Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Thessaloniciens 5.8
Bible en Swahili de l’est


1 Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie.
1 Thessaloniciens 4.9 Actes 1.7 Matthieu 24.3 Matthieu 24.36 Jude 1.3
2 Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.
Apocalypse 16.15 2 Pierre 3.10 Apocalypse 3.3 Matthieu 24.42-24.44 Luc 12.39-12.40
3 Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa.
2 Thessaloniciens 1.9 Luc 21.34-21.35 Hébreux 2.3 Luc 17.26-17.30 Josué 8.20-8.22
4 Bali ninyi, ndugu, hammo gizani, hata siku ile iwapate kama mwivi.
1 Jean 2.8 Romains 13.11-13.13 Actes 26.18 2 Pierre 3.10 Deutéronome 19.6
5 Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa nuru, na wana wa mchana; sisi si wa usiku, wala wa giza.
Ephésiens 5.8 Luc 16.8 Actes 26.18 Jean 12.36
6 Basi tusilale usingizi kama wengine, bali tukeshe, na kuwa na kiasi.
1 Pierre 1.13 Romains 13.11-13.14 Luc 22.46 Matthieu 24.42 Apocalypse 16.15
7 Maana walalao usingizi hulala usiku, pia na walewao hulewa usiku.
2 Pierre 2.13 Actes 2.15 1 Corinthiens 15.34 Romains 13.13 Proverbes 23.29-23.35
8 Lakini sisi tulio wa mchana, tuwe na kiasi, hali tukijivika kifuani imani na upendo, na chapeo yetu iwe tumaini la wokovu.
1 Pierre 1.13 Ephésiens 6.11 1 Thessaloniciens 5.5 Esaïe 59.17 Romains 13.12-13.13
9 Kwa kuwa Mungu hakutuweka kwa hasira yake, bali tupate wokovu, kwa Bwana wetu Yesu Kristo;
1 Thessaloniciens 1.10 2 Thessaloniciens 2.13-2.14 Proverbes 16.4 2 Timothée 2.19-2.20 1 Timothée 1.13
10 ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, kwamba twakesha au kwamba twalala.
Romains 14.8-14.9 2 Corinthiens 5.15 1 Corinthiens 15.3 1 Thessaloniciens 4.13 1 Thessaloniciens 4.17
11 Basi, farijianeni na kujengana kila mtu na mwenzake, vile vile kama mnavyofanya.
Ephésiens 4.29 Hébreux 10.25 Hébreux 3.13 Romains 15.2 1 Thessaloniciens 4.18

Dernières recommandations

12 Lakini, ndugu, tunataka mwatambue wale wanaojitaabisha kwa ajili yenu, na kuwasimamia ninyi katika Bwana, na kuwaonyeni;
Hébreux 13.17 1 Corinthiens 16.16 1 Corinthiens 16.18 Hébreux 13.7 1 Corinthiens 15.10
13 mkawastahi sana katika upendo, kwa ajili ya kazi zao. Iweni na amani ninyi kwa ninyi.
Marc 9.50 Jean 13.34-13.35 Jean 15.17 Hébreux 12.14 Jacques 3.18
14 Ndugu, twawasihi, waonyeni wale wasiokaa kwa utaratibu; watieni moyo walio dhaifu; watieni nguvu wanyonge; vumilieni na watu wote.
2 Timothée 4.2 2 Thessaloniciens 3.6-3.7 Romains 14.1 Hébreux 12.12 Actes 20.35
15 Angalieni mtu awaye yote asimlipe mwenziwe mabaya kwa mabaya; bali siku zote lifuateni lililo jema, ninyi kwa ninyi na kwa watu wote.
1 Pierre 3.9 Galates 6.10 1 Pierre 2.22-2.23 Romains 12.9 Romains 14.19
16 Furahini siku zote;
Philippiens 4.4 Romains 12.12 Matthieu 5.12 2 Corinthiens 6.10 Luc 10.20
17 ombeni bila kukoma;
Romains 12.12 Colossiens 4.2 Luc 18.1 Ephésiens 6.18 Luc 21.36
18 shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu.
Ephésiens 5.20 Philippiens 4.6 Colossiens 3.17 Hébreux 13.15 1 Pierre 2.15
19 Msimzimishe Roho;
Ephésiens 4.30 Actes 7.51 Psaumes 51.11 1 Timothée 4.14 Esaïe 63.10
20 msitweze unabii;
1 Corinthiens 14.37-14.39 1 Corinthiens 14.22-14.25 1 Corinthiens 14.3-14.6 1 Corinthiens 14.1 1 Corinthiens 11.4
21 jaribuni mambo yote; lishikeni lililo jema;
1 Jean 4.1 Romains 12.2 Ephésiens 5.10 Luc 12.57 1 Corinthiens 2.14-2.15
22 jitengeni na ubaya wa kila namna.
Philippiens 4.8 1 Corinthiens 10.31-10.33 Romains 12.17 1 Corinthiens 8.13 2 Corinthiens 6.3
23 Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; nanyi nafsi zenu na roho zenu na miili yenu mhifadhiwe mwe kamili, bila lawama, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
Hébreux 4.12 1 Thessaloniciens 3.13 Jude 1.24 Romains 15.33 1 Pierre 5.10
24 Yeye ni mwaminifu ambaye awaita, naye atafanya.
2 Thessaloniciens 3.3 1 Corinthiens 1.9 Nombres 23.19 Esaïe 25.1 1 Pierre 5.10
25 Ndugu, tuombeeni.
Colossiens 4.3 2 Thessaloniciens 3.1-3.3 2 Corinthiens 1.11 Hébreux 13.18-13.19 Romains 15.30
26 Wasalimuni ndugu wote kwa busu takatifu.
Romains 16.16 1 Corinthiens 16.20
27 Nawaapisha kwa Bwana, ndugu wote wasomewe waraka huu.
Colossiens 4.16 Nombres 27.23 1 Timothée 5.7 1 Timothée 6.17 1 Timothée 1.18
28 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja nanyi.
Romains 16.20 2 Thessaloniciens 3.18 Romains 16.23 Romains 1.7

Cette Bible est dans le domaine public.