Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 34.13
Bible en Swahili de l’est


Prophétie sur Édom

1 Karibuni, enyi mataifa, mpate kusikia; sikilizeni, enyi kabila za watu; dunia na isikie, nacho kiijazacho, ulimwengu na vitu vyote viutokavyo.
Esaïe 41.1 Esaïe 43.9 Deutéronome 32.1 Esaïe 1.2 Juges 5.31
2 Maana Bwana ana ghadhabu juu ya mataifa yote, na hasira kali juu ya jeshi lao lote; amewaangamiza kabisa, amewatoa waende kuchinjwa.
Zacharie 14.3 Esaïe 30.27-30.30 Apocalypse 20.15 Romains 1.18 Nahum 1.2-1.6
3 Watu wao waliouawa watatupwa nje, na uvundo wa maiti zao utapaa juu, na milima itayeyushwa kwa damu yao.
Joël 2.20 Esaïe 34.7 Ezéchiel 39.4 Jérémie 8.1-8.2 2 Rois 9.35-9.37
4 Na jeshi lote la mbinguni litafumuliwa, na mbingu zitakunjwa kama karatasi, na jeshi lao lote litanyauka kama vile jani la mzabibu linyaukavyo na kupukutika, na kama jani la mtini linyaukavyo na kupukutika.
Matthieu 24.29 Apocalypse 6.13-6.14 Ezéchiel 32.7-32.8 Joël 3.15 Esaïe 14.12
5 Maana upanga wangu umekunywa na kushiba mbinguni; tazama, utashukia Edomu, na juu ya watu wa laana yangu, ili kuwahukumu.
Malachie 1.4 Jérémie 46.10 Amos 1.11-1.12 Esaïe 63.1 Ezéchiel 21.3-21.5
6 Upanga wa Bwana umeshiba damu, umenona kwa unono, kwa damu ya wana-kondoo na mbuzi, kwa mafuta ya figo za kondoo waume; maana Bwana ana dhabihu huko Bozra, machinjo makubwa katika nchi ya Edomu.
Esaïe 63.1 Jérémie 49.13 Sophonie 1.7 Esaïe 34.5 Ezéchiel 21.4-21.5
7 Na nyati watatelemka pamoja nao, na mahasai pamoja na mafahali, na nchi yao italewa kwa damu, na mavumbi yake yatanoneshwa kwa shahamu.
Psaumes 68.30 Nombres 23.22 Jérémie 50.27 Jérémie 46.21 Nombres 24.8
8 Maana ni siku ya kisasi cha Bwana, mwaka wa malipo, ili kushindania Sayuni.
Esaïe 63.4 Esaïe 61.2 Psaumes 94.1 Esaïe 35.4 Apocalypse 18.20
9 Na vijito vyake vitageuzwa kuwa lami, na mavumbi yake yatageuzwa kuwa kiberiti, na ardhi yake itakuwa lami iwakayo.
Deutéronome 29.23 Psaumes 11.6 Apocalypse 21.8 Genèse 19.28 Job 18.15
10 Haitazimwa mchana wala usiku, moshi wake utapaa milele; tangu kizazi hata kizazi itakuwa ukiwa; hapana mtu atakayepita kati yake milele na milele.
Apocalypse 19.3 Esaïe 66.24 Esaïe 13.20 Malachie 1.3-1.4 Apocalypse 18.18
11 Kaati na nungu wataimiliki, bundi na kunguru watakaa huko, naye atanyosha juu yake kamba ya ukiwa na timazi ya utupu.
Lamentations 2.8 2 Rois 21.13 Sophonie 2.14 Apocalypse 18.2 Esaïe 14.23
12 Watawaitia wakuu wake ufalme, lakini hawatakuwapo; wakuu wake wote wamekuwa si kitu.
Esaïe 41.24 Esaïe 41.11-41.12 Esaïe 3.6-3.8 1 Corinthiens 8.4 Jérémie 39.6
13 Miiba itamea majumbani mwake, upupu na mbigili ndani ya maboma yake; nayo itakuwa kao la mbweha, na ua la mbuni.
Jérémie 10.22 Jérémie 9.11 Malachie 1.3 Psaumes 44.19 Esaïe 32.13-32.14
14 Na hayawani wa nyikani watakutana na mbwa-mwitu, na beberu anamwita mwenziwe; naam, babewatoto anakaa huko na kujipatia raha.
Esaïe 13.21-13.22
15 Huko pili atafanya kioto chake na kuzaa na kuotamia, na kukusanya watoto wake katika kivuli chake; naam, huko watakusanyika tai, kila mmoja na mwenzake.
Deutéronome 14.13
16 Tafuteni katika kitabu cha Bwana mkasome; hapana katika hao wote atakayekosa kuwapo, hapana mmoja atakayemkosa mwenzake; kwa maana kinywa changu kimeamuru, na roho yake imewakusanya.
Josué 1.8 Psaumes 33.9 Psaumes 33.6 Esaïe 30.8 Jean 10.35
17 Naye amewapigia kura, na mkono wake umewagawanyia kwa kamba; wataimiliki hata milele, watakaa ndani yake kizazi hata kizazi.
Esaïe 34.10 Psaumes 78.55 Actes 13.19 Esaïe 17.14 Josué 18.8

Cette Bible est dans le domaine public.