Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jean 20.29
Bible en Swahili de l’est


Résurrection de Jésus

1 Hata siku ya kwanza ya juma Mariamu Magdalene alikwenda kaburini alfajiri, kungali giza bado; akaliona lile jiwe limeondolewa kaburini.
Matthieu 27.60 Marc 15.46 Jean 20.26 Marc 16.9 Luc 24.1-24.10
2 Basi akaenda mbio, akafika kwa Simoni Petro na kwa yule mwanafunzi mwingine ambaye Yesu alimpenda, akawaambia, Wamemwondoa Bwana kaburini, wala hatujui walikomweka.
Jean 13.23 Jean 20.13 Jean 21.7 Jean 19.26 Jean 21.24
3 Basi Petro akatoka, na yule mwanafunzi mwingine, wakashika njia kwenda kaburini.
Luc 24.12
4 Wakaenda mbio wote wawili; na yule mwanafunzi mwingine akaenda mbio upesi kuliko Petro, akawa wa kwanza kufika kaburini.
2 Samuel 18.23 Lévitique 13.30 2 Corinthiens 8.12 1 Corinthiens 9.24
5 Akainama na kuchungulia, akaona vitambaa vya sanda vimelala; lakini hakuingia.
Jean 19.40 Jean 11.44 Jean 20.11
6 Basi akaja na Simoni Petro, akaingia ndani ya kaburi; akavitazama vitambaa vilivyolala,
Jean 18.17 Matthieu 16.15-16.16 Jean 18.25-18.27 Luc 22.31-22.32 Jean 21.15-21.17
7 na ile leso iliyokuwako kichwani pake; haikulala pamoja na vitambaa, bali imezongwa-zongwa mbali mahali pa peke yake.
Jean 11.44
8 Basi ndipo alipoingia naye yule mwanafunzi mwingine aliyekuwa wa kwanza wa kufika kaburini, akaona na kuamini.
Jean 20.4 Jean 1.50 Jean 20.29 Jean 20.25
9 Kwa maana hawajalifahamu bado andiko, ya kwamba imempasa kufufuka.
Esaïe 25.8 Esaïe 53.10-53.12 Esaïe 26.19 Psaumes 16.10 Luc 24.44-24.46
10 Basi wale wanafunzi wakaenda zao tena nyumbani kwao.
Jean 7.53 Jean 16.32
11 Lakini Mariamu alikuwa akisimama karibu na kaburi, nje yake, analia. Basi akilia hivi, aliinama na kuchungulia ndani ya kaburi.
Jean 20.5
12 Akaona malaika wawili, wenye mavazi meupe, wameketi, mmoja kichwani na mmoja miguuni, hapo ulipolazwa mwili wake Yesu.
Luc 24.22-24.23 Marc 16.5-16.6 Daniel 7.9 Matthieu 17.2 Apocalypse 3.4
13 Nao wakamwambia, Mama, unalilia nini? Akawaambia, Kwa sababu wamemwondoa Bwana wangu, wala mimi sijui walikomweka.
Jean 20.15 Jean 20.2 Jean 2.4 Jean 16.20-16.22 1 Samuel 1.8
14 Naye akiisha kusema hayo, akageuka nyuma, akamwona Yesu amesimama, asijue ya kuwa ni Yesu.
Marc 16.9 Matthieu 28.9 Jean 21.4 Luc 24.16 Luc 24.31
15 Yesu akamwambia, Mama, unalilia nini? Unamtafuta nani? Naye, huku akidhania ya kuwa ni mtunza bustani, akamwambia, Bwana, ikiwa umemchukua wewe, uniambie ulipomweka, nami nitamwondoa.
Jean 18.7 Jean 1.38 Jean 20.13 Jean 18.4 Marc 16.6
16 Yesu akamwambia, Mariamu. Yeye akageuka, akamwambia kwa Kiebrania, Raboni! (Yaani, Mwalimu wangu).
Jean 1.38 Jean 10.3 Cantique 3.4 1 Samuel 3.6 Jean 1.49
17 Yesu akamwambia. Usinishike; kwa maana sijapaa kwenda kwa Baba. Lakini enenda kwa ndugu zangu ukawaambie, Ninapaa kwenda kwa Baba yangu naye ni Baba yenu, kwa Mungu wangu naye ni Mungu wenu.
Hébreux 2.11-2.13 Romains 8.14-8.17 Psaumes 43.4 Jean 7.33 Jean 20.27
18 Mariamu Magdalene akaenda, akawapasha wanafunzi habari ya kwamba, Nimemwona Bwana, na ya kwamba amemwambia hayo.
Luc 24.10 Matthieu 28.10 Luc 24.22-24.23 Jean 20.1 Marc 16.10-16.13

Apparitions de Jésus ressuscité aux disciples

19 Ikawa jioni, siku ile ya kwanza ya juma, pale walipokuwapo wanafunzi, milango imefungwa kwa hofu ya Wayahudi; akaja Yesu, akasimama katikati, akawaambia, Amani iwe kwenu.
Jean 20.26 Jean 14.27 Jean 20.21 Jean 7.13 Matthieu 18.20
20 Naye akiisha kusema hayo, akawaonyesha mikono yake na ubavu wake. Basi wale wanafunzi wakafurahi walipomwona Bwana.
Jean 16.22 1 Jean 1.1 Jean 20.27 Jean 16.20 Jean 19.34
21 Basi Yesu akawaambia tena, Amani iwe kwenu; kama Baba alivyonituma mimi, mimi nami nawapeleka ninyi.
Jean 17.18-17.19 Jean 3.17 Luc 24.47-24.49 Jean 13.20 Marc 16.15-16.18
22 Naye akiisha kusema hayo, akawavuvia, akawaambia, Pokeeni Roho Mtakatifu.
Genèse 2.7 Actes 2.38 Actes 2.4 Actes 8.15 Jean 7.39
23 Wo wote mtakaowaondolea dhambi, wameondolewa; na wo wote mtakaowafungia dhambi, wamefungiwa.
Matthieu 16.19 Matthieu 18.18 Actes 10.43 Actes 2.38 Marc 2.5-2.10
24 Walakini mmoja wa wale Thenashara, Tomaso, aitwaye Pacha, hakuwako pamoja nao alipokuja Yesu.
Jean 11.16 Matthieu 10.3 Jean 14.5 Matthieu 18.20 Hébreux 10.25
25 Basi wanafunzi wengine wakamwambia, Tumemwona Bwana. Akawaambia, Mimi nisipoziona mikononi mwake kovu za misumari, na kutia kidole changu katika mahali pa misumari, na kutia mkono wangu katika ubavu wake, mimi sisadiki hata kidogo.
Marc 16.11 Psaumes 106.21-106.24 Hébreux 10.38-10.39 Psaumes 78.11-78.22 Luc 24.25
26 Basi, baada ya siku nane, wanafunzi wake walikuwamo ndani tena, na Tomaso pamoja nao. Akaja Yesu, na milango imefungwa, akasimama katikati, akasema, Amani iwe kwenu.
Jean 20.19 Matthieu 17.1 Esaïe 26.12 Jean 20.21 Esaïe 54.10
27 Kisha akamwambia Tomaso, Lete hapa kidole chako; uitazame mikono yangu; ulete na mkono wako uutie ubavuni mwangu, wala usiwe asiyeamini, bali aaminiye.
Jean 20.25 Luc 24.40 1 Jean 1.1-1.2 Marc 9.19 Romains 5.20
28 Tomaso akajibu, akamwambia, Bwana wangu na Mungu wangu!
Matthieu 14.33 Esaïe 9.6 Jean 20.16 Jean 1.1 Esaïe 7.14
29 Yesu akamwambia, Wewe, kwa kuwa umeniona, umesadiki; wa heri wale wasioona, wakasadiki.
1 Pierre 1.8 2 Corinthiens 5.7 Hébreux 11.27 Hébreux 11.1 Luc 1.45

Objectif de l’auteur

30 Basi kuna ishara nyingine nyingi alizozifanya Yesu mbele ya wanafunzi wake, zisizoandikwa katika kitabu hiki.
Jean 21.25 Luc 1.3-1.4 1 Jean 5.13 1 Corinthiens 10.11 Romains 15.4
31 Lakini hizi zimeandikwa ili mpate kuamini ya kwamba Yesu ndiye Kristo, Mwana wa Mungu; na kwa kuamini mwe na uzima kwa jina lake.
Actes 10.43 1 Jean 5.10-5.13 Jean 3.15-3.16 1 Jean 5.1 1 Jean 5.20

Cette Bible est dans le domaine public.