Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Luc 15.8
Bible en Swahili de l’est


Paraboles de la brebis et de la pièce perdues

1 Basi watoza ushuru wote na wenye dhambi walikuwa wakimkaribia wamsikilize.
Matthieu 9.10-9.13 1 Timothée 1.15 Matthieu 21.28-21.31 Luc 5.29-5.32 Romains 5.20
2 Mafarisayo na waandishi wakanung’unika, wakisema, Mtu huyu huwakaribisha wenye dhambi, tena hula nao.
Matthieu 9.11 Luc 19.7 Galates 2.12 Actes 11.3 Luc 7.39
3 Akawaambia mfano huu, akisema,
4 Ni nani kwenu, mwenye kondoo mia, akipotewa na mmojawapo, asiyewaacha wale tisini na kenda nyikani, aende akamtafute yule aliyepotea hata amwone?
Ezéchiel 34.16 Ezéchiel 34.11-34.12 Jérémie 50.6 1 Pierre 2.25 Matthieu 12.11
5 Naye akiisha kumwona, humweka mabegani pake akifurahi.
Esaïe 53.10-53.11 Michée 7.18 Ezéchiel 18.23 Ephésiens 2.3-2.6 Esaïe 46.3-46.4
6 Na afikapo nyumbani kwake, huwaita rafiki zake na jirani zake, akawaambia, Furahini pamoja nami, kwa kuwa nimekwisha kumpata kondoo wangu aliyepotea.
Actes 11.23 1 Pierre 2.25 1 Thessaloniciens 3.7-3.9 Philippiens 2.17 Luc 2.13-2.14
7 Nawaambia, Vivyo hivyo kutakuwa na furaha mbinguni kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye, kuliko kwa ajili ya wenye haki tisini na kenda ambao hawana haja ya kutubu.
Luc 5.32 Luc 15.10 Proverbes 30.12 Matthieu 18.13 Luc 15.32
8 Au kuna mwanamke gani mwenye shilingi kumi, akipotewa na moja, asiyewasha taa na kufagia nyumba, na kutafuta kwa bidii hata aione?
Ezéchiel 34.12 Luc 19.10 Jean 10.16 Jean 11.52 Ephésiens 2.17
9 Na akiisha kuiona, huwaita rafiki zake na jirani zake, akawaambia, Furahini pamoja nami, kwa kuwa nimeipata tena shilingi ile iliyonipotea.
Luc 15.6-15.7
10 Nawaambia, Vivyo hivyo kuna furaha mbele ya malaika wa Mungu kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye.
2 Corinthiens 7.10 Hébreux 1.14 Apocalypse 5.11-5.14 Actes 10.3-10.5 Ezéchiel 33.11

Parabole du fils perdu et de son frère

11 Akasema, Mtu mmoja alikuwa na wana wawili;
12 yule mdogo akamwambia babaye, Baba, nipe sehemu ya mali inayoniangukia. Akawagawia vitu vyake.
Marc 12.44 Luc 15.30 Deutéronome 21.16-21.17 Psaumes 17.14 Psaumes 16.5-16.6
13 Hata baada ya siku si nyingi, yule mdogo akakusanya vyote, akasafiri kwenda nchi ya mbali; akatapanya mali zake huko kwa maisha ya uasherati.
Luc 16.19 Luc 16.1 Job 22.17-22.18 Esaïe 22.13 2 Chroniques 33.1-33.10
14 Alipokuwa amekwisha tumia vyote, njaa kuu iliingia nchi ile, yeye naye akaanza kuhitaji.
Amos 8.9-8.12 Osée 2.9-2.14 2 Chroniques 33.11 Ezéchiel 16.27
15 Akaenda akashikamana na mwenyeji mmoja wa nchi ile; naye alimpeleka shambani kwake kulisha nguruwe.
Tite 3.3 Nahum 3.6 Jérémie 8.4-8.6 Malachie 2.9 Exode 10.3
16 Akawa akitamani kujishibisha kwa maganda waliyokula nguruwe, wala hapana mtu aliyempa kitu.
Lamentations 4.5 Psaumes 142.4 Romains 6.19-6.21 Esaïe 44.20 Esaïe 57.3
17 Alipozingatia moyoni mwake, alisema, Ni watumishi wangapi wa baba yangu wanaokula chakula na kusaza, na mimi hapa ninakufa kwa njaa.
Ezéchiel 18.28 Ephésiens 5.14 Ephésiens 2.4-2.5 Luc 15.18-15.19 Actes 26.11-26.19
18 Nitaondoka, nitakwenda kwa baba yangu na kumwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako;
Luc 15.21 Matthieu 3.6 Lamentations 3.40 Matthieu 6.9 Matthieu 6.14
19 sistahili kuitwa mwana wako tena; nifanye kama mmoja wa watumishi wako.
Matthieu 15.26-15.27 Genèse 32.10 Job 42.6 1 Pierre 5.6 Luc 7.6-7.7
20 Akaondoka, akaenda kwa babaye. Alipokuwa angali mbali, baba yake alimwona, akamwonea huruma, akaenda mbio akamwangukia shingoni, akambusu sana.
Psaumes 86.5 Genèse 45.14 Genèse 46.29 Deutéronome 30.2-30.4 Psaumes 86.15
21 Yule mwana akamwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako; sistahili kuitwa mwana wako tena.
Psaumes 51.4 Luc 15.18-15.19 1 Corinthiens 8.12 Jérémie 3.13 Ezéchiel 16.63
22 Lakini baba aliwaambia watumwa wake, Lileteni upesi vazi lililo bora, mkamvike; mtieni na pete kidoleni, na viatu miguuni;
Genèse 41.42 Zacharie 3.3-3.5 Esther 8.2 Apocalypse 6.11 Psaumes 45.13
23 mleteni ndama yule aliyenona mkamchinje; nasi tule na kufurahi;
Esaïe 25.6 Esaïe 65.13-65.14 Genèse 18.7 Proverbes 9.2 Psaumes 63.5
24 kwa kuwa huyu mwanangu alikuwa amekufa, naye amefufuka; alikuwa amepotea, naye ameonekana. Wakaanza kushangilia.
Ephésiens 2.1 Luc 15.32 Ephésiens 5.14 Ephésiens 2.5 1 Timothée 5.6
25 Basi, yule mwanawe mkubwa alikuwako shamba na alipokuwa akija na kuikaribia nyumba, alisikia sauti ya nyimbo na machezo.
Psaumes 149.3 Luc 15.11-15.12 Ecclésiaste 3.4 Exode 15.20 Psaumes 150.4
26 Akaita mtumishi mmoja, akamwuliza, Mambo haya, maana yake nini?
27 Akamwambia, Ndugu yako amekuja, na baba yako amemchinja ndama aliyenona, kwa sababu amempata tena, yu mzima.
Luc 15.30 Actes 22.13 Actes 9.17 Philémon 1.16
28 Akakasirika, akakataa kuingia ndani. Basi babaye alitoka nje, akamsihi.
1 Samuel 18.8 Jonas 4.9 Genèse 4.5-4.7 Jonas 4.1-4.4 Actes 13.50
29 Akamjibu baba yake, akasema, Tazama, mimi nimekutumikia miaka mingapi hii, wala sijakosa amri yako wakati wo wote, lakini hujanipa mimi mwana-mbuzi, nifanye furaha na rafiki zangu;
Luc 18.11-18.12 Apocalypse 3.17 1 Samuel 15.13-15.14 Luc 17.10 1 Jean 1.8-1.10
30 lakini, alipokuja huyu mwana wako aliyekula vitu vyako pamoja na makahaba, umemchinjia yeye ndama aliyenona.
Luc 15.12-15.13 Proverbes 29.3 Exode 32.11 Exode 32.7 Luc 15.32
31 Akamwambia, Mwanangu, wewe u pamoja nami sikuzote, na vyote nilivyo navyo ni vyako.
Romains 11.1 Romains 11.35 Marc 7.27-7.28 Matthieu 20.13-20.16 Luc 19.22-19.23
32 Tena, kufanya furaha na shangwe ilipasa, kwa kuwa huyu ndugu yako alikuwa amekufa, naye amefufuka; alikuwa amepotea, naye ameonekana.
Luc 15.24 Ephésiens 2.1-2.10 Esaïe 35.10 Romains 3.19 Romains 15.9-15.13

Cette Bible est dans le domaine public.