Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Timothée 2.1
Bible en Swahili de l’est


Conseils pour le service dans l’Église

1 Basi wewe, mwanangu, uwe hodari katika neema iliyo katika Kristo Yesu.
Ephésiens 6.10 2 Timothée 1.7 1 Corinthiens 16.13 Philippiens 4.13 1 Timothée 1.18
2 Na mambo yale uliyoyasikia kwangu mbele ya mashahidi wengi, hayo uwakabidhi watu waaminifu watakaofaa kuwafundisha na wengine.
2 Timothée 1.13-1.14 1 Timothée 1.18 1 Timothée 6.12 Tite 1.5-1.9 2 Timothée 3.10
3 Ushiriki taabu pamoja nami, kama askari mwema wa Kristo Yesu.
2 Timothée 1.8 2 Timothée 4.5 Jacques 1.12 1 Timothée 1.18 2 Timothée 2.10
4 Hakuna apigaye vita ajitiaye katika shughuli za dunia, ili ampendeze yeye aliyemwandika awe askari.
Luc 8.14 2 Pierre 2.20 2 Timothée 4.10 1 Thessaloniciens 2.4 1 Corinthiens 7.22-7.23
5 Hata mtu akishindana katika machezo hapewi taji, asiposhindana kwa halali.
Jacques 1.12 1 Corinthiens 9.24-9.27 Colossiens 1.29 Hébreux 2.9 Apocalypse 2.10
6 Yampasa mkulima mwenye taabu ya kazi kuwa wa kwanza wa kupata fungu la matunda.
Hébreux 10.36 1 Corinthiens 3.6-3.9 Esaïe 28.24-28.26 Matthieu 21.33-21.41 Luc 10.2
7 Yafahamu sana hayo nisemayo, kwa maana Bwana atakupa akili katika mambo yote.
Genèse 41.38-41.39 Jacques 3.17 1 Jean 5.20 Hébreux 13.7 Hébreux 12.3
8 Mkumbuke Yesu Kristo, aliyefufuka katika wafu, wa uzao wa Daudi kama inenavyo injili yangu.
Matthieu 1.1 Romains 2.16 Actes 2.24 Hébreux 12.2-12.3 Luc 24.46
9 Nami katika hiyo nimeteswa hata kufungwa kama mtenda mabaya; lakini neno la Mungu halifungwi.
2 Timothée 1.8 Philippiens 1.7 Actes 28.31 2 Thessaloniciens 3.1 2 Timothée 1.12
10 Kwa ajili ya hilo nastahimili mambo yote, kwa ajili ya wateule, ili wao nao waupate wokovu ule ulio katika Kristo Yesu, pamoja na utukufu wa milele.
Colossiens 1.24 2 Corinthiens 1.6 2 Corinthiens 4.17 1 Pierre 5.10 2 Timothée 2.3
11 Ni neno la kuaminiwa. Kwa maana, Kama tukifa pamoja naye, tutaishi pamoja naye pia;
Romains 6.8 1 Timothée 1.15 1 Thessaloniciens 5.10 Romains 6.5 1 Thessaloniciens 4.17
12 Kama tukistahimili, tutamiliki pamoja naye; Kama tukimkana yeye, yeye naye atatukana sisi;
Matthieu 10.33 Romains 8.17 Apocalypse 20.4 Luc 12.9 Apocalypse 20.6
13 Kama sisi hatuamini, yeye hudumu wa kuaminiwa. Kwa maana hawezi kujikana mwenyewe.
Romains 3.3 Nombres 23.19 Tite 1.2 2 Thessaloniciens 3.3 1 Thessaloniciens 5.24
14 Uwakumbushe mambo hayo, ukiwaonya machoni pa Mungu, wasiwe na mashindano ya maneno, ambayo hayana faida, bali huwaharibu wasikiao.
2 Timothée 2.23 1 Timothée 5.21 2 Timothée 4.1 Romains 14.1 1 Samuel 12.21
15 Jitahidi kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mtenda kazi asiye na sababu ya kutahayari, ukitumia kwa halali neno la kweli.
2 Pierre 1.10 2 Corinthiens 5.9 1 Thessaloniciens 2.4 2 Pierre 1.15 2 Corinthiens 10.18
16 Jiepushe na maneno yasiyo na maana, ambayo si ya dini; kwa kuwa wataendelea zaidi katika maovu,
Tite 3.9 1 Timothée 6.20 Osée 12.1 Esdras 10.10 2 Thessaloniciens 2.7-2.8
17 na neno lao litaenea kama donda-ndugu. Miongoni mwa hao wamo Himenayo na Fileto,
1 Timothée 1.20 Nahum 3.15 Jacques 5.3
18 walioikosa ile kweli, wakisema ya kwamba kiyama imekwisha kuwapo, hata kuipindua imani ya watu kadha wa kadha.
1 Corinthiens 15.12 1 Timothée 1.19 Matthieu 15.13 Luc 22.31-22.32 1 Timothée 6.21
19 Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye muhuri hii, Bwana awajua walio wake. Na tena, Kila alitajaye jina la Bwana na auache uovu.
Jean 10.14 1 Corinthiens 8.3 1 Jean 3.7-3.10 Nombres 16.5 Jean 10.27-10.30
20 Basi katika nyumba kubwa havimo vyombo vya dhahabu na fedha tu, bali na vya mti, na vya udongo; vingine vina heshima, vingine havina.
Romains 9.21-9.23 Lamentations 4.2 1 Pierre 2.5 1 Timothée 3.15 Esdras 1.6
21 Basi ikiwa mtu amejitakasa kwa kujitenga na hao, atakuwa chombo cha kupata heshima, kilichosafishwa, kimfaacho Bwana, kimetengenezwa kwa kila kazi iliyo njema.
2 Timothée 3.17 Ephésiens 2.10 1 Jean 3.3 2 Corinthiens 7.1 2 Timothée 2.20
22 Lakini zikimbie tamaa za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi.
1 Corinthiens 6.18 1 Timothée 6.11 1 Pierre 2.11 Hébreux 12.14 1 Corinthiens 10.14
23 Walakini uyakatae maswali ya upumbavu yasiyo na elimu, ukijua ya kuwa huzaa magomvi.
Tite 3.9 2 Timothée 2.14 1 Timothée 4.7 1 Timothée 6.4-6.5 2 Timothée 2.16
24 Tena haimpasi mtumwa wa Bwana kuwa mgomvi; bali kuwa mwanana kwa watu wote, awezaye kufundisha, mvumilivu;
Tite 3.2 1 Timothée 3.2-3.3 Tite 1.7 Philippiens 2.14 Colossiens 3.13
25 akiwaonya kwa upole wao washindanao naye, ili kama ikiwezekana, Mungu awape kutubu na kuijua kweli;
1 Timothée 2.4 Galates 6.1 Actes 8.22 1 Pierre 3.15 Actes 20.21
26 wapate tena fahamu zao, na kutoka katika mtego wa Ibilisi, ambao hao wametegwa naye, hata kuyafanya mapenzi yake.
Esaïe 49.25-49.26 1 Timothée 3.7 Psaumes 124.7 Jean 13.27 Apocalypse 20.2-20.3

Cette Bible est dans le domaine public.