Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 59.6
Bible en Swahili de l’est


Crimes et jugement de Juda

1 Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia;
Esaïe 50.2 Nombres 11.23 Jérémie 32.17 Esaïe 65.24 Hébreux 7.25
2 lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia.
Jérémie 5.25 Michée 3.4 Esaïe 1.15 Ezéchiel 39.23-39.24 Esaïe 57.17
3 Kwa maana mikono yenu imetiwa unajisi kwa damu, na vidole vyenu vimetiwa unajisi kwa uovu; midomo yenu imenena uongo, ndimi zenu zimenong’ona ubaya.
Esaïe 1.15 Jérémie 2.30 Esaïe 1.21 Ezéchiel 7.23 Jérémie 2.34
4 Hapana adaiye kwa haki, wala hapana atetaye kwa kweli; hutumainia ubatili, hunena uongo; hupata mimba ya madhara, na kuzaa uovu.
Job 15.35 Esaïe 30.12 Jérémie 7.8 Jérémie 7.4 Ezéchiel 22.29-22.31
5 Huangua mayai ya fira, na kusuka wavu wa buibui; yeye alaye mayai yao hufa, na hilo livunjwalo hutoka nyoka.
Proverbes 23.32 Matthieu 3.7 Job 8.14 Matthieu 12.34 Esaïe 14.29
6 Nyavu zao hazitakuwa mavazi, wala hawatajifunika kwa kazi zao; kazi zao ni kazi za uovu, na vitendo vya udhalimu vimo mikononi mwao.
Ezéchiel 7.11 Jérémie 6.7 Esaïe 57.12 Job 8.14-8.15 Michée 6.12
7 Miguu yao hukimbilia mabaya, nao hufanya haraka kumwaga damu isiyo na hatia; mawazo yao ni mawazo ya uovu; ukiwa na uharibifu zaonekana katika njia kuu zao.
Proverbes 6.17 Romains 3.15-3.17 Proverbes 1.16 Marc 7.21-7.22 Actes 8.20-8.22
8 Njia ya amani hawaijui; wala hapana hukumu ya haki katika miendo yao; wamejifanyizia njia zilizopotoka; kila apitaye katika njia hizo hajui amani.
Luc 1.79 Esaïe 57.20-57.21 Esaïe 48.22 Osée 4.1-4.2 Matthieu 23.23
9 Kwa sababu hiyo hukumu ya haki i mbali nasi, wala haki haitufikilii; twatazamia nuru, na kumbe! Latokea giza; twatazamia mwanga, lakini twaenda katika giza kuu.
Esaïe 5.30 Lamentations 5.16-5.17 Michée 1.12 Amos 5.18-5.20 Jérémie 8.15
10 Twapapasa-papasa kutafuta ukuta kama kipofu, naam, twapapasa kama watu wasio na macho; twajikwaa wakati wa adhuhuri, kana kwamba ni wakati wa ukungu wa alfajiri; kati yao waliowanda tumekuwa kama wafu.
Deutéronome 28.29 Lamentations 3.6 Job 5.14 Esaïe 8.15 Jean 12.40
11 Sisi sote twanguruma kama dubu; twaomboleza kama hua; twatazamia hukumu ya haki, lakini hapana; na wokovu, lakini u mbali nasi.
Esaïe 38.14 Ezéchiel 7.16 Esaïe 51.20 Psaumes 38.8 Psaumes 85.9
12 Maana makosa yetu yamezidi kuwa mengi mbele zako, na dhambi zetu zashuhudia juu yetu; maana makosa yetu tunayo pamoja nasi, na maovu yetu tumeyajua;
Esdras 9.6 Osée 5.5 Jérémie 14.7 Osée 7.10 Ezéchiel 16.51-16.52
13 katika kukosa na kumkana Bwana, na katika kugeuka tusimfuate Mungu wetu, tukinena jeuri na uasi, na kukusudia maneno ya uongo na kuyatoa moyoni.
Marc 7.21-7.22 Actes 5.3-5.4 Osée 7.13 Esaïe 59.3-59.4 Osée 1.2
14 Na hukumu imegeuka ikaenda nyuma, na haki inasimama mbali sana; maana kweli imeanguka katika njia kuu, na unyofu hauwezi kuingia.
Habakuk 1.4 Esaïe 59.4 Psaumes 82.2-82.5 Michée 3.9-3.11 Esaïe 5.23
15 Naam, kweli imepunguka kabisa, na yeye auachaye uovu ajifanya kuwa mateka; naye Bwana akaona hayo, akachukizwa kwa kuwa hapana hukumu ya haki.
Marc 3.21 Esaïe 48.1 Romains 8.36 Michée 7.2 Jean 10.20
16 Akaona ya kuwa hapana mtu, akastaajabu kwa kuwa hapana mwombezi; basi, mkono wake mwenyewe ndio uliomletea wokovu; na haki yake ndiyo iliyomsaidia.
Psaumes 98.1 Esaïe 52.10 Ezéchiel 22.30 Esaïe 50.2 Marc 6.6
17 Akajivika haki kama deraya kifuani, na chapeo cha wokovu kichwani pake, akajivika mavazi ya kisasi yawe mavazi yake, naye alivikwa wivu kama joho.
Ephésiens 6.17 Ephésiens 6.14 1 Thessaloniciens 5.8 Esaïe 51.9 Romains 13.12-13.14
18 Kadiri ya matendo yao, kwa kadiri iyo hiyo atawalipa, ukali kwao wampingao, malipo kwa adui zake; naye atavirudishia visiwa malipo.
Esaïe 63.6 Jérémie 17.10 Nahum 1.2 Romains 2.6 Matthieu 16.27
19 Basi, wataliogopa jina la Bwana toka magharibi, na utukufu wake toka maawio ya jua; maana yeye atakuja kama mkondo wa mto ufurikao, uendeshwao kwa pumzi ya Bwana.
Psaumes 113.3 Esaïe 49.12 Apocalypse 20.1-20.3 2 Thessaloniciens 2.8 Apocalypse 17.14-17.15
20 Na Mkombozi atakuja Sayuni, kwao waachao maasi yao katika Yakobo, asema Bwana.
Romains 11.26-11.27 Ezéchiel 18.30-18.31 Hébreux 12.14 Joël 2.32 Esaïe 40.9
21 Tena katika habari zangu, hili ndilo agano langu nao, asema Bwana; roho yangu iliyo juu yako, na maneno yangu niliyoyatia kinywani mwako, hayataondoka kinywani mwako, wala kinywani mwa wana wako, wala kinywani mwa wajukuu wako, asema Bwana, tangu leo na hata milele.
Jérémie 31.31-31.34 Hébreux 10.16 Ezéchiel 36.25-36.27 Jérémie 32.38-32.41 2 Corinthiens 3.17-3.18

Cette Bible est dans le domaine public.