Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Corinthiens 7.9
Bible en Swahili de l’est


1 Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu.
1 Thessaloniciens 4.7 Proverbes 8.13 1 Pierre 2.11 Jacques 4.8 Ezéchiel 36.25-36.26

Des nouvelles encourageantes

2 Tupeni nafasi mioyoni mwenu. Hatukumdhulumu mtu ye yote, wala kumharibu mtu, wala kumkaramkia mtu.
Actes 20.33 Colossiens 4.10 Matthieu 10.40 Romains 16.18 Matthieu 10.14
3 Sisemi neno hilo ili niwahukumu ninyi kuwa na hatia; kwa maana nimetangulia kusema, ya kwamba ninyi mmo mioyoni mwetu hata kwa kufa pamoja, na kuishi pamoja.
2 Corinthiens 6.11-6.12 1 Corinthiens 4.14-4.15 Ruth 1.16-1.17 1 Thessaloniciens 2.8 2 Corinthiens 13.10
4 Ninao ujasiri mwingi kwenu; naona fahari kuu juu yenu. Nimejaa faraja, katika dhiki yetu yote nimejaa furaha ya kupita kiasi.
2 Corinthiens 3.12 2 Corinthiens 1.4 Philippiens 2.17 Colossiens 1.24 2 Corinthiens 8.24
5 Kwa maana hata tulipokuwa tumefika Makedonia miili yetu haikupata nafuu; bali tulidhikika kote kote; nje palikuwa na vita, ndani hofu.
Deutéronome 32.25 2 Corinthiens 2.13 Job 18.11 1 Corinthiens 15.31 Actes 20.1
6 Lakini Mungu, mwenye kuwafariji wanyonge, alitufariji kwa kuja kwake Tito.
2 Corinthiens 1.3-1.4 2 Corinthiens 7.13 1 Thessaloniciens 3.6-3.7 1 Thessaloniciens 3.2 Jean 14.16
7 Wala si kwa kuja kwake tu, bali kwa zile faraja nazo alizofarijiwa kwenu, akituarifu habari ya shauku yenu, na maombolezo yenu, na bidii yenu kwa ajili yangu, hata nikazidi kufurahi.
2 Corinthiens 7.10-7.11 2 Corinthiens 8.16 Jacques 4.9-4.10 Romains 1.12 Psaumes 31.9-31.11
8 Kwa sababu, ijapokuwa naliwahuzunisha kwa waraka ule, sijuti; hata ikiwa nalijuta, naona ya kwamba waraka ule uliwahuzunisha, ingawa ni kwa kitambo tu.
2 Corinthiens 7.11 Apocalypse 3.19 2 Corinthiens 7.6 Lamentations 3.32 2 Corinthiens 2.2-2.11
9 Sasa nafurahi, si kwa sababu ya ninyi kuhuzunishwa, bali kwa sababu mlihuzunishwa, hata mkatubu. Maana mlihuzunishwa kwa jinsi ya Mungu, ili msipate hasara kwa tendo letu katika neno lo lote.
2 Corinthiens 13.8-13.10 Actes 20.21 2 Corinthiens 7.10-7.11 Zacharie 12.10 Luc 15.7
10 Maana huzuni iliyo kwa jinsi ya Mungu hufanya toba liletalo wokovu lisilo na majuto; bali huzuni ya dunia hufanya mauti.
Actes 11.18 2 Samuel 12.13 2 Timothée 2.25-2.26 1 Rois 8.47-8.50 Actes 3.19
11 Maana, angalieni, kuhuzunishwa kuko huko kwa jinsi ya Mungu kulitenda bidii kama nini ndani yenu; naam, na kujitetea, naam, na kukasirika, naam, na hofu, naam, na shauku, naam, na kujitahidi, naam, na kisasi! Kwa kila njia mmejionyesha wenyewe kuwa safi katika jambo hilo.
2 Corinthiens 7.7 2 Corinthiens 6.4 Psaumes 145.19 Néhémie 13.25 2 Samuel 12.5-12.7
12 Basi, ijapokuwa naliwaandikia, sikuandika kwa ajili yake yeye aliyedhulumu, wala si kwa ajili yake yeye aliyedhulumiwa, bali bidii yenu kwa ajili yetu ipate kudhihirishwa kwenu mbele za Mungu.
2 Corinthiens 2.9 2 Corinthiens 11.28 2 Corinthiens 2.17 2 Corinthiens 7.8 2 Corinthiens 2.3-2.4
13 Kwa hiyo tulifarijiwa. Tena katika kufarijiwa kwetu tulifurahi sana kupita kiasi kwa sababu ya furaha ya Tito; maana roho yake imeburudishwa na ninyi nyote.
2 Corinthiens 7.6 Romains 15.32 1 Corinthiens 12.26 1 Corinthiens 13.5-13.7 2 Corinthiens 2.3
14 Kwa maana, ikiwa nimejisifu mbele yake katika neno lo lote kwa ajili yenu, sikutahayarishwa; bali, kama tulivyowaambia mambo yote kwa kweli, vivyo hivyo na kujisifu kwetu kwa Tito kulikuwa kweli.
2 Corinthiens 7.4 2 Corinthiens 8.24 2 Thessaloniciens 1.4 2 Corinthiens 10.8 2 Corinthiens 1.18-1.20
15 Na mapenzi yake kwenu yamekuwa mengi kupita kiasi, akumbukapo kutii kwenu ninyi nyote, jinsi mlivyomkaribisha kwa hofu na kutetemeka.
Philippiens 2.12 2 Corinthiens 2.9 Philippiens 1.8 Psaumes 2.11 Cantique 5.4
16 Nafurahi, kwa sababu katika kila neno nina moyo mkuu kwa ajili yenu.
2 Corinthiens 2.3 Philémon 1.8 Philémon 1.21 2 Thessaloniciens 3.4

Cette Bible est dans le domaine public.