Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Timothée 2.9
Bible en Swahili de l’est


Conseils pour le service dans l’Église

1 Basi wewe, mwanangu, uwe hodari katika neema iliyo katika Kristo Yesu.
Ephésiens 6.10 1 Corinthiens 16.13 2 Timothée 1.7 2 Corinthiens 12.9-12.10 Philippiens 4.13
2 Na mambo yale uliyoyasikia kwangu mbele ya mashahidi wengi, hayo uwakabidhi watu waaminifu watakaofaa kuwafundisha na wengine.
2 Timothée 1.13-1.14 1 Timothée 6.12 1 Timothée 1.18 2 Timothée 3.10 Tite 1.5-1.9
3 Ushiriki taabu pamoja nami, kama askari mwema wa Kristo Yesu.
2 Timothée 1.8 2 Timothée 4.5 Jacques 1.12 1 Timothée 1.18 2 Corinthiens 1.6
4 Hakuna apigaye vita ajitiaye katika shughuli za dunia, ili ampendeze yeye aliyemwandika awe askari.
Luc 8.14 2 Timothée 4.10 2 Pierre 2.20 1 Thessaloniciens 2.4 1 Corinthiens 7.22-7.23
5 Hata mtu akishindana katika machezo hapewi taji, asiposhindana kwa halali.
1 Corinthiens 9.24-9.27 Jacques 1.12 Apocalypse 4.10 Hébreux 2.7 1 Pierre 5.4
6 Yampasa mkulima mwenye taabu ya kazi kuwa wa kwanza wa kupata fungu la matunda.
Hébreux 10.36 1 Corinthiens 9.23 Jean 4.35-4.38 Matthieu 9.37-9.38 1 Corinthiens 3.6-3.9
7 Yafahamu sana hayo nisemayo, kwa maana Bwana atakupa akili katika mambo yote.
Genèse 41.38-41.39 1 Jean 5.20 Jacques 3.17 Hébreux 7.4 Philippiens 4.8
8 Mkumbuke Yesu Kristo, aliyefufuka katika wafu, wa uzao wa Daudi kama inenavyo injili yangu.
Romains 2.16 Matthieu 1.1 Actes 2.24 Apocalypse 5.5 Actes 13.23
9 Nami katika hiyo nimeteswa hata kufungwa kama mtenda mabaya; lakini neno la Mungu halifungwi.
2 Timothée 1.8 Philippiens 1.7 Actes 28.31 2 Timothée 4.17 Ephésiens 6.19-6.20
10 Kwa ajili ya hilo nastahimili mambo yote, kwa ajili ya wateule, ili wao nao waupate wokovu ule ulio katika Kristo Yesu, pamoja na utukufu wa milele.
Colossiens 1.24 2 Corinthiens 1.6 2 Corinthiens 4.17 1 Pierre 5.10 2 Timothée 2.3
11 Ni neno la kuaminiwa. Kwa maana, Kama tukifa pamoja naye, tutaishi pamoja naye pia;
Romains 6.8 1 Timothée 1.15 1 Thessaloniciens 5.10 1 Thessaloniciens 4.17 Romains 6.5
12 Kama tukistahimili, tutamiliki pamoja naye; Kama tukimkana yeye, yeye naye atatukana sisi;
Matthieu 10.33 Romains 8.17 Apocalypse 20.4 Apocalypse 20.6 Luc 12.9
13 Kama sisi hatuamini, yeye hudumu wa kuaminiwa. Kwa maana hawezi kujikana mwenyewe.
Romains 3.3 Nombres 23.19 2 Thessaloniciens 3.3 Tite 1.2 1 Thessaloniciens 5.24
14 Uwakumbushe mambo hayo, ukiwaonya machoni pa Mungu, wasiwe na mashindano ya maneno, ambayo hayana faida, bali huwaharibu wasikiao.
2 Timothée 2.23 2 Timothée 4.1 Romains 14.1 1 Timothée 5.21 Hébreux 13.9
15 Jitahidi kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mtenda kazi asiye na sababu ya kutahayari, ukitumia kwa halali neno la kweli.
2 Pierre 1.10 2 Pierre 1.15 2 Corinthiens 10.18 2 Corinthiens 5.9 1 Thessaloniciens 2.4
16 Jiepushe na maneno yasiyo na maana, ambayo si ya dini; kwa kuwa wataendelea zaidi katika maovu,
Tite 3.9 1 Timothée 6.20 2 Thessaloniciens 2.7-2.8 Osée 12.1 Esdras 10.10
17 na neno lao litaenea kama donda-ndugu. Miongoni mwa hao wamo Himenayo na Fileto,
1 Timothée 1.20 Nahum 3.15 Jacques 5.3
18 walioikosa ile kweli, wakisema ya kwamba kiyama imekwisha kuwapo, hata kuipindua imani ya watu kadha wa kadha.
1 Corinthiens 15.12 1 Timothée 1.19 Colossiens 3.1 Hébreux 3.10 1 Corinthiens 11.19
19 Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye muhuri hii, Bwana awajua walio wake. Na tena, Kila alitajaye jina la Bwana na auache uovu.
Jean 10.14 1 Corinthiens 8.3 1 Jean 3.7-3.10 Nombres 16.5 Nahum 1.7
20 Basi katika nyumba kubwa havimo vyombo vya dhahabu na fedha tu, bali na vya mti, na vya udongo; vingine vina heshima, vingine havina.
Lamentations 4.2 1 Pierre 2.5 1 Timothée 3.15 Romains 9.21-9.23 Daniel 5.2
21 Basi ikiwa mtu amejitakasa kwa kujitenga na hao, atakuwa chombo cha kupata heshima, kilichosafishwa, kimfaacho Bwana, kimetengenezwa kwa kila kazi iliyo njema.
2 Timothée 3.17 Ephésiens 2.10 2 Timothée 2.20 Psaumes 119.9 1 Pierre 1.22
22 Lakini zikimbie tamaa za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi.
1 Timothée 6.11 1 Corinthiens 6.18 1 Pierre 2.11 Hébreux 12.14 1 Corinthiens 10.14
23 Walakini uyakatae maswali ya upumbavu yasiyo na elimu, ukijua ya kuwa huzaa magomvi.
Tite 3.9 1 Timothée 4.7 2 Timothée 2.14 1 Timothée 6.4-6.5 2 Timothée 2.16
24 Tena haimpasi mtumwa wa Bwana kuwa mgomvi; bali kuwa mwanana kwa watu wote, awezaye kufundisha, mvumilivu;
1 Timothée 3.2-3.3 Tite 3.2 Tite 1.7 Philippiens 2.14 1 Thessaloniciens 2.7
25 akiwaonya kwa upole wao washindanao naye, ili kama ikiwezekana, Mungu awape kutubu na kuijua kweli;
1 Timothée 2.4 Actes 8.22 Galates 6.1 1 Pierre 3.15 Actes 11.18
26 wapate tena fahamu zao, na kutoka katika mtego wa Ibilisi, ambao hao wametegwa naye, hata kuyafanya mapenzi yake.
Esaïe 49.25-49.26 1 Timothée 3.7 Psaumes 124.7 Esaïe 42.6-42.7 Esaïe 28.13

Cette Bible est dans le domaine public.