Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 36.19
Bible en Swahili de l’est


Rétablissement d’Israël

1 Na wewe, mwanadamu, itabirie milima ya Israeli, useme, Enyi milima ya Israeli, lisikieni neno la Bwana.
Ezéchiel 36.8 Ezéchiel 20.47 Ezéchiel 34.14 Ezéchiel 36.4 Jérémie 22.29
2 Bwana MUNGU asema hivi; Kwa sababu adui amesema juu yenu, Aha! Na, Mahali pa juu pa zamani pamekuwa petu tupamiliki;
Deutéronome 32.13 Ezéchiel 25.3 Ezéchiel 35.10 Ezéchiel 26.2 Esaïe 58.14
3 basi tabiri useme, Bwana MUNGU asema hivi; Kwa sababu, naam, kwa sababu wamewafanya ninyi kuwa ukiwa, na kuwameza pande zote, mpate kuwa milki kwa mabaki ya mataifa, nanyi mmeambwa kwa midomo yao waongeao, na kwa masingizio ya watu;
Psaumes 44.13-44.14 Jérémie 18.16 Lamentations 2.15-2.16 1 Corinthiens 4.13 Proverbes 1.12
4 kwa sababu hiyo, enyi milima ya Israeli, lisikieni neno la Bwana MUNGU; Bwana MUNGU aiambia hivi hiyo milima na vilima, mifereji ya maji na mabonde, mahali palipoharibika na kuwa ukiwa, na miji iliyoachwa na watu, ambayo imekuwa mateka, na kuzomewa na mabaki ya mataifa, walio karibu pande zote;
Ezéchiel 34.28 Deutéronome 11.11 Psaumes 79.4 Ezéchiel 36.1 Ezéchiel 36.6
5 basi Bwana MUNGU asema hivi; Hakika kwa moto wa wivu wangu nimenena juu ya mabaki ya mataifa, na juu ya Edomu yote, waliojiandikia nchi yangu kuwa milki yao, kwa furaha ya mioyo yao yote, kwa jeuri ya roho zao, ili waitupe nje kuwa mawindo;
Ezéchiel 36.3 Jérémie 25.15-25.29 Michée 7.8 Jérémie 25.9 Deutéronome 4.24
6 basi katika kutabiri habari za nchi ya Israeli, uiambie milima na vilima, mifereji ya maji na mabonde, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, nimenena katika wivu wangu na hasira yangu, kwa sababu mmechukua aibu ya mataifa;
Ezéchiel 34.29 Psaumes 123.3-123.4 Psaumes 74.10 Psaumes 74.23 Ezéchiel 36.4-36.5
7 basi Bwana MUNGU asema hivi; Nimeinua mkono wangu, kusema, Hakika, mataifa walio karibu nanyi pande zote, wao watachukua aibu yao.
Ezéchiel 20.5 Jérémie 25.15-25.29 Ezéchiel 20.15 Apocalypse 10.5-10.6 Deutéronome 32.40
8 Lakini ninyi, enyi milima ya Israeli, mtachipuza matawi yenu na kuwapa watu wangu sraeli matunda yenu; maana wa karibu kuja.
Esaïe 27.6 Esaïe 4.2 Ezéchiel 34.26-34.29 Ezéchiel 17.23 Hébreux 10.37
9 Maana, tazama, mimi nasimama upande wenu, nami nitawaelekea, nanyi mtalimwa na kupandwa mbegu;
Psaumes 99.8 Psaumes 46.11 Osée 2.21-2.23 Joël 3.18 Aggée 2.19
10 nami nitaongeza watu juu yenu, nyumba yote ya Israeli, naam, yote pia; nayo miji itakaliwa na watu, na mahali palipoharibika patajengwa.
Ezéchiel 36.33 Esaïe 27.6 Jérémie 31.27-31.28 Ezéchiel 36.37 Jérémie 33.12
11 Nami nitaongeza juu yenu mwanadamu na mnyama, nao watazidi na kuzaa; nami nitawakalisha watu ndani yenu, kwa kadiri ya hali yenu ya kwanza, nami nitawatendea mema kuliko mema ya mianzo yenu; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.
Michée 7.14 Ezéchiel 16.55 Jérémie 31.27 Jérémie 33.12 Jérémie 30.18
12 Naam, nitaleta watu watembee juu yenu, naam, watu wangu Israeli; nao watakumiliki, nawe utakuwa urithi wao, wala hutawafisha watoto wao tena tangu leo.
Jérémie 15.7 Jérémie 32.44 Ezéchiel 36.13 Ezéchiel 47.14 Nombres 13.32
13 Bwana MUNGU asema hivi; Kwa kuwa watu hukuambia, wewe nchi u mwenye kula watu, nawe umekuwa mwenye kufisha watu wa taifa lako;
Nombres 13.32
14 basi hutakula watu tena, wala hutafisha watu wa taifa lako tena, asema Bwana MUNGU;
Ezéchiel 37.25-37.28 Esaïe 60.21 Amos 9.15
15 wala sitakusikizisha tena aibu yao wasioamini, wala hutachukua matukano ya watu tena; wala hutalikwaza taifa lako tena, asema Bwana MUNGU.
Psaumes 89.50 Ezéchiel 34.29 Ezéchiel 36.6 Esaïe 60.14 Esaïe 54.4
16 Tena, neno la Bwana likanijia, kusema,
17 Mwanadamu, nyumba ya Israeli walipokaa katika nchi yao wenyewe, waliitia uchafu kwa njia yao na kwa matendo yao. Njia yao mbele zangu ilikuwa kama uchafu wa mwanamke wakati wa kutengwa kwake.
Jérémie 2.7 Psaumes 106.37-106.38 Esaïe 24.5 Jérémie 3.9 Lévitique 15.19-15.33
18 Kwa hiyo nalimwaga hasira yangu juu yao, kwa ajili ya damu waliyoimwaga juu ya nchi, na kwa sababu wameitia uchafu kwa vinyago vyao.
2 Chroniques 34.21 Ezéchiel 7.8 Lamentations 4.11 Lamentations 2.4 Jérémie 44.6
19 Nikawatawanya katika mataifa, wakatapanyika katika nchi nyingi; kwa kadiri ya njia yao, na kwa kadiri ya matendo yao, naliwahukumu.
Ezéchiel 39.24 Deutéronome 28.64 Romains 2.6 Ezéchiel 5.12 Ezéchiel 18.30
20 Nao walipoyafikilia mataifa yale waliyoyaendea, walilitia unajisi jina langu takatifu; kwa kuwa watu waliwanena, wakisema, Watu hawa ni watu wa Bwana, nao wametoka katika nchi yake.
Esaïe 52.5 Romains 2.24 Jérémie 33.24 Exode 32.11-32.13 Daniel 3.15
21 Lakini, naliwahurumia kwa ajili ya jina langu takatifu, ambalo nyumba ya Israeli walikuwa wamelitia unajisi katika mataifa waliyoyaendea.
Psaumes 74.18 Esaïe 48.9 Ezéchiel 20.9 Ezéchiel 20.14 Esaïe 37.35
22 Kwa hiyo; waambieni nyumba ya Israeli, Bwana MUNGU asema hivi Sitendi hili kwa ajili yenu, Ee nyumba ya Israeli, bali kwa ajili ya jina langu takatifu, mlilolitia unajisi katika mataifa mliyoyaendea.
Ezéchiel 36.32 Deutéronome 7.7-7.8 Psaumes 106.8 Psaumes 115.1-115.2 Deutéronome 9.5-9.7
23 Nami nitalitakasa jina langu kuu, lililotiwa unajisi katika mataifa, mlilolitia unajisi kati yao; nao mataifa watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, asema Bwana MUNGU, nitakapotakaswa kati yenu mbele ya macho yao.
Ezéchiel 20.41 Esaïe 5.16 Psaumes 126.1-126.3 Psaumes 46.10 Ezéchiel 39.7
24 Maana nitawatwaa kati ya mataifa, nami nitawakusanya na kuwatoa katika nchi zote, na kuwarudisha katika nchi yenu wenyewe.
Ezéchiel 37.21 Ezéchiel 34.13 Esaïe 43.5-43.6 Ezéchiel 11.17 Jérémie 30.18
25 Nami nitawanyunyizia maji safi, nanyi mtakuwa safi; nitawatakaseni na uchafu wenu wote, na vinyago vyenu vyote.
Hébreux 10.22 Tite 3.5-3.6 Esaïe 4.4 Psaumes 51.7 Osée 14.3
26 Nami nitawapa ninyi moyo mpya, nami nitatia roho mpya ndani yenu, nami nitatoa moyo wa jiwe uliomo ndani ya mwili wenu, nami nitawapa moyo wa nyama.
Ezéchiel 11.19-11.20 Psaumes 51.10 2 Corinthiens 5.17 Deutéronome 30.6 2 Corinthiens 3.3
27 Nami nitatia roho yangu ndani yenu, na kuwaendesha katika sheria zangu, nanyi mtazishika hukumu zangu, na kuzitenda.
Tite 3.3-3.6 Ezéchiel 39.29 Ezéchiel 37.14 Hébreux 13.21 Ezéchiel 37.24
28 Nanyi mtakaa katika nchi ile niliyowapa baba zenu, nanyi mtakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu.
Ezéchiel 37.27 Ezéchiel 37.23 Ezéchiel 11.20 Jérémie 31.33 Ezéchiel 28.25
29 Nami nitawaokoeni na uchafu wenu wote; nitaiita ngano, na kuiongeza, wala sitaweka njaa juu yenu tena.
Matthieu 1.21 Osée 2.21-2.23 Ezéchiel 34.27-34.29 Michée 7.19 Joël 3.21
30 Nami nitazidisha matunda ya miti, na mazao ya mashamba, msipate tena kutukanwa na mataifa kwa sababu ya njaa.
Ezéchiel 34.27 Joël 2.17 Joël 2.26 Deutéronome 29.23-29.28 Lévitique 26.4
31 Ndipo mtazikumbuka njia zenu mbaya, na matendo yenu yasiyokuwa mema, nanyi mtajichukia nafsi zenu kwa macho yenu, kwa sababu ya maovu yenu na machukizo yenu.
Ezéchiel 6.9 Ezéchiel 20.43 Néhémie 9.26-9.35 Ezéchiel 16.61-16.63 Esaïe 6.5
32 Ijulikane kwenu ya kuwa silitendi neno hili kwa ajili yenu, asema Bwana MUNGU; tahayarikeni, na kufadhaika, kwa sababu ya njia zenu, Enyi nyumba ya Israeli.
Deutéronome 9.5 Ezéchiel 36.22 Esdras 9.6 Romains 6.21 1 Pierre 4.2-4.3
33 Bwana MUNGU asema hivi; Siku ile nitakapowatakaseni na maovu yenu yote, nitaifanya miji ikaliwe na watu, na palipobomolewa pajengwe tena.
Ezéchiel 36.10 Esaïe 58.12 Zacharie 8.7-8.8 Amos 9.14-9.15 Jérémie 50.19-50.20
34 Nchi iliyokuwa ukiwa italimwa, ijapokuwa ilikuwa ukiwa mbele ya macho ya watu wote waliopita.
2 Chroniques 36.21 Jérémie 25.9-25.11 Ezéchiel 6.14 Deutéronome 29.23-29.28
35 Nao watasema, Nchi hii, iliyokuwa ukiwa, imekuwa kama bustani ya Adeni; nayo miji iliyokuwa mahame, na ukiwa, na magofu, sasa ina maboma, inakaliwa na watu.
Esaïe 51.3 Joël 2.3 Ezéchiel 37.13 Psaumes 58.11 Genèse 2.8-2.9
36 Ndipo mataifa, waliobaki karibu yenu pande zote, watajua ya kuwa mimi, Bwana, nimejenga mahali palipoharibika, nami nimepanda mbegu katika nchi iliyokuwa ukiwa; mimi, Bwana, nimesema hayo; tena nitayatenda.
Ezéchiel 17.24 Ezéchiel 22.14 Ezéchiel 37.14 Nombres 23.19 Osée 14.4-14.9
37 Bwana MUNGU asema hivi, Tena kwa ajili ya jambo hili nitaulizwa na nyumba ya sraeli, ili niwatendee; nami nitawaongeza kwa watu kama kundi la kondoo.
Ezéchiel 14.3 1 Jean 5.14 Ezéchiel 20.31 Jacques 4.2-4.3 Psaumes 102.17
38 Kama kundi lililo tayari kutolewa sadaka, kama kundi la Yerusalemu katika sikukuu zake zilizoamriwa; ndivyo itakavyojazwa watu, miji ile iliyokuwa maganjo; nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.
Jean 10.16 Apocalypse 7.4-7.9 Deutéronome 16.16 2 Chroniques 35.7-35.19 Jérémie 30.19

Cette Bible est dans le domaine public.