Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 17.23
Bible en Swahili de l’est


La transfiguration

1 Na baada ya siku sita Yesu akawatwaa Petro, na Yakobo, na Yohana nduguye, akawaleta juu ya mlima mrefu faraghani;
Marc 5.37 Matthieu 26.37 Luc 9.28-9.36 Marc 9.2-9.13 2 Corinthiens 13.1
2 akageuka sura yake mbele yao; uso wake ukang’aa kama jua, mavazi yake yakawa meupe kama nuru.
Apocalypse 10.1 Psaumes 104.2 Matthieu 28.3 Luc 9.29 Exode 34.29-34.35
3 Na tazama, wakatokewa na Musa na Eliya, wakizungumza naye.
Deutéronome 34.5-34.6 2 Corinthiens 3.7-3.11 Marc 9.4 Luc 24.44 Luc 1.17
4 Petro akajibu akamwambia Yesu, Bwana, ni vizuri sisi kuwapo hapa; ukitaka, nitafanya hapa vibanda vitatu, kimoja chako wewe, na kimoja cha Musa, na kimoja cha Eliya.
Luc 9.33 Apocalypse 21.23 Marc 9.5-9.6 Psaumes 16.11 Apocalypse 22.3-22.5
5 Alipokuwa katika kusema, tazama, wingu jeupe likawatia uvuli; na tazama, sauti ikatoka katika lile wingu, ikasema, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye; msikieni yeye.
Matthieu 3.17 Esaïe 42.1 Deutéronome 18.15 Luc 3.22 Marc 9.7
6 Na wale wanafunzi waliposikia, walianguka kifulifuli, wakaogopa sana.
2 Pierre 1.18 Juges 13.22 Ezéchiel 43.3 Daniel 10.7-10.9 Ezéchiel 3.23
7 Yesu akaja, akawagusa, akasema, Inukeni, wala msiogope.
Daniel 10.18 Daniel 10.10 Matthieu 14.27 Daniel 8.18 Apocalypse 1.17
8 Wakainua macho yao, wasione mtu ila Yesu peke yake.
Marc 9.8 Luc 9.36 Actes 12.10-12.11
9 Na walipokuwa wakishuka mlimani, Yesu aliwaagiza, akasema, Msimwambie mtu ye yote habari ya maono hayo, hata Mwana wa Adamu atakapofufuka katika wafu.
Marc 8.30 Luc 8.56 Luc 9.21-9.22 Marc 9.9-9.13 Matthieu 8.20
10 Wanafunzi wake wakamwuliza, wakisema, Basi kwa nini waandishi hunena ya kwamba imempasa Eliya kuja kwanza?
Matthieu 11.14 Malachie 4.5-4.6 Jean 1.25 Matthieu 27.47-27.49 Jean 1.21
11 Naye akajibu, akawaambia, Kweli Eliya yuaja kwanza, naye atatengeneza yote,
Luc 1.16-1.17 Actes 3.21 Malachie 4.6 Luc 3.3-3.14
12 ila nawaambia, ya kwamba Eliya amekwisha kuja, wasimtambue, lakini wakamtenda yote waliyotaka. Vivyo hivyo Mwana wa Adamu naye yuaenda kuteswa kwao.
Matthieu 16.21 Actes 13.24-13.28 Actes 4.10 Esaïe 53.3-53.12 Actes 3.14-3.15
13 Ndipo wale wanafunzi walipofahamu ya kuwa amesema nao habari za Yohana Mbatizaji.
Matthieu 11.14

Guérison d’un épileptique

14 Nao walipoufikia mkutano, mtu mmoja akamjia, akampigia magoti, akisema,
Actes 10.25-10.26 Matthieu 17.14-17.19 Luc 9.37-9.43 Marc 9.14-9.29 Marc 10.17
15 Bwana, umrehemu mwanangu, kwa kuwa ana kifafa, na kuteswa vibaya; maana mara nyingi huanguka motoni, na mara nyingi majini.
Matthieu 4.24 Matthieu 8.31-8.32 Marc 9.20-9.22 Luc 9.38-9.42 Matthieu 15.22
16 Nikamleta kwa wanafunzi wako, wasiweze kumponya.
Actes 3.16 Actes 19.15-19.16 2 Rois 4.29-4.31 Matthieu 17.19-17.20 Luc 9.40
17 Yesu akajibu, akasema, Enyi kizazi kisichoamini, kilichopotoka, nitakaa pamoja nanyi hata lini? Nitachukuliana nanyi hata lini? Mleteni huku kwangu.
Hébreux 3.16-3.19 Matthieu 16.8 Actes 13.18 Jean 20.27 Marc 9.19
18 Yesu akamkemea pepo, naye akamtoka; yule kijana akapona tangu saa ile.
Matthieu 9.22 Jean 4.52-4.53 Marc 5.8 Actes 19.13-19.15 Actes 16.18
19 Kisha wale wanafunzi wakamwendea Yesu kwa faragha wakasema Mbona sisi hatukuweza kumtoa?
Marc 4.10 Marc 9.28
20 Yesu akawaambia, Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana, amin, nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu.
Marc 11.23 Luc 17.6 Matthieu 21.21 Luc 1.37 Luc 18.27
21 [Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.]
22 Nao walipokuwa wakikaa Galilaya, Yesu akawaambia, Mwana wa Adamu anakwenda kutiwa katika mikono ya watu, nao watamwua, na siku ya tatu atafufuka.
Matthieu 16.21 Matthieu 20.17-20.18 Marc 9.30-9.32 Matthieu 16.28 Luc 24.26
23 Wakasikitika sana.
Matthieu 16.21 Zacharie 13.7 Jean 16.20-16.22 Marc 8.31 Esaïe 53.10-53.12
24 Hata walipofika Kapernaumu, wale watozao nusu-shekeli walimwendea Petro, wakasema, Je! Mwalimu wenu hatoi nusu-shekeli? Akasema, Hutoa.
Exode 30.13 Exode 38.26 Marc 9.33
25 Naye alipoingia nyumbani, Yesu alitangulia kumwuliza, akisema, Waonaje, Simoni? Wafalme wa dunia hutwaa kodi ama ushuru kwa watu gani? Kwa wana wao au kwa wageni?
Matthieu 22.21 Matthieu 22.17 Matthieu 22.19 Romains 13.6-13.7 Matthieu 3.15
26 Naye aliposema, Kwa wageni, Yesu alimwambia, Basi, kama ni hivyo, wana ni mahuru.
27 Lakini tusije tukawakwaza, enenda baharini ukatupe ndoana, ukatwae samaki yule azukaye kwanza; na ukifumbua mdomo wake utaona shekeli ichukue hiyo ukawape kwa ajili yangu na kwa ajili yako.
Jonas 1.17 Jean 6.61 Jacques 2.5 1 Corinthiens 9.19-9.22 Tite 2.7-2.8

Cette Bible est dans le domaine public.