Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Osée 4.4
Bible en Swahili de l’est


Péché et jugement d’Israël

Reproches contre l’idolâtrie

1 Lisikieni neno la Bwana, enyi wana wa Israeli; kwa maana Bwana ana mateto nao wakaao katika nchi, kwa sababu hapana kweli, wala fadhili, wala kumjua Mungu katika nchi.
Jérémie 4.22 Michée 6.2 Esaïe 3.13-3.14 Jérémie 25.31 Osée 12.2
2 Hapana neno ila kuapa kwa uongo, na kuvunja ahadi, na kuua, na kuiba, na kuzini; huruka mpaka, na damu hugusana na damu.
Osée 6.9 Osée 7.1 Jérémie 6.7 Jérémie 7.6-7.10 Jérémie 5.26-5.27
3 Kwa ajili ya hayo nchi itaomboleza, na kila mtu akaaye ndani yake atadhoofika, pamoja na wanyama wa kondeni na ndege wa angani; naam, samaki wa baharini pia wataondolewa.
Sophonie 1.3 Amos 5.16 Ezéchiel 38.20 Jérémie 4.27-4.28 Jérémie 4.25
4 Walakini asishindane mtu, wala mtu asikemee; maana watu wako ni kama wao washindanao na kuhani.
Deutéronome 17.12 Osée 4.17 Amos 5.13 Jérémie 18.18 Ezéchiel 3.26
5 Na wewe utajikwaa wakati wa mchana, na nabii naye atajikwaa pamoja nawe wakati wa usiku; nami nitamwangamiza mama yako.
Jérémie 15.8 Osée 2.2 Ezéchiel 13.9-13.16 Ezéchiel 16.44-16.45 Jérémie 6.4-6.5
6 Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa; kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa, mimi nami nitakukataa wewe, usiwe kuhani kwangu mimi; kwa kuwa umeisahau sheria ya Mungu wako, mimi nami nitawasahau watoto wako.
Esaïe 5.13 Proverbes 19.2 Esaïe 17.10 Esaïe 1.3 Osée 8.14
7 Kadiri walivyozidishwa, kwa kadiri iyo hiyo walinitenda dhambi; nami nitageuza utukufu wao kuwa aibu.
Osée 13.6 1 Samuel 2.30 Malachie 2.9 Habakuk 2.16 Philippiens 3.19
8 Hujilisha dhambi ya watu wangu, hujifurahisha moyo kwa uovu wao.
Lévitique 6.26 Esaïe 56.11 Michée 3.11 Malachie 1.10 Romains 16.18
9 Hata itakuwa, kama walivyo watu, ndivyo atakavyokuwa kuhani; nami nitawaadhibu kwa ajili ya njia zao, na kuwalipa kwa matendo yao.
Esaïe 24.2 Jérémie 5.31 Osée 9.9 Psaumes 109.17-109.18 Jérémie 23.11-23.12
10 Nao watakula, lakini hawatashiba; watafanya zinaa, lakini hawataongezeka; kwa sababu wameacha kumwangalia Bwana.
Michée 6.14 Lévitique 26.26 Aggée 1.6 2 Chroniques 24.17 Psaumes 36.3
11 Uzinzi na divai na divai mpya huondoa fahamu za wanadamu.
Proverbes 20.1 Luc 21.34 Esaïe 28.7 Esaïe 5.12 Osée 4.12
12 Watu wangu hutaka shauri kwa gongo lao, na fimbo yao huwahubiri mambo; maana roho ya uzinzi imewakosesha, nao wamekwenda kuzini mbali na Mungu wao.
Jérémie 2.27 Osée 5.4 Habakuk 2.19 Esaïe 44.18-44.20 Jérémie 10.8
13 Hutoa dhabihu juu ya vilele vya milima, na kufukiza uvumba juu ya vilima, chini ya mialoni na milibua na miela, kwa kuwa uvuli wake ni mwema; kwa sababu hiyo binti zenu huzini, na bibi arusi zenu hufanya uasherati.
Esaïe 1.29 Jérémie 3.6 Ezéchiel 6.13 Amos 7.17 Esaïe 57.7
14 Sitawaadhibu binti zenu wazinipo, wala bibi arusi zenu wafanyapo uasherati; maana wao wenyewe huenda kando pamoja na wanawake wazinzi, hutoa dhabihu pamoja na makahaba; na watu hawa wasiofahamu wataangamia.
Osée 4.1 Esaïe 56.11 Osée 4.17 2 Rois 23.7 Deutéronome 23.17
15 Ingawa wewe, Israeli, unafanya uzinzi, lakini asiasi Yuda; nanyi msiende Gilgali wala msipande mpaka Beth-Aveni, wala msiape mkisema, Aishivyo Bwana.
Osée 12.11 Osée 9.15 Amos 4.4 Amos 8.14 Osée 10.8
16 Kwa maana Israeli ametenda kwa ukaidi, kama ndama mkaidi; sasa je! Bwana atawalisha kama mwana-kondoo katika mahali penye nafasi!
Jérémie 14.7 Jérémie 7.24 Lévitique 26.33 Zacharie 7.11 Jérémie 3.8
17 Efraimu amejiungamanisha na sanamu; mwache.
Osée 13.2 Psaumes 81.12 Matthieu 15.14 Osée 4.4 Osée 11.2
18 Kileo chao kimegeuka kuwa uchungu; huzini daima; wakuu wake hupenda aibu.
Michée 3.11 2 Rois 17.7-17.17 Psaumes 47.9 Amos 5.12 Proverbes 30.15-30.16
19 Upepo umemfunikiza kwa mbawa zake; nao watatahayarika kwa sababu ya dhabihu zao.
Esaïe 1.29 Jérémie 4.11-4.12 Osée 13.15 Jérémie 51.1 Jérémie 3.24-3.25

Cette Bible est dans le domaine public.