Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Deutéronome 3.23
Bible en Swahili de l’est


Conquête du royaume d’Og

1 Ndipo tukageuka, tukakwea njia ya Bashani; na Ogu, mfalme wa Bashani, akatutokea juu yetu, yeye na watu wake wote, kuja kupigana huko Edrei.
Deutéronome 29.7 Nombres 21.33-21.35 Deutéronome 1.4 Deutéronome 31.4 Psaumes 136.20
2 Bwana akaniambia, Usimwogope; kwa kuwa nimemtia mkononi mwako, yeye na watu wake wote na nchi yake; nawe utamtenda mfano wa ulivyomtenda Sihoni, mfalme wa Waamori, aliyekuwa akikaa Heshboni.
Nombres 21.23-21.25 Deutéronome 3.11 Apocalypse 2.10 Nombres 14.9 Deutéronome 20.3
3 Basi Bwana, Mungu wetu, akamtia mikononi mwetu na Ogu mfalme wa Bashani, na watu wake wote; tukampiga, asisaziwe cho chote.
Nombres 21.35 Josué 13.12 Josué 13.30 Deutéronome 2.33-2.34
4 Tukatwaa miji yake yote wakati huo; hapakuwa na mji tusiotwaa kwao miji sitini, nchi yote ya Argobu, ndio ufalme wa Ogu ulio katika Bashani.
1 Rois 4.13 Josué 12.4 Josué 13.30-13.31 Nombres 32.33-32.42
5 Miji hiyo yote ilikuwa yenye maboma marefu, na malango, na makomeo, pamoja na miji isiyokuwa na maboma, mingi sana.
Deutéronome 1.28 Nombres 13.28 Hébreux 11.30
6 Tukaiharibu kabisa, kama tulivyomfanya huyo Sihoni, mfalme wa Heshboni, kwa kuharibu kabisa kila mji uliokuwa na watu, pamoja na wanawake na watoto.
Deutéronome 2.34 Deutéronome 2.24 Psaumes 135.10-135.12 Lévitique 27.28-27.29 Josué 11.14
7 Lakini wanyama wote wa mji, na nyara za miji, tulitwaa kuwa mawindo yetu.
Deutéronome 2.35 Josué 8.27 Josué 11.11-11.14
8 Tukaitwaa na nchi wakati huo, katika mikono ya hao wafalme wawili wa Waamori waliokuwa ng’ambo ya Yordani, tokea bonde la Arnoni mpaka kilima cha Hermoni;
Josué 13.9-13.12 Josué 12.2-12.6 Nombres 32.33-32.42
9 (na hiyo Hermoni Wasidoni huiita Sirioni, na Waamori huiita Seniri);
1 Chroniques 5.23 Psaumes 29.6 Psaumes 133.3 Cantique 4.8 Ezéchiel 27.5
10 miji yote ya nchi tambarare, na Gileadi yote, na Bashani yote, mpaka Saleka na Edrei, nayo ni miji ya ufalme wa Ogu katika Bashani.
Deutéronome 4.49 Josué 13.11-13.12 Josué 12.4-12.5 Nombres 21.33 Josué 13.31
11 (Kwani aliyesalia katika mabaki ya Warefai ni Ogu pekee, mfalme wa Bashani; tazama, kitanda chake kilikuwa kitanda cha chuma; kitanda hicho je! Hakiko Raba kwa wana wa Amoni? Urefu wake ulikuwa ni mikono kenda,na upana wake mikono minne,kwa mfano wa mkono wa mtu)
Genèse 14.5 Jérémie 49.2 2 Samuel 12.26 Amos 1.14 1 Samuel 17.4

Attribution des premiers territoires

12 Na nchi hiyo tuliitwaa ikawa milki yetu, wakati huo; tokea Aroeri iliyo kwenye bonde la Arnoni, na nusu ya nchi ya milima ya Gileadi, na miji iliyokuwamo, niliwapa Wareubeni na Wagadi;
Deutéronome 2.36 Nombres 32.32-32.38 Josué 13.8-13.28 Deutéronome 4.48 Josué 12.2-12.6
13 na nchi ya Gileadi iliyobaki, na Bashani yote, maana huo ufalme wa Ogu niliwapa nusu ya kabila ya Manase; nchi yote ya Argobu, nayo ndiyo Bashani yote. (Na nchi hii yaitwa nchi ya Warefai.
Nombres 32.39-32.42 Josué 13.29-13.32 1 Chroniques 5.23-5.26
14 Yairi, mwana wa Manase, alitwaa nchi yote ya Argobu, hata mpaka wa Wageshuri na Wamaaka; akaziita nchi hizo Hawoth-yairi, kwa jina lake mwenyewe, hata hivi leo, maana, hizo nchi za Bashani.)
Nombres 32.41 Josué 13.13 2 Samuel 3.3 2 Samuel 13.37 2 Samuel 10.6
15 Na Makiri nilimpa Gileadi.
Nombres 32.39-32.40 Josué 22.7 Genèse 50.23 Josué 17.1-17.3 Nombres 26.29
16 Na Wareubeni na Wagadi niliwapa tokea Gileadi mpaka bonde la Arnoni, katikati ya bonde, na mpaka wake; mpaka mto wa Yaboki, nao ni mpaka wa wana wa Amoni;
Nombres 21.24 2 Samuel 24.5 Deutéronome 2.37 Genèse 32.22 Josué 12.2-12.3
17 na nchi ya Araba nayo, na mto wa Yordani, na mpaka wake, tokea Kinerethi mpaka bahari ya hiyo Araba, nayo ni Bahari ya Chumvi, chini ya matelemko ya Pisga, upande wa mashariki.
Josué 12.3 Genèse 14.3 Josué 3.16 Deutéronome 4.49 Josué 13.27
18 Nikawaamuru wakati huo, nikawaambia, Bwana, Mungu wenu, amewapa ninyi nchi hii mwimiliki, basi vukeni ng’ambo wenye silaha mbele ya ndugu zenu, wana wa Israeli, nyote mlio mashujaa.
Josué 4.12-4.13 Josué 22.1-22.9 Josué 1.12-1.15 Nombres 32.20-32.24
19 Lakini wake wenu na watoto wenu, na wanyama wenu wa mji, (nawajua kwamba mna wanyama wengi), na wakae katika miji yenu niliyowapa;
20 hata Bwana awapumzishe ndugu zenu kama ninyi, nao pia waimiliki nchi wapewayo na Bwana, Mungu wenu, ng’ambo ya Yordani; ndipo mtakaporudi kila mmoja aende katika milki yake niliyowapa.
Josué 22.4 Josué 22.8
21 Nikamwamuru Yoshua wakati huo, nikamwambia, Macho yako yameona yote aliyowatenda Bwana, Mungu wenu, wale wafalme wawili, navyo ndivyo atakavyoutenda Bwana kila ufalme huko uvukiako.
2 Corinthiens 1.10 2 Corinthiens 12.10 Nombres 27.18-27.23 1 Samuel 17.36-17.37 Psaumes 9.10
22 Msiwache, kwa kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye awapiganiaye.
Deutéronome 20.4 Exode 14.14 Deutéronome 1.30 2 Chroniques 20.29 Josué 10.42

L’entrée en Canaan refusée à Moïse

23 Nikamnyenyekea Bwana wakati huo, nikamwambia,
2 Corinthiens 12.8-12.9
24 Ee Bwana Mungu, umeanza kumwonyesha mtumishi wako ukubwa wako, na mkono wako wa nguvu; kwani kuna mungu gani mbinguni au duniani awezaye kufanya mfano wa kazi zako, na mfano wa matendo yako yenye nguvu?
Exode 15.11 Deutéronome 11.2 Psaumes 71.19 Psaumes 86.8 2 Samuel 7.22
25 Nami nakuomba nivuke, nikaione hiyo nchi nzuri iliyoko ng’ambo ya Jordani, mlima ule mzuri, na Lebanoni.
Exode 3.8 Deutéronome 4.21-4.22 Deutéronome 11.11-11.12 Nombres 32.5 Ezéchiel 20.6
26 Lakini Bwana alikuwa amenikasirikia kwa ajili yenu, asinisikize; Bwana akaniambia, Na ikutoshe, usinene nami zaidi jambo hili.
Deutéronome 1.37 Deutéronome 31.2 Psaumes 106.32-106.33 Matthieu 26.39 1 Chroniques 17.4
27 Kwea katika kilele cha Pisga ukainue macho yako upande wa magharibi, na kaskazini, na kusini, na mashariki, ukatazame kwa macho yako, kwa maana huuvuki mto huu wa Yordani.
Nombres 27.12 Genèse 13.14-13.15 Deutéronome 34.1-34.4
28 Lakini mwagize Yoshua umtie moyo mkuu, umtie na nguvu; kwani ndiye atakayevuka mbele ya watu hawa, na nchi utakayoiona atawarithisha yeye.
Deutéronome 31.3 Deutéronome 31.23 Deutéronome 1.38 Deutéronome 31.7 Nombres 27.18-27.23
29 Basi tukakaa katika bonde lililoelekea Beth-peori.
Deutéronome 4.46 Deutéronome 34.6 Nombres 25.3 Deutéronome 4.3 Nombres 33.48-33.49

Cette Bible est dans le domaine public.