Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Sophonie 3.13
Bible en Swahili de l’est


Causes du jugement de Jérusalem

1 Ole wake yeye aliyeasi na kutiwa unajisi, mji wa udhalimu!
Jérémie 6.6 Esaïe 59.13 Ezéchiel 22.7 Esaïe 5.7 Michée 2.2
2 Hakuitii sauti; hakukubali kurudiwa; hakumwamini Bwana; hakumkaribia Mungu wake.
Jérémie 5.3 Jérémie 22.21 Psaumes 78.22 Jérémie 2.30 Jérémie 7.23-7.28
3 Wakuu wake walio ndani yake ni simba wangurumao; makadhi wake ni mbwa-mwitu wa jioni; hawasazi kitu cho chote hata siku ya pili.
Habakuk 1.8 Jérémie 5.6 Proverbes 28.15 Jérémie 22.17 Michée 3.9-3.11
4 Manabii wake ni watu hafifu, wadanganyifu; makuhani wake wamepatia unajisi patakatifu, wameifanyia sheria udhalimu.
Ezéchiel 22.26 Malachie 2.8 Osée 9.7 Jérémie 14.13-14.15 Esaïe 9.15
5 Bwana kati yake ni mwenye haki; hatatenda uovu; kila asubuhi hudhihirisha hukumu yake, wala hakomi; bali mtu asiye haki hajui kuona haya.
Deutéronome 32.4 Sophonie 3.15 Ecclésiaste 3.16-3.17 Psaumes 99.3-99.4 Sophonie 3.17
6 Nimekatilia mbali mataifa, buruji zao zina ukiwa; nimeziharibu njia kuu zao, hata hapana mmoja apitaye; miji yao imeangamizwa; hamna mtu hata mmoja, wala hapana akaaye huko.
Jérémie 25.9-25.11 Esaïe 37.36 Esaïe 19.1-19.25 Esaïe 37.11-37.13 Lévitique 26.31
7 Nalisema, Hakika utaniogopa, utakubali kurudiwa; ili yasikatiliwe mbali makao yake, sawasawa ya yote niliyoagiza katika habari zake; lakini waliondoka mapema na kuyaharibu matendo yao yote.
Osée 9.9 Jérémie 7.7 Jérémie 36.3 Sophonie 3.2 2 Chroniques 32.1-32.2
8 Basi ningojeni, asema Bwana, hata siku ile nitakapoondoka kuteka mateka; maana nimeazimia kuwakusanya mataifa, ili nizikutanishe falme, nipate kuwamwagia ghadhabu yangu; naam, ukali wote wa hasira yangu; kwa maana dunia yote itateketezwa kwa moto wa wivu wangu.
Joël 3.2 Sophonie 1.18 2 Pierre 3.10 Psaumes 27.14 Habakuk 2.3

Bénédictions en perspective

9 Maana hapo ndipo nitakapowarudishia mataifa lugha iliyo safi, wapate kuliitia jina la Bwana, wamtumikie kwa nia moja.
Esaïe 19.18 Psaumes 22.27 Habakuk 2.14 Genèse 11.1 Actes 2.4-2.13
10 Maana toka nchi iliyo mbali na mito ya Kushi, waniombao dua, yaani, binti za watu wangu waliotawanyika, wataleta matoleo yangu.
Psaumes 68.31 Esaïe 11.11 Esaïe 18.1 Romains 15.16 1 Pierre 1.1
11 Siku ile hutatahayarikia matendo yako yote uliyoniasi; maana hapo nitawaondoa watu wako wanaotakabari na kujivuna, wasiwe kati yako, wala hutatakabari tena katika mlima wangu mtakatifu.
Esaïe 54.4 Esaïe 11.9 Joël 2.26-2.27 Matthieu 3.9 Jérémie 7.4
12 Lakini nitasaza ndani yako watu walioonewa na maskini, nao watalitumainia jina la Bwana.
Esaïe 14.32 Nahum 1.7 Zacharie 13.8-13.9 Matthieu 5.3 Esaïe 50.10
13 Mabaki ya Israeli hawatatenda uovu, wala kusema uongo; wala ulimi wa hadaa hautaonekana kinywani mwao; kwa maana watakula na kulala, wala hapana mtu atakayewaogofya.
Apocalypse 14.5 Sophonie 2.7 Michée 4.7 Esaïe 60.21 Ezéchiel 34.13-34.15
14 Imba, Ee binti Sayuni; piga kelele, Ee Israeli; Furahi na kushangilia kwa moyo wako wote, Ee binti Yerusalemu.
Esaïe 12.6 Esaïe 54.1 Luc 2.10-2.14 Jérémie 33.11 Psaumes 126.2-126.3
15 Bwana ameziondoa hukumu zako, Amemtupa nje adui yako; Mfalme wa Israeli, naam, yeye Bwana, yu katikati yako; Hutaogopa uovu tena.
Esaïe 51.22 Zacharie 10.6-10.7 Sophonie 3.5 Jean 1.49 Ezéchiel 39.29
16 Katika siku ile Yerusalemu utaambiwa, Usiogope, Ee Sayuni; mikono yako isilegee.
Hébreux 12.12 Esaïe 35.3-35.4 Apocalypse 2.3 Aggée 2.4-2.5 Esaïe 40.9
17 Bwana, Mungu wako, yu katikati yako shujaa awezaye kuokoa; Atakushangilia kwa furaha kuu, Atakutuliza katika upendo wake, Atakufurahia kwa kuimba.
Hébreux 7.25 Psaumes 149.4 Sophonie 3.15 Esaïe 62.4-62.5 Jérémie 32.41
18 Nitawakusanya wanaousikitikia mkutano wa ibada, hao waliokuwa wa kwako; ambao mzigo uliokuwa juu yake ulikuwa fedheha kwao.
Psaumes 42.2-42.4 Lamentations 1.4 Psaumes 43.3 Psaumes 84.1-84.2 Ezéchiel 34.13
19 Tazama, wakati huo nitawapatiliza watu wote wanaokutesa; nami nitamponya yeye achechemeaye, nami nitamkusanya yeye aliyefukuzwa; nami nitawafanya kuwa sifa na jina, hao ambao fedheha yao ilikuwa katika dunia yote.
Esaïe 60.14 Jérémie 33.9 Michée 4.6-4.7 Zacharie 2.8-2.9 Esaïe 62.7
20 Wakati huo nitawaingizeni, na wakati huo nitawakusanya; kwa maana nitawafanya ninyi kuwa sifa na jina, miongoni mwa watu wote wa dunia, nitakapowarudisha wafungwa wenu mbele ya macho yenu, asema Bwana.
Jérémie 29.14 Joël 3.1 Sophonie 3.19 Ezéchiel 37.21 Malachie 3.12

Cette Bible est dans le domaine public.