Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 48.33
Bible en Swahili de l’est


Partage du pays

1 Basi, haya ndiyo majina ya kabila hizo; toka mwisho wa pande za kaskazini, karibu na njia ya Hethloni, hata maingilio ya Hamathi, hata Hasar-enoni, penye mpaka wa Dameski, yaani, upande wa kaskazini karibu na Hamathi, watakuwa na upande wa mashariki, na upande wa magharibi; Dani fungu moja.
Ezéchiel 47.15-47.17 Josué 19.40-19.47 Exode 1.1-1.5 Juges 18.26-18.29 2 Samuel 24.2
2 Tena mpakani mwake Dani, toka upande wa mashariki hata upande wa magharibi; Asheri, fungu moja.
Josué 19.24-19.31 Genèse 30.12-30.13
3 Na mpakani mwa Asheri, toka upande wa mashariki hata upande wa magharibi; Naftali, fungu moja.
Josué 19.32-19.39 Genèse 30.7-30.8
4 Na mpakani mwa Naftali, toka upande wa mashariki hata upande wa magharibi; Manase, fungu moja.
Josué 17.1-17.11 Josué 13.29-13.31 Genèse 30.22-30.24 Genèse 48.14-48.20 Genèse 41.51
5 Na mpakani mwa Manase, toka upande wa mashariki hata upande wa magharibi; Efraimu, fungu moja.
Josué 17.8-17.10 Josué 17.14-17.18 Josué 16.1-16.10
6 Na mpakani mwa Efraimu, toka upande wa mashariki hata upande wa magharibi; Reubeni, fungu moja.
Josué 13.15-13.21 Genèse 49.3-49.4 Genèse 29.32
7 Na mpakani mwa Reubeni, toka upande wa mashariki hata upande wa magharibi; Yuda, fungu moja.
Josué 15.1-15.63 Josué 19.9 Genèse 29.35
8 Na mpakani mwa Yuda, toka upande wa mashariki hata upande wa magharibi, yatakuwapo matoleo mtakayotoa, upana wake mianzi ishirini na tano elfu, na urefu wake sawasawa na moja la mafungu hayo, toka upande wa mashariki hata upande wa magharibi; na mahali patakatifu ni katikati yake.
Esaïe 33.20-33.22 Esaïe 12.6 Ezéchiel 45.1-45.6 2 Corinthiens 6.16 Zacharie 2.11-2.12
9 Matoleo hayo, mtakayomtolea Bwana, urefu wake ni mianzi ishirini na tano elfu, na upana wake elfu kumi.
10 Matoleo hayo matakatifu yatakuwa kwa watu hawa, kwa makuhani; upande wa kaskazini urefu wake ishirini na tano elfu, na upande wa magharibi upana wake elfu kumi, na upande wa mashariki upana wake elfu kumi, na upande wa kusini urefu wake ishirini na tano elfu; na mahali patakatifu pa Bwana patakuwa katikati yake.
Ezéchiel 45.4 Ezéchiel 44.28 Josué 21.1-21.45 1 Corinthiens 9.13-9.14 Nombres 35.1-35.9
11 Patakuwa kwa makuhani wa wana wa Sadoki, waliotakasika, walioulinda ulinzi wangu, wasioasi, wana wa Israeli walipoasi, kama Walawi walivyoasi.
Ezéchiel 44.10 Ezéchiel 40.46 1 Pierre 5.4 2 Timothée 4.7-4.8 Ezéchiel 43.19
12 Na matoleo hayo ya nchi yatolewayo, yatakuwa kwao kitu kitakatifu sana, karibu na mpaka wa Walawi.
Ezéchiel 45.4 Lévitique 27.21
13 Na kuukabili mpaka wa makuhani, Walawi watakuwa na fungu, urefu wake ishirini na tano elfu, na upana wake elfu kumi; urefu wote utakuwa ishirini na tano elfu, na upana wake elfu kumi.
Ezéchiel 45.3 Ezéchiel 45.5 Luc 10.7 Deutéronome 12.19
14 Wala hawatauza sehemu yake, wala kuibadili, wala hawatawapa wengine malimbuko ya nchi; maana ni matakatifu kwa Bwana.
Lévitique 27.28 Lévitique 27.32-27.33 Lévitique 27.9-27.10 Exode 22.29 Ezéchiel 48.12
15 Na mianzi elfu tano iliyosalia katika upana, kuikabili hiyo ishirini na tano elfu, itatumiwa na watu wote, kwa huo mji, na kwa maskani, na kwa viunga, na huo mji utakuwa katikati yake.
Ezéchiel 45.6 Ezéchiel 42.20 Ezéchiel 44.23 Ezéchiel 22.26 1 Timothée 3.15
16 Na vipimo vyake ni hivi; upande wa kaskazini elfu nne na mia tano, na upande wa kusini elfu nne na mia tano, na upande wa mashariki elfu nne na mia tano, na upande wa magharibi elfu nne na mia tano.
Apocalypse 21.16
17 Nao mji utakuwa na malisho; upande wa kaskazini mia mbili na hamsini, na upande wa kusini mia mbili na hamsini, na upande wa mashariki mia mbili na hamsini, na upande wa magharibi mia mbili na hamsini.
18 Na mabaki ya urefu wake yaelekeayo matoleo matakatifu, upande wa mashariki yatakuwa elfu kumi, na upande wa magharibi elfu kumi; nayo yatakuwa sawasawa na matoleo matakatifu; na mazao yake yatakuwa ni chakula cha watu wafanyao kazi humo mjini.
Ezéchiel 45.6 Néhémie 7.46-7.62 Esdras 2.43-2.58 Josué 9.27
19 Na hao wafanyao kazi mjini, wa kabila zote za Israeli, watailima nchi hiyo.
Ezéchiel 45.6 Néhémie 11.1-11.36 1 Rois 4.7-4.23
20 Matoleo yote yatakuwa ishirini na tano elfu, kwa ishirini na tano elfu; mtatoa matoleo matakatifu, nchi ya mraba, pamoja na milki ya mji.
Apocalypse 21.16 Hébreux 12.17
21 Nayo mabaki yake yatakuwa ya huyo mkuu, upande huu na upande huu wa matoleo matakatifu, na milki ya mji, kuikabili hiyo ishirini na tano elfu ya matoleo, kuelekea mpaka wa mashariki; tena upande wa magharibi kuikabili hiyo ishirini na tano elfu, upande wa kuelekea mpaka wa magharibi; sawa na yale mafungu, hayo yatakuwa ya huyo mkuu; na matoleo matakatifu na mahali patakatifu pa nyumba patakuwa katikati yake.
Ezéchiel 48.22 Osée 1.11 Ezéchiel 45.7-45.8 Ezéchiel 37.24 Ezéchiel 34.23-34.24
22 Tena tokea milki ya Walawi, na tokea milki ya mji, kwa kuwa ni katikati ya nchi iliyo ya mkuu, katikati ya mpaka wa Yuda na mpaka wa Benyamini, itakuwa ya mkuu.
23 Na katika habari za kabila zilizosalia; toka upande wa mashariki hata upande wa magharibi; Benyamini, fungu moja.
Josué 18.21-18.28 Genèse 35.16-35.19 Ezéchiel 48.1-48.7
24 Tena mpakani mwa Benyamini, toka upande wa mashariki hata upande wa magharibi; Simeoni, fungu moja.
Josué 19.1-19.9 Genèse 29.33 Genèse 49.5-49.7
25 Tena mpakani mwa Simeoni, toka upande wa mashariki hata upande wa magharibi; sakari, fungu moja.
Josué 19.17-19.23 Genèse 30.14-30.18
26 Na mpakani mwa Isakari, toka upande wa mashariki hata upande wa magharibi; Zabuloni, fungu moja.
Josué 19.10-19.16 Genèse 30.19-30.20
27 Na mpakani mwa Zabuloni, toka upande wa mashariki hata upande wa magharibi; Gadi, fungu moja.
Josué 13.24-13.28 Genèse 30.10-30.11
28 Na mpakani mwa Gadi, upande wa kusini kuelekea kusini, mpaka wake utakuwa toka Tamari, mpaka maji ya Meriba-Kadeshi, mpaka kijito cha Misri, mpaka bahari kubwa.
2 Chroniques 20.2 Ezéchiel 47.15 Ezéchiel 47.19-47.20 Ezéchiel 47.10 Nombres 20.1
29 Hiyo ndiyo nchi mtakayozigawanyia kabila za Israeli, kuwa urithi wao, na hayo ndiyo mafungu yao, asema Bwana MUNGU.
Josué 13.1-13.21 Nombres 34.2 Nombres 34.13 Ezéchiel 47.13-47.22
30 Na matokeo ya mji ndiyo haya; upande wa kaskazini, mianzi elfu nne na mia tano, kwa kupima;
Ezéchiel 48.16 Ezéchiel 48.32-48.35 Apocalypse 21.16
31 na malango ya mji yatatajwa kwa majina ya kabila za Israeli, malango matatu upande wa kaskazini; lango la Reubeni, moja; lango la Yuda, moja; na lango la Lawi, moja.
Apocalypse 21.12-21.13 Esaïe 26.1-26.2 Esaïe 60.11 Esaïe 54.12 Apocalypse 21.21
32 Na upande wa mashariki, elfu nne na mia tano, kwa kupima; na malango matatu; lango la Yusufu, moja; lango la Benyamini, moja; lango la Dani, moja.
33 Na upande wa kusini, elfu nne na mia tano kwa kupima; na malango matatu; lango la Simeoni, moja; lango la Isakari, moja; lango la Zabuloni, moja.
34 Na upande wa magharibi, elfu nne na mia tano; pamoja na malango yake matatu; lango la Gadi, moja; lango la Asheri, moja; na lango la Naftali, moja.
35 Kuuzunguka ni mianzi kumi na nane elfu; na jina la mji huo tangu siku hiyo litakuwa hili, Bwana yupo hapa.
Jérémie 33.16 Jérémie 3.17 Zacharie 2.10 Apocalypse 21.3 Joël 3.21

Cette Bible est dans le domaine public.