Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Zacharie 9.10
Bible en Swahili de l’est


L’avenir messianique

Venue du roi et victoire sur les nations

1 Ufunuo wa neno la Bwana, lililosemwa juu ya nchi ya Hadraki, na Dameski itakuwa mahali pake pa kustarehe; kwa maana jicho la mwanadamu na la kabila zote za Israeli linamwelekea Bwana;
Jérémie 49.23-49.27 Amos 1.3-1.5 Amos 3.12 Esaïe 17.1-17.3 Jérémie 16.19
2 na Hamathi pia iliyo mpakani mwake; na Tiro, na Sidoni, kwa maana ana akili nyingi.
Ezéchiel 28.12 Jérémie 49.23 Ezéchiel 28.2-28.5 Nombres 13.21 2 Rois 25.21
3 Na Tiro alijijengea ngome, akakusanya fedha kama mchanga, dhahabu safi kama matope ya njia kuu.
Josué 19.29 Job 27.16 Ezéchiel 28.4-28.5 2 Samuel 24.7 Ezéchiel 27.33
4 Tazama, Bwana atamwondolea mali zake, naye ataupiga uwezo wake alio nao baharini, naye mwenyewe atateketezwa kwa moto.
Ezéchiel 28.18 Ezéchiel 26.17 Amos 1.10 Proverbes 10.2 Joël 3.8
5 Ashkeloni ataona haya na kuogopa; Gaza pia, naye atafadhaika sana; na Ekroni, kwa maana taraja lake litatahayarika; na mfalme ataangamia toka Gaza, na Ashkeloni atakuwa hana watu.
Jérémie 47.4-47.7 Jérémie 51.8-51.9 Philippiens 1.20 Ezéchiel 26.15-26.21 Esaïe 20.5-20.6
6 Na mwana wa haramu atatawala huko Ashdodi, nami nitakatilia mbali kiburi cha Wafilisti.
Amos 1.8 Sophonie 2.10 Ecclésiaste 6.2 Esaïe 2.12-2.17 1 Pierre 5.5
7 Nami nitaondoa damu yake kinywani mwake, na machukizo yake nitayatoa katika meno yake; yeye naye atakuwa ni mabaki kwa Mungu wetu; naye atakuwa kama mtu mkuu katika Yuda, na Ekroni kama Myebusi.
1 Chroniques 21.15-22.1 Esaïe 19.23-19.25 Esaïe 60.14-60.16 Jérémie 49.39 Amos 3.12
8 Nami nitapiga kambi yangu pande zote za nyumba yangu ili kuwapinga adui, mtu awaye yote asipite ndani yake wala kurudi; wala mtu aoneaye hatapita tena kati yao; kwa maana sasa nimeona kwa macho yangu.
Esaïe 52.1 Esaïe 54.14 Esaïe 60.18 Zacharie 2.1-2.13 Daniel 11.40-11.45
9 Furahi sana, Ee binti Sayuni; Piga kelele, Ee binti Yerusalemu; Tazama, mfalme wako anakuja kwako; Ni mwenye haki, naye ana wokovu; Ni mnyenyekevu, amepanda punda, Naam, mwana-punda, mtoto wa punda.
Sophonie 3.14-3.15 Jérémie 23.5-23.6 Zacharie 2.10 Matthieu 11.29 Esaïe 9.6-9.7
10 Na gari la vita nitaliondoa liwe mbali na Efraimu, na farasi awe mbali na Yerusalemu, na upinde wa vita utaondolewa mbali; naye atawahubiri mataifa yote habari za amani; na mamlaka yake yatakuwa toka bahari hata bahari, na toka Mto hata miisho ya dunia.
Osée 1.7 Osée 2.18 Colossiens 1.20-1.21 2 Corinthiens 10.4-10.5 Michée 5.4
11 Na kwa habari zako wewe, kwa sababu ya damu ya agano lako, nimewatoa wafungwa wako katika shimo lile lisilo na maji.
Exode 24.8 Esaïe 51.14 Esaïe 42.7 Esaïe 61.1 Matthieu 26.28
12 Irudieni ngome, enyi wafungwa wa tumaini; hata hivi leo nasema ya kwamba nitakurudishia maradufu.
Lamentations 3.21-3.22 Job 42.10 Jérémie 31.17 Hébreux 6.18 Esaïe 61.7
13 Maana nimejipindia Yuda, nimeujaza upinde wangu Efraimu; nami nitawaondokesha wana wako, Ee Sayuni, wapigane na wana wako, Ee Uyunani, nami nitakufanya wewe kuwa kama upanga wa shujaa.
Esaïe 49.2 Psaumes 45.3 Zacharie 10.3-10.7 Psaumes 149.6 Hébreux 4.12
14 Naye Bwana ataonekana juu yao, Na mshale wake utatoka kama umeme; Na Bwana MUNGU ataipiga tarumbeta, Naye atakwenda kwa pepo za kisulisuli za kusini.
Esaïe 21.1 Esaïe 27.13 Psaumes 18.14 Esaïe 66.15 Zacharie 2.5
15 Bwana wa majeshi atawalinda; Nao watakula na kuyakanyaga mawe ya teo; Nao watakunywa na kufanya kelele kama kwa divai; Nao watajazwa kama mabakuli, kama pembe za madhabahu.
Zacharie 12.6 Zacharie 10.5 Exode 27.2 Psaumes 78.65 Lévitique 4.25
16 Na Bwana, Mungu wao, atawaokoa siku hiyo, Kama kundi la watu wake; Kwa maana watakuwa kama vito vya taji, Vikimeta-meta juu ya nchi yake.
Esaïe 62.3 Psaumes 100.3 Michée 5.4 Esaïe 11.10-11.12 Zacharie 8.23
17 Maana wema wake, jinsi ulivyo mwingi! Na uzuri wake, jinsi ulivyo mwingi! Nafaka itawasitawisha vijana wanaume, Na divai mpya vijana wanawake.
Esaïe 62.8-62.9 Esaïe 33.17 Romains 5.20 Exode 15.11 Ephésiens 3.18-3.19

Cette Bible est dans le domaine public.