Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 52.26
Bible en Swahili de l’est


Récit de la chute de Jérusalem

Siège et prise de Jérusalem

1 Sedekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja hapo alipoanza kumiliki; naye akamiliki miaka kumi na mmoja huko Yerusalemu; na jina la mama yake aliitwa Hamutali, binti Yeremia wa Libna.
2 Rois 24.18 Josué 10.29 2 Chroniques 36.11 Josué 15.42 2 Rois 8.22
2 Naye alitenda yaliyo mabaya machoni pa Bwana, sawasawa na yote aliyoyatenda Yehoyakimu.
1 Rois 14.22 2 Chroniques 36.12-36.13 Jérémie 26.21-26.23 Jérémie 36.29-36.31 Ezéchiel 21.25
3 Maana, kwa sababu ya hasira ya Bwana, mambo haya yalitokea katika Yerusalemu na katika Yuda, hata akawaondosha wasiwe mbele za uso wake, naye Sedekia akamwasi mfalme wa Babeli.
2 Chroniques 36.13 Esaïe 3.4-3.5 Ezéchiel 17.12-17.21 Ecclésiaste 10.16 Esaïe 3.1
4 Ikawa, katika mwaka wa kenda wa kumiliki kwake, katika mwezi wa kumi, na siku ya kumi ya mwezi huo, Nebukadreza, mfalme wa Babeli, akaja, yeye na jeshi lake lote, juu ya Yerusalemu, akapanga hema zake juu yake; nao wakajenga ngome juu yake pande zote.
Jérémie 39.1 Ezéchiel 24.1-24.2 Zacharie 8.19 Jérémie 32.24 Jérémie 52.7
5 Basi mji huo ulihusuriwa hata mwaka wa kumi na mmoja wa mfalme Sedekia.
6 Katika mwezi wa nne, siku ya kenda ya mwezi, njaa ilizidi sana ndani ya mji, hata hapakuwa na chakula kwa watu wa nchi.
Esaïe 3.1 2 Rois 25.3 Jérémie 38.9 Jérémie 39.2 Lamentations 5.10
7 Ukuta wa mji ukabomolewa, watu wote wa vita wakakimbia, wakatoka mjini usiku, kwa njia ya lango lililokuwa kati ya zile kuta mbili, karibu na bustani ya mfalme; (basi wale Wakaldayo walikuwa wameuzunguka mji pande zote;) wakaenda zao kwa njia ya Araba.
Jérémie 51.32 2 Rois 25.4 Jérémie 39.4-39.7 Deutéronome 32.30 Deutéronome 28.25
8 Lakini jeshi la Wakaldayo wakamfuatia mfalme, wakampata Sedekia katika nchi tambarare ya Yeriko, na jeshi lake lote walikuwa wametawanyika na kumwacha.
Jérémie 34.21 Jérémie 32.4 Jérémie 38.23 Jérémie 21.7 Jérémie 37.18
9 Nao wakamshika mfalme, wakamchukua kwa mfalme wa Babeli, aliyekuwa huko Ribla katika nchi ya Hamathi, naye akatoa hukumu juu yake.
Nombres 13.21 Jérémie 39.5 Josué 13.5 2 Rois 25.6 Nombres 34.11
10 Ndipo mfalme wa Babeli akawaua wana wa Sedekia mbele ya macho yake; pia akawaua wakuu wote wa Yuda huko Ribla.
Jérémie 22.30 2 Rois 25.7 Deutéronome 28.34 Jérémie 39.6-39.7 Ezéchiel 11.7-11.11
11 Akampofusha macho Sedekia; tena mfalme wa Babeli akamfunga kwa pingu, akamchukua mpaka Babeli, akamtia gerezani hata siku ya kufa kwake.
Ezéchiel 12.13 Jérémie 34.3-34.5
12 Basi katika mwezi wa tano, siku ya kumi ya mwezi, ndio mwaka wa kumi na kenda wa mfalme Nebukadreza, mfalme wa Babeli; Nebuzaradani, amiri wa askari walinzi, aliyesimama mbele ya mfalme wa Babeli, aliingia Yerusalemu.
2 Rois 25.8 Jérémie 52.29 Zacharie 8.19 Jérémie 39.9 2 Rois 24.12
13 Akaiteketeza nyumba ya Bwana, na nyumba ya mfalme; na nyumba zote za Yerusalemu, naam, kila nyumba kubwa aliiteketeza kwa moto.
2 Chroniques 36.19 Michée 3.12 Psaumes 79.1 2 Rois 25.9 Esaïe 64.10-64.11
14 Na jeshi lote la Wakaldayo, waliokuwa pamoja na huyo amiri wa askari walinzi, wakazibomoa kuta zote za Yerusalemu pande zote.
Néhémie 1.3 2 Rois 25.10
15 Kisha Nebuzaradani, amiri wa askari walinzi, akawachukua wafungwa baadhi ya watu waliokuwa maskini, na mabaki ya watu walioachwa katika mji, nao wale walioasi na kumkimbilia mfalme wa Babeli, nao mabaki ya vibarua.
Jérémie 15.1-15.2 Zacharie 14.2
16 Lakini Nebuzaradani, amiri wa askari walinzi, akawaacha watu walio maskini kabisa ili wawe watunza mizabibu na wakulima.
2 Rois 25.12 Jérémie 39.9-39.10 Jérémie 40.5-40.7 Ezéchiel 33.24
17 Na nguzo za shaba zilizokuwa katika nyumba ya Bwana, na matako ya bahari ya shaba iliyokuwa katika nyumba ya Bwana, Wakaldayo walivivunja vipande vipande, wakaichukua shaba yake yote mpaka Babeli.
Jérémie 27.19-27.22 2 Chroniques 4.12-4.15 Jérémie 52.21-52.23 Lamentations 1.10 Daniel 1.2
18 Nayo masufuria, na majembe, na makasi, na mabakuli, na miiko, na vyombo vyote vya shaba walivyokuwa wakivitumia, wakavichukua vyote.
Nombres 4.14 1 Rois 7.45 Exode 27.3 1 Rois 7.40 2 Chroniques 4.22
19 Navyo vikombe, na vyombo vya kutolea majivu, na mabakuli, na masufuria, na vinara, na miiko, na vyetezo, vilivyokuwa vya dhahabu katika dhahabu, na vilivyokuwa vya fedha katika fedha, amiri wa askari walinzi akavichukua.
1 Rois 7.49-7.50 Lévitique 26.12 Nombres 16.46 2 Rois 25.15 Apocalypse 8.3-8.5
20 Nguzo mbili, bahari moja, na ng’ombe kumi na mbili za shaba zilizokuwa chini ya matako yake, ambavyo mfalme Sulemani aliifanyia nyumba ya Bwana; shaba ya vitu hivyo vyote ilikuwa haiwezi kupimwa kwa kuwa nyingi sana.
1 Rois 7.47 2 Rois 25.16 1 Chroniques 22.14 2 Chroniques 4.18
21 Na nguzo hizo, urefu wa nguzo moja ulikuwa dhiraa kumi na nane, na uzi wa dhiraa kumi na mbili ungeweza kuizunguka; na unene wake ulikuwa nyanda nne; nayo ilikuwa ya uvungu.
2 Rois 25.17 1 Rois 7.15-7.21 2 Chroniques 3.15-3.17
22 Nayo ilikuwa na kichwa cha shaba juu yake; na urefu wa kichwa kimoja ulikuwa dhiraa tano; palikuwa na mapambo ya wavu na makomamanga juu ya kichwa hicho pande zote; vyote vilikuwa vya shaba; nayo nguzo ya pili ilikuwa na mapambo kama hayo, na makomamanga.
Exode 28.14-28.22 2 Chroniques 4.12-4.13 Exode 39.15-39.18 1 Rois 7.16-7.17 Exode 28.25
23 Palikuwa na makomamanga tisini na sita katika pande zake; makomamanga; yote yalikuwa mia juu ya wavu huo pande zote.
1 Rois 7.20
24 Naye amiri wa askari walinzi akamtwaa Seraya, kuhani mkuu, na Sefania, kuhani wa pili, na wale walinzi watatu wa mlango;
2 Rois 25.18 1 Chroniques 6.14 Jérémie 29.25 Jérémie 37.3 Jérémie 21.1
25 na katika mji akatwaa towashi mmoja aliyewasimamia watu wa vita; na watu saba katika wale waliouona uso wa mfalme, walioonekana katika mji; na karani wa jemadari wa jeshi, aliyewaandika watu wa nchi; na watu sitini katika watu wa nchi, walioonekana ndani ya mji.
Esther 1.14 2 Rois 25.19 Matthieu 18.10
26 Na Nebuzaradani, amiri wa askari walinzi, akawatwaa, akawaleta kwa mfalme wa Babeli huko Ribla.
27 Naye mfalme wa Babeli akawapiga na kuwaua huko Ribla katika nchi ya Hamathi. Ndivyo Yuda alivyochukuliwa utumwani, akatolewa katika nchi yake.
Michée 4.10 Ezéchiel 8.11-8.18 Esaïe 27.10 Jérémie 25.9-25.11 Esaïe 6.11-6.12
28 Watu hawa ndio wale ambao Nebukadreza aliwachukua mateka; katika mwaka wa saba, Wayahudi elfu tatu na ishirini na watatu;
2 Rois 24.2-24.3 2 Rois 24.12-24.16 Daniel 1.1-1.3 2 Chroniques 36.20
29 katika mwaka wa kumi na nane wa Nebukadreza aliwachukua toka Yerusalemu watu mia nane na thelathini na wawili;
Genèse 12.5 Jérémie 52.12 2 Chroniques 36.20 2 Rois 25.11 Exode 1.5
30 katika mwaka wa ishirini na tatu wa Nebukadreza, Nebuzaradani, amiri wa askari walinzi, akawachukua mateka katika Wayahudi watu mia saba na arobaini na watano; jumla ya watu hao wote ni watu elfu nne na mia sita.
Jérémie 52.15 Jérémie 6.9
31 Hata ikawa, katika mwaka wa thelathini na saba wa kuhamishwa kwake Yehoyakini, mfalme wa Yuda, katika mwezi wa kumi na mbili, siku ya ishirini na tano ya mwezi, Evil-merodaki, mfalme wa Babeli, katika mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, akamwinua kichwa chake Yehoyakini, mfalme wa Yuda, akamtoa gerezani.
2 Rois 25.27-25.30 Psaumes 3.3 Genèse 40.13 Psaumes 27.6 Proverbes 21.1
32 Akasema naye maneno mazuri, akaweka kiti chake juu ya viti vya wafalme waliokuwa pamoja naye huko Babeli.
Proverbes 12.25 Jérémie 27.6-27.11 Daniel 2.37 Daniel 5.18-5.19
33 Naye akabadili mavazi yake ya gerezani, akala chakula mbele yake daima, siku zote za maisha yake.
2 Samuel 9.7 Genèse 41.42 Genèse 41.14 2 Samuel 9.13 1 Rois 2.7
34 Na kwa posho yake, alipewa posho ya daima na mfalme wa Babeli; kila siku alipewa posho hata siku ya kufa kwake, siku zote za maisha yake.
2 Samuel 9.10 Matthieu 6.11 Luc 11.3

Cette Bible est dans le domaine public.