Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Deutéronome 33.15
Bible en Swahili de l’est


Bénédiction de Moïse

1 Hii ndiyo baraka ya Musa, huyo mtu wa Mungu, aliyowabarikia wana wa Israeli kabla ya kufa kwake.
Josué 14.6 Jean 14.27 2 Pierre 1.21 Genèse 27.27-27.29 Luc 24.50-24.51
2 Akasema,Bwana alitoka Sinai,Akawaondokea kutoka Seiri;Aliangaza katika kilima cha Parani,Akaja Meribath-Kadeshi.Upande wake wa kuume Palikuwa na sheria ya moto-moto kwao.
Actes 7.53 Habakuk 3.3 Apocalypse 5.11 Psaumes 68.17 Psaumes 68.7-68.8
3 Hakika awapenda hayo makabila ya watu; Watakatifu wake wote wamo mkononi mwako; Nao waliketi miguuni pako; Watapokea kila mmoja katika maneno yako.
Luc 10.39 Deutéronome 7.6-7.8 Actes 22.3 Malachie 1.2 Osée 11.1
4 Musa alituagiza torati, Ni urithi kwa mkutano wa Yakobo.
Psaumes 119.111 Jean 1.17 Jean 7.19 Deutéronome 9.26-9.29 Psaumes 119.72
5 Akawa mfalme katika Yeshuruni, Walipokutanika wakuu wa watu, Makabila yote ya Israeli pamoja.
Deutéronome 32.15 Nombres 16.13-16.15 Genèse 36.31 Juges 8.22 Juges 9.2
6 Reubeni na aishi, asife; Lakini watu wake na wawe wachache.
Genèse 49.3-49.4 Nombres 32.31-32.32 Josué 22.1-22.9 Genèse 49.8
7 Na baraka ya Yuda ni hii; akasema, Isikize, Ee Bwana, sauti ya Yuda, Umlete ndani kwa watu wake; Alijitetea kwa mikono yake; Nawe utakuwa msaada juu ya adui zake.
Genèse 49.8-49.12 2 Samuel 7.9-7.12 Apocalypse 19.13-19.16 Juges 1.1-1.7 Psaumes 110.1-110.2
8 Akamnena Lawi, Thumimu yako na Urimu yako vina mtakatifu wako, Uliyemjaribu huko Masa; Ukateta naye kwenye maji ya Meriba.
Exode 17.7 Exode 28.30 Nombres 20.13 Lévitique 8.8 Psaumes 106.16
9 Aliyemtaja baba yake na mama yake, Mimi sikumwona; Wala nduguze hakuwakubali; Wala hakuwajua watoto wake mwenyewe; Maana wameliangalia neno lako, Wamelishika agano lako.
Matthieu 22.16 2 Corinthiens 5.16 1 Chroniques 17.17 Lévitique 21.11 Luc 14.26
10 Watamfundisha Yakobo hukumu zako, Na Israeli torati yako, Wataweka uvumba mbele zako, Na sadaka nzima za kuteketezwa madhabahuni mwako.
Psaumes 51.19 Lévitique 10.11 Exode 30.7-30.8 Ezéchiel 43.27 1 Samuel 2.28
11 Ee Bwana, ubariki mali zake, Utakabali kazi ya mikono yake; Uwapige viuno vyao waondokao juu yake, Na wenye kumchukia, wasiinuke tena.
Ezéchiel 43.27 Ezéchiel 20.40-20.41 2 Samuel 24.23 Luc 10.10-10.12 Deutéronome 18.1-18.5
12 Akamnena Benyamini, Mpenzi wa Bwana atakaa salama kwake; Yuamfunika mchana kutwa, Naye hukaa kati ya mabega yake.
1 Rois 12.21 Deutéronome 12.10 Esaïe 37.35 Esaïe 51.16 Esaïe 37.22
13 Na Yusufu akamnena, Nchi yake na ibarikiwe na Bwana; Kwa vitu vya thamani vya mbinguni, kwa huo umande, Na kwa kilindi kilalacho chini,
Genèse 49.22-49.26 Genèse 27.28-27.29 Deutéronome 32.2 Psaumes 110.3 Genèse 48.15-48.20
14 Na kwa vitu vilivyo bora vya matunda ya jua, Na kwa vitu vilivyo bora vya maongeo ya miezi,
Apocalypse 22.2 Deutéronome 28.8 Matthieu 5.45 2 Samuel 23.4 1 Timothée 6.17
15 Na kwa vitu viteule vya milima ya kale, Na kwa vitu vilivyo bora vya vilima vya milele,
Habakuk 3.6 Genèse 49.26 Jacques 5.7
16 Na kwa vitu vilivyo bora vya nchi, na kujaa kwake, Na uradhi wake aliyekaa ndani ya kile kijiti; Na ije baraka juu ya kichwa chake Yusufu, Juu ya utosi wa kichwa chake aliyetengwa na nduguze.
Psaumes 24.1 Exode 3.2-3.4 Actes 7.35 Genèse 49.26 Genèse 45.9-45.11
17 Mzaliwa wa kwanza wa ng’ombe wake mume, enzi ni yake; Na pembe zake ni pembe za nyati; Kwa hizo atayasukuma mataifa yote, hata ncha za nchi; Nao ni makumi ya maelfu ya Efraimu, Nao ni maelfu ya Manase.
Nombres 23.22 Psaumes 44.5 1 Rois 22.11 Psaumes 92.10 1 Chroniques 5.1
18 Na Zabuloni akamnena, Furahi Zabuloni, katika kutoka kwako;
Genèse 49.13-49.15 Josué 19.11 Juges 5.14
19 Watayaita mataifa waje mlimani; Wakasongeze huko sadaka za haki; Kwa kuwa watanyonya wingi wa bahari, Na akiba zilizofichamana za mchangani.
Esaïe 60.5 Psaumes 4.5 Esaïe 2.3 Exode 15.17 Psaumes 107.22
20 Na Gadi akamnena, Na abarikiwe amwongezaye Gadi; Yeye hukaa kama simba mke, Hurarua mkono, naam, na utosi wa kichwa.
Genèse 49.19 1 Chroniques 5.18-5.21 Psaumes 18.36 Josué 13.24-13.28 1 Chroniques 12.8-12.14
21 Akajichagulia sehemu ya kwanza, Kwani ndiko lilikowekwa fungu la mtoa-sheria; Akaja pamoja na wakuu wa watu, Akaitekeleza haki ya Bwana, Na hukumu zake kwa Israeli.
Josué 1.14 Josué 22.1-22.4 Juges 5.2 Juges 5.11 Nombres 32.16-32.42
22 Na Dani akamnena, Dani ni mwana-simba, Arukaye kutoka Bashani.
Juges 18.27 Josué 19.47 Juges 13.2 Juges 13.24-13.25 Juges 14.19
23 Na Naftali akamnena, Ee Naftali, uliyeshiba fadhili, Uliyejawa na baraka ya Bwana; Umiliki magharibi na kusini.
Genèse 49.21 Josué 19.32-19.39 Matthieu 4.16 Psaumes 36.8 Matthieu 4.13
24 Na Asheri akamnena, Na abarikiwe Asheri kwa watoto; Na akubaliwe katika nduguze, Na achovye mguu wake katika mafuta.
Genèse 49.20 Job 29.6 Psaumes 128.3 Psaumes 128.6 Romains 15.31
25 Makomeo yako yatakuwa ya chuma na shaba; Na kadiri ya siku zako ndivyo zitakavyokuwa nguvu zako.
Esaïe 41.10 Psaumes 138.3 Philippiens 4.13 2 Chroniques 16.9 Luc 15.22
26 Hapana aliyefanana na Mungu, Ee Yeshuruni, Ajaye amepanda juu ya mbingu ili akusaidie. Na juu ya mawingu katika utukufu wake.
Exode 15.11 Psaumes 104.3 Habakuk 3.8 Psaumes 68.33-68.34 Jérémie 10.6
27 Mungu wa milele ndiye makazi yako, Na mikono ya milele i chini yako. Na mbele yako amemsukumia mbali adui; Akasema, Angamiza.
Psaumes 18.2 Esaïe 25.4 Romains 16.20 Psaumes 91.9 Esaïe 57.15
28 Na Israeli anakaa salama, Chemchemi ya Yakobo peke yake, Katika nchi ya ngano na divai; Naam, mbingu zake zadondoza umande.
Nombres 23.9 Genèse 27.28 Jérémie 23.6 Deutéronome 33.13 Esaïe 48.1
29 U heri, Israeli. Ni nani aliye kama wewe, taifa lililookolewa na Bwana! Ndiye ngao ya msaada wako, Na upanga wa utukufu wako; Na adui zako watajitiisha chini yako, Nawe utapakanyaga mahali pao pa juu.
Psaumes 115.9-115.11 2 Samuel 7.23 Esaïe 45.17 Deutéronome 32.13 Habakuk 3.19

Cette Bible est dans le domaine public.