi wa kusikia, bali si mwepesi wa kusema; wala kukasirika;
Proverbes 17.27 Proverbes 10.19 Proverbes 21.23 Proverbes 13.3 Proverbes 14.29
20 kwa maana hasira ya mwanadamu haiitendi haki ya Mungu.
2 Timothée 2.24-2.25 Ephésiens 4.26 Nombres 20.11-20.12 Jacques 3.17-3.18
21 Kwa hiyo wekeeni mbali uchafu wote na ubaya uzidio, na kupokea kwa upole neno lile lililopandwa ndani, liwezalo kuziokoa roho zenu.
Ephésiens 4.22 Ephésiens 1.13 Psaumes 25.9 Colossiens 3.5-3.8 1 Pierre 2.1
22 Lakini iweni watendaji wa neno, wala si wasikiaji tu, hali mkijidanganya nafsi zenu.
Romains 2.13 Jean 13.17 Luc 6.46-6.48 1 Jean 2.3 Jacques 4.17
23 Kwa sababu mtu akiwa ni msikiaji wa neno tu, wala si mtendaji, mtu huyo ni kama mtu anayejiangalia uso wake katika kioo.
Matthieu 7.26-7.27 Jacques 2.14-2.26 Ezéchiel 33.31-33.32 Luc 6.47 Jérémie 44.16
24 Maana hujiangalia, kisha huenda zake, mara akasahau jinsi alivyo.
2 Pierre 3.11 Luc 7.39 Matthieu 8.27 1 Thessaloniciens 1.5 Juges 8.18
25 Lakini aliyeitazama sheria kamilifu iliyo ya uhuru, na kukaa humo, asiwe msikiaji msahaulifu, bali mtendaji wa kazi, huyo atakuwa heri katika kutenda kwake.
Luc 11.28 1 Pierre 2.16 Jean 13.17 Galates 5.1 Jacques 2.12
26 Mtu akidhani ya kuwa anayo dini, wala hauzuii ulimi wake kwa hatamu, hali akijidanganya moyo wake, dini yake mtu huyo haifai.
Psaumes 141.3 1 Pierre 3.10 Ephésiens 4.29 Psaumes 34.13 Jacques 3.2-3.6
27 Dini iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu Baba ni hii, Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa.
Esaïe 1.16-1.17 1 Jean 3.17-3.19 Matthieu 25.34-25.46 1 Jean 2.15-2.17 Galates 6.9-6.10

Cette Bible est dans le domaine public.