Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Lamentations 2.18
Bible en Swahili de l’est


Le jugement de Jérusalem

1 Jinsi Bwana alivyomfunika binti Sayuni Kwa wingu katika hasira yake! Ameutupa toka mbinguni hata nchi Huo uzuri wa Israeli; Wala hakukikumbuka kiti cha miguu yake Katika siku ya hasira yake.
Psaumes 132.7 1 Chroniques 28.2 Esaïe 64.11 Ezéchiel 28.14-28.16 Matthieu 11.23
2 Bwana ameyameza makao yote ya Yakobo, Wala hakuona huruma; Ameziangusha ngome za binti Yuda Katika ghadhabu yake; Amezibomoa hata nchi Ameunajisi ufalme na wakuu wake.
Psaumes 89.39-89.40 Lamentations 3.43 Lamentations 2.17 Esaïe 43.28 Psaumes 21.9
3 Ameikata pembe yote ya Israeli Katika hasira yake kali; Ameurudisha nyuma mkono wake wa kuume Mbele ya hao adui, Naye amemteketeza Yakobo kama moto uwakao, Ulao pande zote.
Psaumes 74.11 Psaumes 75.10 Esaïe 42.25 Psaumes 75.5 Jérémie 48.25
4 Ameupinda upinde wake kama adui, Amesimama na mkono wake wa kuume kama mtesi; Naye amewaua hao wote Waliopendeza macho; Katika hema ya binti Sayuni Amemimina kani yake kama moto.
Jérémie 7.20 Lamentations 3.12-3.13 Esaïe 42.25 Jérémie 21.5 Ezéchiel 24.25
5 Bwana amekuwa mfano wa adui, Amemmeza Israeli; Ameyameza majumba yake yote, Ameziharibu ngome zake; Tena amemzidishia binti Yuda Matanga na maombolezo.
Lamentations 2.2 Jérémie 30.14 Jérémie 52.13 Lamentations 2.4 2 Rois 25.9
6 Naye ameondoa maskani yake kwa nguvu, Kana kwamba ni ya bustani tu; Ameziharibu sikukuu zake; Bwana amezisahauzisha katika Sayuni Sikukuu za makini na sabato; Naye amewadharau mfalme na kuhani Katika uchungu wa hasira yake.
Sophonie 3.18 Lamentations 1.4 Lamentations 4.16 Esaïe 43.28 Esaïe 64.11
7 Bwana ameitupilia mbali madhabahu yake, Amepachukia patakatifu pake; Amezitia katika mikono ya hao adui Kuta za majumba yake; Wamepiga kelele ndani ya nyumba ya Bwana Kama katika siku ya kusanyiko la makini.
Ezéchiel 7.20-7.22 Psaumes 74.3-74.8 Ezéchiel 24.21 Jérémie 52.13 Psaumes 78.59-78.61
8 Bwana amekusudia kuuharibu Ukuta wa binti Sayuni; Ameinyosha hiyo kamba, Hakuuzuia mkono wake usiangamize; Bali amefanya boma na ukuta kuomboleza; Zote pamoja hudhoofika.
2 Rois 21.13 Esaïe 34.11 Jérémie 14.2 Esaïe 3.26 Jérémie 5.10
9 Malango yake yamezama katika nchi; Ameyaharibu makomeo yake na kuyavunja; Mfalme wake na wakuu wake wanakaa Kati ya mataifa wasio na sheria; Naam, manabii wake hawapati maono Yatokayo kwa Bwana.
Osée 3.4 Néhémie 1.3 2 Chroniques 15.3 Ezéchiel 7.26 Deutéronome 28.36
10 Wazee wa binti Sayuni huketi chini, Hunyamaza kimya; Wametupa mavumbi juu ya vichwa vyao, Wamejivika viunoni nguo za magunia; Wanawali wa Yerusalemu huinama vichwa vyao Kuielekea nchi.
Esaïe 3.26 Esaïe 15.3 Job 2.12-2.13 Lamentations 3.28 Amos 8.3
11 Macho yangu yamechoka kwa machozi, Mtima wangu umetaabika; Ini langu linamiminwa juu ya nchi Kwa uharibifu wa binti ya watu wangu; Kwa sababu watoto wachanga na wanyonyao, Huzimia katika mitaa ya mji.
Lamentations 1.20 Lamentations 1.16 Job 16.13 Jérémie 4.19 Esaïe 22.4
12 Wao huwauliza mama zao, Zi wapi nafaka na divai? Hapo wazimiapo kama waliojeruhiwa Katika mitaa ya mji, Hapo walipomiminika nafsi zao Vifuani mwa mama zao.
Ezéchiel 30.24 Esaïe 53.12
13 Nikushuhudie nini? Nikufananishe na nini, Ee Binti Yerusalemu? Nikusawazishe na nini, nipate kukufariji, Ee bikira binti Sayuni? Kwa maana uvunjifu wako ni mkuu kama bahari, Ni nani awezaye kukuponya?
Lamentations 1.12 Jérémie 14.17 Jérémie 8.22 Jérémie 30.12-30.15 2 Samuel 5.20
14 Manabii wako wameona maono kwa ajili yako Ya ubatili na upumbavu Wala hawakufunua uovu wako, Wapate kurudisha kufungwa kwako; Bali wameona mabashiri ya ubatili kwa ajili yako Na sababu za kuhamishwa.
Esaïe 58.1 Ezéchiel 22.28 Jérémie 5.31 Ezéchiel 22.25 Jérémie 2.8
15 Hao watu wote wapitao Hukupigia makofi; Humzomea binti Yerusalemu, Na kutikisa vichwa vyao; Je! Mji huu ndio ulioitwa, Ukamilifu wa uzuri, Furaha ya dunia yote?
Psaumes 48.2 Jérémie 18.16 Psaumes 50.2 Jérémie 19.8 Ezéchiel 25.6
16 Juu yako adui zako wote Wamepanua vinywa vyao; Huzomea, husaga meno yao, Husema, Tumemmeza; Hakika siku hii ndiyo tuliyoitazamia; Tumeipata, tumeiona.
Psaumes 35.21 Lamentations 3.46 Psaumes 56.2 Job 16.9-16.10 Jérémie 51.34
17 Bwana ameyatenda aliyoyakusudia; amelitimiza neno lake, Aliloliamuru siku za kale; Ameangusha hata chini, Wala hakuona huruma; Naye amemfurahisha adui juu yako, Ameitukuza pembe ya watesi wako.
Psaumes 89.42 Ezéchiel 5.11 Lamentations 1.5 Ezéchiel 8.18 Ezéchiel 7.8-7.9
18 Mioyo yao ilimlilia Bwana; Ee ukuta wa binti Sayuni! Machozi na yachuruzike kama mto Mchana na usiku; Usijipatie kupumzika; Mboni ya jicho lako isikome.
Lamentations 2.8 Jérémie 9.1 Lamentations 1.16 Psaumes 119.145 Psaumes 119.136
19 Inuka, ulalamike usiku, Mwanzo wa makesha yake; Mimina moyo wako kama maji usoni pa Bwana; Umwinulie mikono yako; Kwa uhai wa watoto wako wachanga wazimiao kwa njaa, Mwanzo wa kila njia kuu.
Psaumes 62.8 Psaumes 142.2 Esaïe 26.9 1 Samuel 1.15 Psaumes 119.147-119.148
20 Tazama, Bwana, uangalie, Ni nani uliyemtenda hayo! Je! Wanawake wale mazao yao, Watoto waliowabeba? Je! Kuhani na nabii wauawe Katika patakatifu pa Bwana?
Lamentations 4.10 Jérémie 19.9 Psaumes 78.64 Lamentations 4.13 Deutéronome 9.26
21 Kijana na mzee hulala chini Katika njia kuu; Wasichana wangu na wavulana wangu Wameanguka kwa upanga; Umewaua katika siku ya hasira yako; Umeua, wala hukuona huruma.
2 Chroniques 36.17 Lamentations 3.43 Zacharie 11.6 Jérémie 13.14 Lamentations 2.2
22 Umeziita kama katika siku ya mkutano wa makini; Hofu zangu zije pande zote; Wala hapana hata mmoja aliyepona wala kusalia Katika siku ya hasira ya Bwana; Hao niliowabeba na kuwalea Huyo adui yangu amewakomesha.
Jérémie 6.25 Psaumes 31.13 Jérémie 16.2-16.4 Osée 9.12-9.16 Jérémie 46.5

Cette Bible est dans le domaine public.