Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Nombres 25.14
Bible en Swahili de l’est


Idolâtrie dans les plaines de Moab

1 Basi Israeli akakaa Shitimu, kisha watu wakaanza kuzini pamoja na wanawake wa Moabu;
Josué 2.1 Michée 6.5 Nombres 33.49 1 Corinthiens 10.8 Nombres 31.15-31.16
2 kwa kuwa waliwaalika hao watu waende sadakani, sadaka walizowachinjia miungu yao; watu wakala chakula, wakaisujudu hiyo miungu yao.
1 Corinthiens 10.20 Exode 20.5 Exode 34.15-34.16 1 Rois 11.1-11.8 Josué 22.17
3 Ikawa Israeli kujiungamanisha na Baal-peori; hasira za Bwana zikawaka juu ya Israeli.
Osée 9.10 Josué 22.17 Psaumes 106.28-106.29 Juges 2.20 Deutéronome 4.3-4.4
4 Kisha Bwana akamwambia Musa, Watwae wakuu wote wa hao watu, ukamtungikie Bwana watu hao mbele ya jua, ili kwamba hizo hasira kali za Bwana ziwaondokee Israeli.
Deutéronome 13.17 Deutéronome 4.3 2 Samuel 21.6 Deutéronome 21.23 Nombres 25.11
5 Basi Musa akawaambia waamuzi wa Israeli, Waueni kila mtu watu wake waliojiungamanisha na Baal-peori.
Exode 18.21 Deutéronome 13.13 Deutéronome 13.15 Exode 22.20 Exode 18.25-18.26
6 Na tazama, mtu mmoja miongoni mwa wana wa Israeli akaja na kuwaletea nduguze mwanamke Mmidiani mbele ya macho ya Musa, na mbele ya macho ya mkutano wote wa wana wa Israeli, hapo walipokuwa walia mbele ya mlango wa hema ya kukutania.
Joël 2.17 Nombres 22.4 Nombres 25.14-25.15 Jérémie 3.3 Esdras 10.6-10.9
7 Naye Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa Haruni kuhani, alipoona jambo hilo, akaondoka hapo katikati ya mkutano, akashika fumo mkononi mwake;
Exode 6.25 Juges 20.28 Psaumes 106.30 Josué 22.30-22.31 1 Samuel 18.10-18.11
8 akamwandama huyo mtu wa Israeli na kuingia ndani ya hema nyuma yake, naye akawachoma wote wawili kwa fumo lake, yule mume wa Israeli na huyo mwanamke kati ya tumbo lake. Basi pigo likazuiwa kwao wana wa Israeli.
Nombres 16.46-16.48 Nombres 25.11 Psaumes 106.29-106.31 1 Chroniques 21.22 2 Samuel 24.25
9 Nao waliokufa kwa hilo pigo walikuwa watu elfu ishirini na nne hesabu yao.
1 Corinthiens 10.8 Nombres 16.49-16.50 Deutéronome 4.3-4.4 Nombres 31.16 Nombres 14.37
10 Kisha Bwana akanena na Musa, akamwambia,
11 Finehasi, mwana wa Eleazari, mwana wa Haruni kuhani, amezigeuza hasira zangu zisiwe juu ya wana Wa Israeli, kwa kuwa alikuwa na wivu kati yao kwa wivu wangu mimi, hata nisiwaangamize wana wa Israeli katika wivu wangu.
Psaumes 78.58 Deutéronome 32.16 Deutéronome 32.21 1 Rois 14.22 Sophonie 3.8
12 Basi kwa hiyo, sema, Tazama, nampa yeye agano langu la amani;
Malachie 2.4-2.5 Esaïe 54.10 Nombres 13.29 Ezéchiel 34.25 Malachie 3.1
13 tena kwake yeye, na kizazi chake baada yake, litakuwa agano la ukuhani wa milele; kwa sababu alikuwa na wivu kwa ajili ya Mungu wake, na kuwafanyia upatanisho wana wa Israeli.
Exode 40.15 Psaumes 106.31 Jérémie 33.22 Jérémie 33.18 1 Chroniques 6.4-6.15
14 Basi jina la Mwisraeli huyo aliyeuawa pamoja na yule mwanamke Mmidiani, aliitwa Zimri, mwana wa Salu, mkuu wa nyumba ya baba zake, katika kabila la Simeoni.
Nombres 25.4-25.5 2 Chroniques 19.7 Nombres 1.23 Nombres 26.14
15 Na jina la huyo mwanamke Mmidiani aliyeuawa, aliitwa Kozbi, binti Suri; naye alikuwa kichwa cha watu wa nyumba ya baba zake huko Midiani
Nombres 31.8 Josué 13.21 Nombres 25.18
16 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
17 Wasumbue Wamidiani, na kuwapiga;
Apocalypse 18.6 Nombres 31.1-31.3
18 kwa sababu wao wawasumbua ninyi kwa hila zao, ambazo kwa hizo wamewadanganya ninyi katika jambo la Peori, na katika jambo la huyo Kozbi, binti wa mkuu wa Midiani, umbu lao, huyo aliyeuawa siku hiyo ya pigo katika jambo la Peori.
Apocalypse 2.14 2 Pierre 2.18 2 Pierre 2.14-2.15 Exode 32.21 Nombres 31.15-31.16

Cette Bible est dans le domaine public.