Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 42.19
Bible en Swahili de l’est


Appel à ne pas aller en Égypte

1 Ndipo maakida wote wa majeshi, na Yohana, mwana wa Karea, na Yezania, mwana wa Hoshaya, na watu wote tangu wadogo hata wakubwa, wakakaribia,
Jérémie 40.13 Jérémie 41.11 Jérémie 6.13 Jérémie 42.8 Jérémie 40.8
2 wakamwambia Yeremia, nabii, Twakusihi, maombi yetu yakubaliwe mbele yako, ukatuombee kwa Bwana, Mungu wako, yaani, watu hawa wote waliosalia; maana tumesalia wachache tu katika watu wengi, kama macho yako yatuonavyo;
Jérémie 36.7 Lévitique 26.22 Lamentations 1.1 Actes 8.24 Esaïe 1.9
3 ili kwamba Bwana, Mungu wako, atuonyeshe njia ambayo yatupasa tuiendee, na jambo litupasalo tulitende.
Proverbes 3.6 Psaumes 86.11 Esdras 8.21 Michée 4.2 Jérémie 6.16
4 Ndipo Yeremia, nabii, akawaambia, Nimewasikia; tazama, nitamwomba Bwana, Mungu wenu, sawasawa na maneno yenu; tena itakuwa, neno lo lote ambalo Bwana atawajibu, nitawaambia; sitawazuilia neno liwalo lote.
1 Samuel 3.17-3.18 1 Samuel 12.23 Exode 8.29 Psaumes 40.10 Jérémie 23.28
5 Wakamwambia Yeremia, Bwana na awe shahidi wa kweli na uaminifu kati yetu; ikiwa hatufanyi sawasawa na neno lile, ambalo Bwana, Mungu wako, atakutuma utuletee.
Genèse 31.50 Juges 11.10 Apocalypse 3.14 Malachie 2.14 Malachie 3.5
6 Likiwa jema, au likiwa baya, sisi tutaitii sauti ya Bwana, Mungu wetu, ambaye tunakutuma kwake; ipate kuwa faida yetu, tunapoitii sauti ya Bwana, Mungu wetu.
Jérémie 7.23 Deutéronome 5.29 Deutéronome 5.33 Deutéronome 6.2-6.3 Exode 24.7
7 Ikawa, baada ya siku kumi, neno la Bwana likamjia Yeremia.
Psaumes 27.14 Esaïe 28.16 Habakuk 2.3
8 Ndipo akamwita Yohana, mwana wa Karea, na maakida wote wa majeshi waliokuwa pamoja naye, na watu wote tangu wadogo hata wakubwa,
Jérémie 42.1 Jérémie 40.8 Jérémie 40.13 Jérémie 43.2-43.5 Jérémie 41.11-41.16
9 akawaambia, Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye mlinituma kwake, ili niyaweke maombi yenu mbele yake, asema hivi;
Jérémie 42.2 2 Rois 19.4 2 Rois 19.6 2 Rois 22.15-22.20 2 Rois 19.20-19.37
10 Ikiwa mtakaa bado katika nchi hii, ndipo nitawajenga, wala sitawabomoa, nami nitawapanda, wala sitawang’oa; kwa maana nayajutia mabaya niliyowatenda.
Jérémie 24.6 Ezéchiel 36.36 Jérémie 31.28 Deutéronome 32.36 Amos 7.3
11 Msimwogope mfalme wa Babeli, mnayemwogopa; msimwogope, asema Bwana; maana mimi ni pamoja nanyi, niwaokoe, na kuwaponya na mkono wake.
Romains 8.31 Jérémie 1.19 Esaïe 43.5 2 Chroniques 32.7-32.8 Jérémie 41.18
12 Nami nitawapa rehema, kwamba awarehemu ninyi, na kuwarudisha mkae katika nchi yenu wenyewe.
Néhémie 1.11 Proverbes 16.7 Psaumes 106.45-106.46
13 Lakini mkisema, Hatutaki kukaa katika nchi hii; msiitii sauti ya Bwana, Mungu wenu;
Jérémie 44.16 Exode 5.2 Jérémie 42.10
14 mkisema, La! Lakini tutakwenda nchi ya Misri, ambayo hatutaona vita, wala kuisikia sauti ya tarumbeta, wala kuona njaa kwa kukosa chakula; nasi tutakaa huko;
Jérémie 41.17 Jérémie 4.19 Jérémie 4.21 Exode 16.3 Esaïe 31.1
15 basi, lisikieni neno la Bwana, enyi mabaki ya Yuda; Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Ikiwa mwakaza nyuso zenu kuingia Misri, na kwenda kukaa huko;
Deutéronome 17.16 Jérémie 44.12-44.14 Jérémie 42.17 Luc 9.51 Daniel 11.17
16 basi, itakuwa, upanga mnaouogopa utawapata huko, katika nchi ya Misri, nayo njaa mnayoiogopa itawafuatia mbio huko Misri, nanyi mtakufa huko.
Ezéchiel 11.8 Jérémie 44.27 Amos 9.1-9.4 Proverbes 13.21 Jérémie 42.13
17 Haya ndiyo yatakayowapata watu wote waelekezao nyuso zao kwenda Misri, na kukaa huko; watakufa kwa upanga, na kwa njaa, na kwa tauni; hapana mtu awaye yote miongoni mwao atakayesalia, au kuokoka katika mabaya nitakayoyaleta juu yao.
Jérémie 42.22 Jérémie 24.10 Jérémie 44.28 Jérémie 44.13-44.14
18 Maana Bwana wa majeshi Mungu wa Israeli, asema hivi, Kama hasira yangu, na ghadhabu yangu, ilivyomwagwa juu ya hao wakaao Yerusalemu, ndivyo ghadhabu yangu itakavyomwagwa juu yenu, mtakapoingia Misri; nanyi mtakuwa apizo, na ajabu, na laana, na aibu; wala hamtapaona mahali hapa tena.
Jérémie 7.20 Jérémie 18.16 Jérémie 29.18 Jérémie 39.1-39.9 2 Chroniques 36.16-36.19
19 Bwana asema katika habari zenu, enyi mabaki ya Yuda, Msiingie Misri; jueni sana ya kuwa nimewashuhudia hivi leo.
Deutéronome 17.16 Néhémie 9.26 Néhémie 9.29-9.30 Esaïe 30.1-30.7 2 Chroniques 24.19
20 Maana mmetenda kwa hila juu ya nafsi zenu wenyewe; kwa kuwa mmenituma kwa Bwana, Mungu wenu, mkisema, Utuombee kwa Bwana, Mungu wetu, ukatufunulie sawasawa na yote atakayoyanena Bwana, Mungu wetu, nasi tutayatenda;
Psaumes 18.44 Psaumes 65.3 Galates 6.7 Jérémie 17.10 Nombres 16.38
21 nami nimewafunulia haya leo; lakini ninyi hamkuitii sauti ya Bwana, Mungu wenu, katika neno lo lote ambalo amenituma kwenu.
Ezéchiel 2.7 Actes 20.26-20.27 Zacharie 7.11-7.12 Ezéchiel 3.17 Deutéronome 11.26-11.27
22 Basi, sasa jueni sana ya kuwa mtakufa kwa upanga, na kwa njaa, na kwa tauni, katika mahali pale mnapopatamani kwenda na kukaa.
Jérémie 42.17 Osée 9.6 Ezéchiel 6.11 Jérémie 43.11 Ezéchiel 5.3-5.4

Cette Bible est dans le domaine public.