Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Nombres 25.13
Bible en Swahili de l’est


Idolâtrie dans les plaines de Moab

1 Basi Israeli akakaa Shitimu, kisha watu wakaanza kuzini pamoja na wanawake wa Moabu;
Josué 2.1 Nombres 33.49 1 Corinthiens 10.8 Michée 6.5 Nombres 31.15-31.16
2 kwa kuwa waliwaalika hao watu waende sadakani, sadaka walizowachinjia miungu yao; watu wakala chakula, wakaisujudu hiyo miungu yao.
1 Corinthiens 10.20 Exode 20.5 Exode 34.15-34.16 Psaumes 106.28 Osée 9.10
3 Ikawa Israeli kujiungamanisha na Baal-peori; hasira za Bwana zikawaka juu ya Israeli.
Osée 9.10 Josué 22.17 Psaumes 106.28-106.29 Nombres 25.5 Juges 2.14
4 Kisha Bwana akamwambia Musa, Watwae wakuu wote wa hao watu, ukamtungikie Bwana watu hao mbele ya jua, ili kwamba hizo hasira kali za Bwana ziwaondokee Israeli.
Deutéronome 13.17 Deutéronome 4.3 2 Samuel 21.6 Deutéronome 21.23 Nombres 25.11
5 Basi Musa akawaambia waamuzi wa Israeli, Waueni kila mtu watu wake waliojiungamanisha na Baal-peori.
Exode 18.21 Exode 18.25-18.26 Exode 32.27-32.28 1 Rois 18.40 Deutéronome 13.9
6 Na tazama, mtu mmoja miongoni mwa wana wa Israeli akaja na kuwaletea nduguze mwanamke Mmidiani mbele ya macho ya Musa, na mbele ya macho ya mkutano wote wa wana wa Israeli, hapo walipokuwa walia mbele ya mlango wa hema ya kukutania.
Joël 2.17 Nombres 22.4 2 Pierre 2.13-2.15 Jérémie 36.23 Jude 1.13
7 Naye Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa Haruni kuhani, alipoona jambo hilo, akaondoka hapo katikati ya mkutano, akashika fumo mkononi mwake;
Exode 6.25 Psaumes 106.30 Josué 22.30-22.31 1 Samuel 18.10-18.11 1 Samuel 19.9
8 akamwandama huyo mtu wa Israeli na kuingia ndani ya hema nyuma yake, naye akawachoma wote wawili kwa fumo lake, yule mume wa Israeli na huyo mwanamke kati ya tumbo lake. Basi pigo likazuiwa kwao wana wa Israeli.
Nombres 16.46-16.48 Psaumes 106.29-106.31 1 Chroniques 21.22 2 Samuel 24.25 Nombres 25.5
9 Nao waliokufa kwa hilo pigo walikuwa watu elfu ishirini na nne hesabu yao.
1 Corinthiens 10.8 Nombres 16.49-16.50 Nombres 31.16 Nombres 14.37 Nombres 25.4-25.5
10 Kisha Bwana akanena na Musa, akamwambia,
11 Finehasi, mwana wa Eleazari, mwana wa Haruni kuhani, amezigeuza hasira zangu zisiwe juu ya wana Wa Israeli, kwa kuwa alikuwa na wivu kati yao kwa wivu wangu mimi, hata nisiwaangamize wana wa Israeli katika wivu wangu.
Deutéronome 32.21 Psaumes 78.58 Deutéronome 32.16 Exode 20.5 2 Corinthiens 11.2
12 Basi kwa hiyo, sema, Tazama, nampa yeye agano langu la amani;
Malachie 2.4-2.5 Nombres 13.29 Ezéchiel 34.25 Malachie 3.1 Esaïe 54.10
13 tena kwake yeye, na kizazi chake baada yake, litakuwa agano la ukuhani wa milele; kwa sababu alikuwa na wivu kwa ajili ya Mungu wake, na kuwafanyia upatanisho wana wa Israeli.
Psaumes 106.31 Jérémie 33.22 Jérémie 33.18 1 Chroniques 6.4-6.15 Exode 40.15
14 Basi jina la Mwisraeli huyo aliyeuawa pamoja na yule mwanamke Mmidiani, aliitwa Zimri, mwana wa Salu, mkuu wa nyumba ya baba zake, katika kabila la Simeoni.
2 Chroniques 19.7 Nombres 1.23 Nombres 26.14 Nombres 25.4-25.5
15 Na jina la huyo mwanamke Mmidiani aliyeuawa, aliitwa Kozbi, binti Suri; naye alikuwa kichwa cha watu wa nyumba ya baba zake huko Midiani
Nombres 31.8 Josué 13.21 Nombres 25.18
16 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
17 Wasumbue Wamidiani, na kuwapiga;
Nombres 31.1-31.3 Apocalypse 18.6
18 kwa sababu wao wawasumbua ninyi kwa hila zao, ambazo kwa hizo wamewadanganya ninyi katika jambo la Peori, na katika jambo la huyo Kozbi, binti wa mkuu wa Midiani, umbu lao, huyo aliyeuawa siku hiyo ya pigo katika jambo la Peori.
Apocalypse 2.14 Exode 32.21 Nombres 31.15-31.16 2 Corinthiens 11.3 Genèse 26.10

Cette Bible est dans le domaine public.