Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 59.15
Bible en Swahili de l’est


Crimes et jugement de Juda

1 Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia;
Esaïe 50.2 Jérémie 32.17 Nombres 11.23 Esaïe 65.24 Hébreux 7.25
2 lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia.
Jérémie 5.25 Esaïe 1.15 Michée 3.4 Ezéchiel 39.23-39.24 Josué 7.11
3 Kwa maana mikono yenu imetiwa unajisi kwa damu, na vidole vyenu vimetiwa unajisi kwa uovu; midomo yenu imenena uongo, ndimi zenu zimenong’ona ubaya.
Esaïe 1.15 Jérémie 2.34 Osée 4.2 Jérémie 2.30 Esaïe 1.21
4 Hapana adaiye kwa haki, wala hapana atetaye kwa kweli; hutumainia ubatili, hunena uongo; hupata mimba ya madhara, na kuzaa uovu.
Job 15.35 Jérémie 7.4 Esaïe 30.12 Jérémie 7.8 Job 15.31
5 Huangua mayai ya fira, na kusuka wavu wa buibui; yeye alaye mayai yao hufa, na hilo livunjwalo hutoka nyoka.
Matthieu 3.7 Job 8.14 Matthieu 12.34 Esaïe 14.29 Proverbes 23.32
6 Nyavu zao hazitakuwa mavazi, wala hawatajifunika kwa kazi zao; kazi zao ni kazi za uovu, na vitendo vya udhalimu vimo mikononi mwao.
Jérémie 6.7 Esaïe 57.12 Ezéchiel 7.11 Esaïe 58.4 Michée 2.1-2.3
7 Miguu yao hukimbilia mabaya, nao hufanya haraka kumwaga damu isiyo na hatia; mawazo yao ni mawazo ya uovu; ukiwa na uharibifu zaonekana katika njia kuu zao.
Marc 7.21-7.22 Proverbes 6.17 Romains 3.15-3.17 Proverbes 1.16 Proverbes 24.9
8 Njia ya amani hawaijui; wala hapana hukumu ya haki katika miendo yao; wamejifanyizia njia zilizopotoka; kila apitaye katika njia hizo hajui amani.
Luc 1.79 Esaïe 57.20-57.21 Esaïe 48.22 Romains 3.17 Proverbes 28.18
9 Kwa sababu hiyo hukumu ya haki i mbali nasi, wala haki haitufikilii; twatazamia nuru, na kumbe! Latokea giza; twatazamia mwanga, lakini twaenda katika giza kuu.
Esaïe 5.30 Jérémie 8.15 1 Thessaloniciens 5.3 Habakuk 1.13 Jérémie 14.19
10 Twapapasa-papasa kutafuta ukuta kama kipofu, naam, twapapasa kama watu wasio na macho; twajikwaa wakati wa adhuhuri, kana kwamba ni wakati wa ukungu wa alfajiri; kati yao waliowanda tumekuwa kama wafu.
Deutéronome 28.29 Lamentations 3.6 Job 5.14 Proverbes 4.19 1 Jean 2.11
11 Sisi sote twanguruma kama dubu; twaomboleza kama hua; twatazamia hukumu ya haki, lakini hapana; na wokovu, lakini u mbali nasi.
Esaïe 38.14 Ezéchiel 7.16 Psaumes 119.155 Psaumes 32.3-32.4 Jérémie 8.15
12 Maana makosa yetu yamezidi kuwa mengi mbele zako, na dhambi zetu zashuhudia juu yetu; maana makosa yetu tunayo pamoja nasi, na maovu yetu tumeyajua;
Esdras 9.6 Osée 5.5 Jérémie 14.7 Néhémie 9.33 Matthieu 23.32-23.33
13 katika kukosa na kumkana Bwana, na katika kugeuka tusimfuate Mungu wetu, tukinena jeuri na uasi, na kukusudia maneno ya uongo na kuyatoa moyoni.
Marc 7.21-7.22 Jérémie 2.13 Jérémie 2.19-2.21 Psaumes 78.36 Jérémie 42.20
14 Na hukumu imegeuka ikaenda nyuma, na haki inasimama mbali sana; maana kweli imeanguka katika njia kuu, na unyofu hauwezi kuingia.
Habakuk 1.4 Esaïe 1.21 Sophonie 3.1-3.3 Amos 5.11 Esaïe 10.1-10.2
15 Naam, kweli imepunguka kabisa, na yeye auachaye uovu ajifanya kuwa mateka; naye Bwana akaona hayo, akachukizwa kwa kuwa hapana hukumu ya haki.
Jérémie 29.26 Actes 9.1 2 Corinthiens 5.13 Jean 8.52 Psaumes 5.9
16 Akaona ya kuwa hapana mtu, akastaajabu kwa kuwa hapana mwombezi; basi, mkono wake mwenyewe ndio uliomletea wokovu; na haki yake ndiyo iliyomsaidia.
Psaumes 98.1 Ezéchiel 22.30 Esaïe 52.10 Jérémie 5.1 Esaïe 63.3-63.5
17 Akajivika haki kama deraya kifuani, na chapeo cha wokovu kichwani pake, akajivika mavazi ya kisasi yawe mavazi yake, naye alivikwa wivu kama joho.
Ephésiens 6.17 Ephésiens 6.14 1 Thessaloniciens 5.8 Romains 13.12-13.14 Esaïe 51.9
18 Kadiri ya matendo yao, kwa kadiri iyo hiyo atawalipa, ukali kwao wampingao, malipo kwa adui zake; naye atavirudishia visiwa malipo.
Esaïe 63.6 Jérémie 17.10 Matthieu 16.27 Lamentations 4.11 Job 34.11
19 Basi, wataliogopa jina la Bwana toka magharibi, na utukufu wake toka maawio ya jua; maana yeye atakuja kama mkondo wa mto ufurikao, uendeshwao kwa pumzi ya Bwana.
Psaumes 113.3 Esaïe 49.12 Apocalypse 20.1-20.3 Apocalypse 12.10 Zacharie 4.6
20 Na Mkombozi atakuja Sayuni, kwao waachao maasi yao katika Yakobo, asema Bwana.
Romains 11.26-11.27 Hébreux 12.14 Ezéchiel 18.30-18.31 Actes 3.19 Tite 2.11-2.14
21 Tena katika habari zangu, hili ndilo agano langu nao, asema Bwana; roho yangu iliyo juu yako, na maneno yangu niliyoyatia kinywani mwako, hayataondoka kinywani mwako, wala kinywani mwa wana wako, wala kinywani mwa wajukuu wako, asema Bwana, tangu leo na hata milele.
Jérémie 31.31-31.34 Hébreux 10.16 Ezéchiel 36.25-36.27 Jérémie 32.38-32.41 2 Corinthiens 3.17-3.18

Cette Bible est dans le domaine public.