Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Osée 2.20
Bible en Swahili de l’est


1 Waambieni ndugu zenu wanaume, Ami na ndugu zenu wanawake , Ruhama.
Osée 2.23 Zacharie 13.9 Romains 11.30-11.31 Osée 1.9-1.11 Jérémie 31.33
2 Msihini mama yenu, msihini; kwa maana yeye si mke wangu, wala mimi si mume wake; na ayawekee mbali mambo ya uasherati wake yasiwe mbele ya uso wake, na mambo ya uzinzi wake yasiwe kati ya maziwa yake;
Esaïe 50.1 Ezéchiel 23.45 Jérémie 3.1 Jérémie 3.13 Osée 1.2
3 nisije nikamvua nguo zake akawa uchi, nikamweka katika hali aliyokuwa nayo siku ya kuzaliwa kwake, na kumfanya kama jangwa, na kumweka kama nchi kame, na kumfisha kwa kiu;
Ezéchiel 16.22 Esaïe 32.13-32.14 Amos 8.11-8.13 Jérémie 13.22 Ezéchiel 19.13
4 naam, sitawaonea rehema watoto wake; kwa maana ni watoto wa uzinzi.
Jérémie 13.14 Ezéchiel 8.18 Osée 1.6 Osée 1.2 Esaïe 27.11
5 Maana mama yao amezini; yeye aliyewachukua mimba ametenda mambo ya aibu; maana alisema, Nitafuatana na wapenzi wangu, wanipao chakula changu na maji yangu, sufu yangu na kitani yangu, mafuta yangu na vileo vyangu.
Osée 3.1 Osée 2.8 Esaïe 1.21 Jérémie 44.17-44.18 Osée 2.12-2.13
6 Basi kwa ajili ya hayo, angalia, nitaiziba njia yako kwa miiba, nami nitafanya kitalu juu yake, asipate kuyaona mapito yake.
Job 19.8 Job 3.23 Luc 19.43 Lamentations 3.7-3.9 Luc 15.14-15.16
7 Naye atawafuata wapenzi wake, lakini hatawapata; atawatafuta, lakini hatawaona; ndipo atakaposema, Nitakwenda nikamrudie mume wangu wa kwanza; kwa maana hali yangu ya zamani ilikuwa njema kuliko hali yangu ya sasa.
Jérémie 2.2 Osée 5.13 Osée 13.6 Jérémie 14.22 Ezéchiel 23.4
8 Maana hakujua ya kuwa mimi ndiye aliyempa ngano, na divai, na mafuta, na kumwongezea fedha na dhahabu, walivyovitumia kwa ajili ya Baali.
Esaïe 1.3 Ezéchiel 16.16-16.19 Osée 8.4 Osée 4.11 Osée 13.2
9 Basi kwa ajili ya hayo, nitaitwaa tena ngano yangu kwa wakati wake, na divai yangu kwa wakati wake, nami nitamnyang’anya sufu yangu na kitani yangu, vya kumfunika uchi wake.
Osée 2.3 Esaïe 17.10-17.11 Esaïe 3.18-3.26 Ezéchiel 16.39 Sophonie 1.13
10 Na sasa nitaifunua aibu yake mbele ya macho ya wapenzi wake, wala hapana mtu atakayemwokoa katika mkono wangu.
Ezéchiel 23.29 Jérémie 13.22 Proverbes 11.21 Michée 5.8 Psaumes 50.22
11 Tena nitaikomesha furaha yake yote, na sikukuu zake, na siku zake za mwandamo wa mwezi, na sabato zake, na makusanyiko yake yote yaliyoamriwa.
Esaïe 1.13-1.14 Jérémie 7.34 Jérémie 16.9 Amos 5.21 Amos 8.5
12 Nami nitaiharibu mizabibu yake na mitini yake, ambayo alisema, Hii ndiyo ujira wangu niliopewa na wapenzi wangu; nami nitaifanya kuwa msitu, na wanyama wa mashamba wataila.
Esaïe 5.5 Esaïe 7.23 Osée 2.5 Osée 13.8 Jérémie 8.13
13 Nami nitamwadhibu kwa sababu ya siku za Mabaali, aliowafukizia uvumba; hapo alipojipamba kwa pete masikioni mwake, na kwa vito asema Bwana.
Osée 11.2 Juges 3.7 Osée 13.1 Jérémie 7.9 Ezéchiel 16.17
14 Kwa hiyo angalia, mimi nitamshawishi, na kumleta nyikani, na kusema naye maneno ya kumtuliza moyo.
Ezéchiel 20.35-20.36 Apocalypse 12.6 Apocalypse 12.14 Michée 7.14-7.20 Jean 6.44
15 Nami nitampa mashamba yake ya mizabibu toka huko, na bonde la Akori kuwa mlango wa tumaini; naye ataniitikia huko, kama siku zile za ujana wake, na kama siku ile alipopanda kutoka nchi ya Misri.
Jérémie 2.2 Osée 11.1 Ezéchiel 28.26 Ezéchiel 16.8 Josué 7.26
16 Tena siku hiyo itakuwa, asema Bwana, utaniita Ishi
Esaïe 54.5 Osée 2.7 2 Corinthiens 11.2 Apocalypse 19.7 Jean 3.29
17 Kwa maana nitayaondoa majina ya Mabaali kinywani mwake, wala hawatatajwa tena kwa majina yao.
Exode 23.13 Psaumes 16.4 Josué 23.7 Zacharie 13.2 Jérémie 10.11
18 Nami siku hiyo nitafanya agano na wanyama wa mashamba kwa ajili yao, tena na ndege wa angani, tena na wadudu wa nchi; nami nitavivunja upinde na upanga na silaha vitoke katika nchi, nami nitawalalisha salama salimini.
Ezéchiel 34.25 Esaïe 2.4 Jérémie 23.6 Job 5.23 Ezéchiel 39.9-39.10
19 Nami nitakuposa uwe wangu kwa milele; naam, nitakuposa kwa haki, na kwa hukumu, na kwa ufadhili, na kwa rehema.
2 Corinthiens 11.2 Ezéchiel 37.25-37.28 Jérémie 3.14-3.15 Esaïe 54.14 Psaumes 85.10
20 Nami nitakuposa kwa uaminifu; nawe utamjua Bwana.
Jean 17.3 Jérémie 31.33-31.34 1 Jean 5.20 2 Timothée 1.12 Jérémie 24.7
21 Tena itakuwa siku hiyo, mimi nitaitika, asema Bwana; nitaziitikia mbingu, nazo zitaiitikia nchi;
Zacharie 8.12 Matthieu 6.33 1 Corinthiens 3.21-3.23 Zacharie 13.9 Esaïe 55.10
22 nayo nchi itaiitikia nafaka na divai na mafuta; nayo yataiitikia Yezreeli.
Osée 1.4 Osée 1.11 Jérémie 31.12 Joël 2.19
23 Nami nitampanda katika nchi kwa ajili yangu mwenyewe; nami nitamrehemu yeye asiyepewa rehema; nami nitawaambia wale wasiokuwa watu wangu, Ninyi ndinyi watu wangu; nao watasema, Wewe ndiwe Mungu wangu.
Romains 9.25-9.26 1 Pierre 2.9-2.10 Zacharie 13.9 Osée 1.6 Jérémie 31.27

Cette Bible est dans le domaine public.