Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Lévitique 23.26
Bible en Swahili de l’est


Les rendez-vous fixés par l’Éternel

1 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
2 Nena na wana wa Israeli, na kuwaambia, Sikukuu za Bwana, ambazo mtazipigia mbiu kuwa ni makusanyiko matakatifu; hizi ni sikukuu zangu.
Lévitique 23.37 Lévitique 23.4 Joël 2.15 Osée 2.11 Nombres 29.39

Le sabbat

3 Mtafanya kazi siku sita; lakini siku ya saba ni Sabato ya kustarehe kabisa, kusanyiko takatifu; msifanye kazi ya namna yo yote; ni Sabato kwa Bwana katika makao yenu yote.
Lévitique 19.3 Exode 23.12 Luc 13.14 Exode 34.21 Exode 20.8-20.11

La Pâque et la fête des pains sans levain

4 Sikukuu za Bwana ni hizi, ni makusanyiko matakatifu, ambayo mtayapigia mbiu kwa nyakati zake.
Lévitique 23.2 Lévitique 23.37 Exode 23.14
5 Mwezi wa kwanza, siku ya kumi na nne ya mwezi wakati wa jioni, ni pasaka ya Bwana.
Josué 5.10 Deutéronome 16.1-16.8 Nombres 28.16-28.17 Exode 12.2-12.14 Matthieu 26.17
6 Na siku ya kumi na tano ya mwezi ule ule ni sikukuu kwa Bwana ya mkate usiotiwa chachu; mtaila mikate isiyochachwa muda wa siku saba.
Exode 34.18 Deutéronome 16.8 Exode 12.15-12.16 Nombres 28.17-28.18 Exode 13.6-13.7
7 Siku ya kwanza mtakuwa na kusanyiko takatifu msifanye kazi yo yote ya utumishi.
Lévitique 23.8 Lévitique 23.21 Nombres 28.18-28.25 Lévitique 23.35-23.36 Lévitique 23.25
8 Lakini mtasongeza sadaka kwa Bwana kwa njia ya moto siku saba; siku ya saba ni kusanyiko takatifu; msifanye kazi yo yote ya utumishi.

La fête des prémices et la fête des moissons

9 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
10 Nena na wana wa Israeli, uwaambie, Hapo mtakapokuwa mmekwisha ingia hiyo nchi niwapayo, na kuyavuna mavuno yake, ndipo mtakapomletea kuhani mganda wa malimbuko ya mavuno yenu;
Exode 23.19 Exode 34.26 Nombres 28.26 Deutéronome 16.9 Lévitique 2.12-2.16
11 naye atautikisa mganda mbele za Bwana ili kwamba ukubaliwe kwa ajili yenu; siku ya pili baada ya Sabato kuhani atautikisa.
Exode 29.24 Lévitique 10.14 Lévitique 9.21
12 Na siku hiyo mtakayoutikisa mganda, mtamsongeza mwana-kondoo wa kiume mkamilifu wa mwaka wa kwanza awe sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana.
Lévitique 1.10 1 Pierre 1.19 Hébreux 10.10-10.12
13 Na sadaka yake ya unga itakuwa sehemu za kumi mbili za efa za unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, ni kafara iliyosongezwa kwa Bwana kwa moto kuwa harufu ya kupendeza; na sadaka yake ya kinywaji itakuwa ni divai, robo ya hini.
Lévitique 2.14-2.16 Ezéchiel 4.11 Joël 1.13 Joël 1.9 Exode 29.40-29.41
14 Nanyi msile mkate, wala bisi, wala masuke machanga, hata siku iyo hiyo, hata mtakapokuwa mmekwisha kuleta sadaka ya Mungu wenu; hii ni amri ya milele katika vizazi vyenu katika makao yenu yote.
Exode 34.26 Lévitique 10.11 Lévitique 19.23-19.25 Nombres 15.20-15.21 Josué 5.11-5.12
15 Nanyi mtajihesabia tangu siku ya pili baada ya Sabato, tangu siku hiyo mliyouleta mganda wa sadaka ya kutikiswa; zitatimia Sabato saba;
Lévitique 23.10-23.11 Lévitique 25.8 Deutéronome 16.9-16.10 Exode 34.22 Nombres 28.26
16 hata siku ya pili ya hiyo Sabato ya saba mtahesabu siku hamsini; nanyi mtamsongezea Bwana sadaka ya unga mpya.
Actes 2.1 Nombres 28.26
17 Mtatoa katika makao yenu mikate miwili ya kutikiswa, itakuwa ya sehemu za kumi mbili za efa; itakuwa ya unga mwembamba, itaokwa na chachu, iwe malimbuko kwa Bwana.
Lévitique 23.10 Exode 34.22 Exode 23.19 Exode 34.26 Nombres 28.26
18 Nanyi, pamoja na hiyo mikate, mtasongeza wana-kondoo saba, walio wakamilifu, wa mwaka wa kwanza, na ng’ombe mume mmoja, na kondoo waume wawili; watakuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana, pamoja na sadaka yao ya unga, na sadaka zao za kinywaji, sadaka ya harufu ya kupendeza iliyosongezwa kwa Bwana kwa njia ya moto.
Lévitique 23.12-23.13 Malachie 1.13-1.14 Nombres 15.4-15.12 Nombres 28.27-28.31
19 Nanyi mtasongeza mbuzi mume mmoja kuwa sadaka ya dhambi, na wana-kondoo wawili waume wa mwaka wa kwanza kuwa dhabihu ya sadaka za amani.
Nombres 28.30 Lévitique 4.23-4.28 Nombres 15.24 Lévitique 3.1-3.17 2 Corinthiens 5.21
20 Kisha kuhani atawatikisa pamoja na hiyo mikate ya malimbuko kuwa sadaka ya kutikiswa mbele za Bwana, pamoja na wale wana-kondoo wawili; watakuwa watakatifu kwa Bwana, wawe wa huyo kuhani.
Deutéronome 18.4 Lévitique 10.14-10.15 Exode 29.24 Lévitique 23.17 Lévitique 8.29
21 Nanyi mtapiga mbiu siku iyo hiyo; kutakuwa na kusanyiko takatifu kwenu; msifanye kazi yo yote ya utumishi; ni amri ya milele katika makao yenu yote, katika vizazi vyenu.
Lévitique 23.2 Lévitique 23.4 Nombres 18.23 Genèse 17.7 Lévitique 23.14
22 Nanyi hapo mtakapovuna mavuno ya nchi yenu, usivune kabisa kabisa pembe za shamba lako, wala msiyakusanye masazo ya mavuno yako; utayaacha kwa ajili ya huyo maskini, na mgeni; mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.
Lévitique 19.9-19.10 Deutéronome 24.19-24.21 Luc 11.41 Deutéronome 16.11-16.14 Proverbes 11.24-11.25

La fête des trompettes

23 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
24 Nena na wana wa Israeli, uwaambie, Mwezi wa saba, siku ya kwanza ya mwezi, kutakuwa na kustarehe kabisa kwenu, ni ukumbusho wa kuzipiga baragumu, ni kusanyiko takatifu.
Lévitique 25.9 1 Corinthiens 15.52 Nombres 10.9-10.10 Psaumes 98.6 2 Chroniques 5.13
25 Msifanye kazi yo yote ya utumishi; nanyi mtasongeza sadaka kwa Bwana kwa njia ya moto.
Lévitique 23.21

Le jour des expiations

26 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
27 Lakini siku ya kumi ya mwezi huo wa saba ni siku ya upatanisho; itakuwa kusanyiko takatifu kwenu, nanyi mtazitesa nafsi zenu; nanyi mtasongeza sadaka kwa Bwana kwa njia ya moto.
Lévitique 16.15 Lévitique 16.29-16.31 Lévitique 16.24 Exode 30.10 Lévitique 16.11
28 Nanyi msifanye kazi yo yote siku hiyo; kwa kuwa ni siku ya upatanisho, ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu mbele za Bwana, Mungu wenu.
Lévitique 16.34 Hébreux 10.10 Esaïe 53.10 1 Jean 5.6 Hébreux 10.14
29 Kwa kuwa mtu awaye yote asiyejitesa mwenyewe siku iyo hiyo, atakatiliwa mbali na watu wake.
Genèse 17.14 Nombres 5.2 Lévitique 23.32 Ezéchiel 7.16 Jérémie 31.9
30 Na mtu ye yote afanyaye kazi ya namna yo yote siku hiyo, mtu huyo nitamwangamiza atoke katika watu wake.
Lévitique 20.3 Lévitique 20.5-20.6 Ezéchiel 14.9 Genèse 17.14 1 Corinthiens 3.17
31 Msifanye kazi ya namna yo yote; ni amri ya milele katika vizazi vyenu, katika makao yenu yote.
32 Itakuwa kwenu sabato ya kustarehe kabisa, nanyi mtazitesa nafsi zenu; siku ya kenda ya mwezi wakati wa jioni, tangu jioni hata jioni, mtaishika hiyo Sabato yenu.
Esaïe 57.15 Hébreux 4.11 Esaïe 61.3 Esaïe 58.3-58.7 Psaumes 51.17

La fête des tentes

33 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
34 Nena na wana wa Israeli, uwaambie, Siku ya kumi na tano ya mwezi huo wa saba ni sikukuu ya vibanda muda wa siku saba kwa Bwana.
Jean 7.2 Esdras 3.4 Néhémie 8.14 Nombres 29.12 Jean 1.14
35 Siku ya kwanza kutakuwa na kusanyiko takatifu; msifanye kazi yo yote ya utumishi.
Lévitique 23.7-23.8 Lévitique 23.24-23.25
36 Mtamsongezea Bwana sadaka kwa moto siku saba; siku ya nane kutakuwa na kusanyiko takatifu kwenu; nanyi mtamsongezea Bwana sadaka kwa moto; ni mkutano wa makini huu; msifanye kazi yo yote ya utumishi.
Néhémie 8.18 Jean 7.37 Joël 2.15 Deutéronome 16.8 Joël 1.14
37 Sikukuu za Bwana ni hizi, ambazo mtazipigia mbiu ya kuwa ni makusanyiko matakatifu, ili mmsongezee Bwana sadaka kwa moto, sadaka ya kuteketezwa, na sadaka ya unga, na dhabihu, na sadaka za kinywaji, kila sadaka kwa siku yake;
Lévitique 23.2 Lévitique 23.4 Ecclésiaste 3.1 Deutéronome 16.16-16.17
38 zaidi ya hizo Sabato za Bwana, na zaidi ya matoleo yenu, na zaidi ya hizo nadhiri zenu zote, na zaidi ya sadaka zenu za hiari, ambazo mwampa Bwana.
Nombres 29.39 Genèse 2.2-2.3 1 Chroniques 29.3-29.8 Exode 20.8-20.11 2 Chroniques 35.7-35.8
39 Lakini siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba, hapo mtakapokuwa mmekwisha kuyachuma mavuno ya nchi, mtaweka sikukuu ya Bwana muda wa siku saba; siku ya kwanza kutakuwa na kustarehe kabisa, na siku ya nane kutakuwa na kustarehe kabisa.
Exode 23.16 Deutéronome 16.13 Lévitique 23.34 Lévitique 23.24 Lévitique 23.36
40 Nanyi siku ya kwanza mtajipatia matunda ya miti mizuri, na makuti ya mitende, na matawi ya miti minene, na mierebi ya vijitoni; nanyi mtafurahi mbele za Bwana, Mungu wenu, muda wa siku saba.
Deutéronome 16.14-16.15 Néhémie 8.14-8.17 Romains 5.11 Matthieu 21.8 Jean 16.22
41 Nanyi mtaishika kuwa sikukuu kwa Bwana muda wa siku saba katika mwaka; ni amri ya milele katika vizazi vyenu; mtaishika katika mwezi wa saba.
Nombres 29.12 Néhémie 8.18
42 Mtakaa katika vibanda muda wa siku saba; wazalia wote wa Israeli watakaa katika vibanda;
Néhémie 8.14-8.17 2 Corinthiens 5.1 Genèse 33.17 Jérémie 35.10 Nombres 24.2
43 ili vizazi vyenu vipate kujua ya kuwa niliwaketisha wana wa Israeli katika vibanda, hapo nilipowaleta kutoka nchi ya Misri; mimi ndimi Bwana Mungu wenu.
Deutéronome 31.10-31.13 Exode 13.14 Psaumes 78.5-78.6
44 Naye Musa akawaambia wana wa Israeli hizo sikukuu za Bwana.
Lévitique 21.24 Matthieu 18.20 Lévitique 23.1-23.2

Cette Bible est dans le domaine public.