Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Corinthiens 7.10
Bible en Swahili de l’est


1 Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu.
Proverbes 8.13 1 Thessaloniciens 4.7 1 Pierre 2.11 Hébreux 4.1 Psaumes 51.10

Des nouvelles encourageantes

2 Tupeni nafasi mioyoni mwenu. Hatukumdhulumu mtu ye yote, wala kumharibu mtu, wala kumkaramkia mtu.
Actes 20.33 2 Jean 1.10 Philippiens 2.29 Luc 10.8 2 Corinthiens 11.9
3 Sisemi neno hilo ili niwahukumu ninyi kuwa na hatia; kwa maana nimetangulia kusema, ya kwamba ninyi mmo mioyoni mwetu hata kwa kufa pamoja, na kuishi pamoja.
2 Corinthiens 6.11-6.12 1 Thessaloniciens 2.8 2 Corinthiens 13.10 2 Corinthiens 11.11 2 Corinthiens 12.15
4 Ninao ujasiri mwingi kwenu; naona fahari kuu juu yenu. Nimejaa faraja, katika dhiki yetu yote nimejaa furaha ya kupita kiasi.
2 Corinthiens 1.4 2 Corinthiens 3.12 Colossiens 1.24 Philippiens 2.17 2 Corinthiens 11.21
5 Kwa maana hata tulipokuwa tumefika Makedonia miili yetu haikupata nafuu; bali tulidhikika kote kote; nje palikuwa na vita, ndani hofu.
Deutéronome 32.25 2 Corinthiens 2.13 Jérémie 20.10 Galates 4.19-4.20 Jérémie 6.25
6 Lakini Mungu, mwenye kuwafariji wanyonge, alitufariji kwa kuja kwake Tito.
2 Corinthiens 1.3-1.4 2 Corinthiens 7.13 1 Thessaloniciens 3.6-3.7 Romains 15.5 Jérémie 31.13
7 Wala si kwa kuja kwake tu, bali kwa zile faraja nazo alizofarijiwa kwenu, akituarifu habari ya shauku yenu, na maombolezo yenu, na bidii yenu kwa ajili yangu, hata nikazidi kufurahi.
Psaumes 6.1-6.6 Proverbes 9.8-9.9 Jude 1.3 Luc 22.44 2 Jean 1.4
8 Kwa sababu, ijapokuwa naliwahuzunisha kwa waraka ule, sijuti; hata ikiwa nalijuta, naona ya kwamba waraka ule uliwahuzunisha, ingawa ni kwa kitambo tu.
Lamentations 3.32 2 Corinthiens 2.2-2.11 Jean 21.17 Hébreux 12.9-12.11 Exode 5.22-5.23
9 Sasa nafurahi, si kwa sababu ya ninyi kuhuzunishwa, bali kwa sababu mlihuzunishwa, hata mkatubu. Maana mlihuzunishwa kwa jinsi ya Mungu, ili msipate hasara kwa tendo letu katika neno lo lote.
2 Corinthiens 13.8-13.10 Actes 20.21 2 Corinthiens 2.16 Luc 15.17-15.24 Luc 15.10
10 Maana huzuni iliyo kwa jinsi ya Mungu hufanya toba liletalo wokovu lisilo na majuto; bali huzuni ya dunia hufanya mauti.
Actes 11.18 2 Samuel 12.13 1 Rois 8.47-8.50 Actes 3.19 2 Timothée 2.25-2.26
11 Maana, angalieni, kuhuzunishwa kuko huko kwa jinsi ya Mungu kulitenda bidii kama nini ndani yenu; naam, na kujitetea, naam, na kukasirika, naam, na hofu, naam, na shauku, naam, na kujitahidi, naam, na kisasi! Kwa kila njia mmejionyesha wenyewe kuwa safi katika jambo hilo.
2 Corinthiens 7.7 Proverbes 28.14 Psaumes 130.6 Job 42.6 1 Corinthiens 12.25
12 Basi, ijapokuwa naliwaandikia, sikuandika kwa ajili yake yeye aliyedhulumu, wala si kwa ajili yake yeye aliyedhulumiwa, bali bidii yenu kwa ajili yetu ipate kudhihirishwa kwenu mbele za Mungu.
2 Corinthiens 2.9 2 Corinthiens 7.8 2 Corinthiens 2.3-2.4 1 Corinthiens 5.1-5.2 1 Timothée 3.5
13 Kwa hiyo tulifarijiwa. Tena katika kufarijiwa kwetu tulifurahi sana kupita kiasi kwa sababu ya furaha ya Tito; maana roho yake imeburudishwa na ninyi nyote.
2 Corinthiens 7.6 Romains 15.32 2 Corinthiens 2.13 1 Pierre 3.8 Romains 12.15
14 Kwa maana, ikiwa nimejisifu mbele yake katika neno lo lote kwa ajili yenu, sikutahayarishwa; bali, kama tulivyowaambia mambo yote kwa kweli, vivyo hivyo na kujisifu kwetu kwa Tito kulikuwa kweli.
2 Corinthiens 8.24 2 Corinthiens 7.4 2 Corinthiens 1.18-1.20 2 Corinthiens 7.6 2 Corinthiens 9.2-9.4
15 Na mapenzi yake kwenu yamekuwa mengi kupita kiasi, akumbukapo kutii kwenu ninyi nyote, jinsi mlivyomkaribisha kwa hofu na kutetemeka.
Philippiens 2.12 2 Corinthiens 2.9 Ephésiens 6.5 Genèse 43.30 Actes 16.29
16 Nafurahi, kwa sababu katika kila neno nina moyo mkuu kwa ajili yenu.
2 Corinthiens 2.3 2 Thessaloniciens 3.4 Philémon 1.8 Philémon 1.21

Cette Bible est dans le domaine public.