Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 30.8
Bible en Swahili de l’est


Annonce de la punition de Juda

1 Ole wa watoto waasi; asema Bwana; watakao mashauri lakini hawayataki kwangu mimi; wajifunikao kifuniko lakini si cha roho yangu; wapate kuongeza dhambi juu ya dhambi;
Esaïe 1.2 Esaïe 29.15 Esaïe 65.2 Esaïe 30.9 Actes 7.51-7.52
2 waendao kutelemkia Misri wala hawakuuliza kinywani mwangu; ili wajitie nguvu kwa nguvu za Farao, na kutumainia kivuli cha Misri.
Jérémie 43.7 Esaïe 36.6 Nombres 27.21 Jérémie 21.2 Esaïe 36.9
3 Basi, nguvu za Farao zitakuwa aibu yenu, na kutumainia kivuli cha Misri kutakuwa kufadhaika kwenu.
Esaïe 20.5 Romains 5.5 Jérémie 37.5-37.10 Esaïe 36.6 Esaïe 45.16-45.17
4 Kwa maana wakuu wake wako Soani, na wajumbe wake wamefika Hanesi.
Esaïe 19.11 Jérémie 43.7 Nombres 13.22 Esaïe 57.9 Ezéchiel 30.18
5 Wote watawaonea haya watu wasioweza kuwafaidia, wasio na msaada wala faida, bali ni aibu na sababu ya kushutumiwa.
Jérémie 2.36 Esaïe 30.7 Esaïe 30.16 Esaïe 20.5-20.6 Esaïe 31.1-31.3
6 Ufunuo juu ya hayawani wa Negebu. Katikati ya nchi ya taabu na dhiki, Ambayo hutoka huko simba jike na simba, Nyoka na joka la moto arukaye, Huchukua mali zao mabegani mwa punda wachanga, Na hazina zao juu ya nundu za ngamia Waende kwa watu ambao hawatawafaa kitu.
Deutéronome 8.15 Esaïe 46.1-46.2 Jérémie 11.4 Deutéronome 4.20 1 Rois 10.2
7 Kwa maana Misri huwasaidia bure, bila faida; Kwa hiyo nimemwita, Rahabu aketiye kimya.
Osée 5.13 Psaumes 76.8-76.9 Esaïe 28.12 Esaïe 30.15 Exode 14.13
8 Haya, enenda sasa, andika neno hili katika kibao mbele ya macho yao, lichore katika kitabu ili liwe kwa ajili ya majira yatakayokuja, kwa ushuhuda hata milele.
Esaïe 8.1 Habakuk 2.2 Deutéronome 4.30 Ezéchiel 38.16 Job 19.23-19.25
9 Kwa maana watu hawa ni watu waasi, watoto wasemao uongo, watoto wasiotaka kuisikia sheria ya Bwana;
Esaïe 30.1 Matthieu 23.31-23.33 Actes 7.51 Esaïe 63.8 2 Chroniques 33.10
10 wawaambiao waonaji, Msione; na manabii, Msitoe unabii wa mambo ya haki, tuambieni maneno laini, hubirini maneno yadanganyayo;
Amos 7.13 Jérémie 11.21 Romains 16.18 Amos 2.12 Ezéchiel 13.7-13.10
11 tokeni katika njia, geukeni mtoke katika mapito; mkomesheni Mtakatifu wa Israeli mbele yetu.
Job 21.14 Romains 1.28 Amos 7.13 Esaïe 29.21 Romains 8.7
12 Basi kwa ajili ya hayo Mtakatifu wa Israeli asema hivi, Kwa sababu mwalidharau neno hili, na kutumainia jeuri na ukaidi, na kuyategemea hayo;
Esaïe 5.24 Psaumes 52.7 Esaïe 47.10 Psaumes 62.10 Esaïe 30.7
13 basi, uovu huu utakuwa kwenu kama mahali palipobomoka, palipo tayari kuanguka patokezapo katika ukuta mrefu, ambapo kuvunjika kwake huja ghafula kwa mara moja.
Esaïe 29.5 Psaumes 62.3 1 Rois 20.30 Luc 6.49 Psaumes 73.19-73.20
14 Naye atapavunja kama chombo cha mfinyanzi kivunjwavyo, akikivunja-vunja asiache kukivunja, hata hakipatikani katika vipande vyake kigae kitoshacho kutwaa moto jikoni, au kuteka maji kisimani.
Psaumes 2.9 Jérémie 19.10-19.11 Romains 11.21 2 Pierre 2.4-2.5 Apocalypse 2.27
15 Kwa maana Bwana MUNGU, Mtakatifu wa Israeli, asema hivi, Kwa kurudi na kustarehe mtaokolewa; nguvu zenu zitakuwa katika kutulia na kutumaini; lakini hamkukubali.
Esaïe 32.17 Luc 13.34 Esaïe 26.3-26.4 Jérémie 3.22-3.23 2 Chroniques 16.8
16 Bali ninyi mlisema, La! Maana tutakimbia juu ya farasi; basi, ni kweli, mtakimbia; tena, Sisi tutakimbia juu ya wanyama waendao upesi; basi, wale watakaowafuatia watakuwa wepesi.
Esaïe 31.1 Esaïe 31.3 Deutéronome 28.25 Psaumes 33.17 Jérémie 52.7
17 Elfu moja watakimbia kwa kukemewa na mtu mmoja; kwa kukemewa na watano mtakimbia; hata mtakapoachwa kama mlingoti juu ya kilele cha mlima, na kama bendera juu ya kilima.
Lévitique 26.8 Deutéronome 28.25 Deutéronome 32.30 Lévitique 26.36 Josué 23.10

Promesses pour l’avenir

18 Kwa ajili ya hayo Bwana atangoja, ili awaonee huruma, na kwa ajili ya hayo atatukuzwa, ili awarehemu; kwa maana Bwana ni Mungu wa hukumu; heri wote wamngojao.
Proverbes 16.20 2 Pierre 3.9 Psaumes 34.8 2 Pierre 3.15 Jérémie 17.7
19 Kwa maana watu watakaa katika Sayuni huko Yerusalemu; wewe hutalia tena; hakika yake atakuonea rehema nyingi kwa sauti ya kilio chako; asikiapo ndipo atakapokujibu.
Esaïe 65.24 Esaïe 60.20 Matthieu 7.7-7.11 Esaïe 58.9 Psaumes 50.15
20 Na ingawa Bwana atawapeni chakula cha shida na maji ya msiba, lakini waalimu wako hawatafichwa tena, ila macho yako yatawaona waalimu wako;
1 Rois 22.27 Psaumes 74.9 Psaumes 127.2 Psaumes 80.5 Actes 14.22
21 na masikio yako yatasikia neno nyuma yako, likisema, Njia ni hii, ifuateni; mgeukapo kwenda mkono wa kulia, na mgeukapo kwenda mkono wa kushoto.
Psaumes 32.8 Proverbes 3.5-3.6 Esaïe 58.11 Esaïe 35.8-35.9 Psaumes 25.8-25.9
22 Nanyi mtakitia najisi kifuniko cha sanamu zenu za fedha zilizochongwa, na mabamba ya sanamu zenu za dhahabu zilizoyeyushwa; utazitupilia mbali kama kitu kilicho najisi; utasema, Haya, toka hapa.
Juges 17.3-17.4 Esaïe 46.6 Osée 14.8 Esaïe 31.7 Esaïe 17.7-17.8
23 Naye atatoa mvua juu ya mbegu zako, upate kuipanda nchi hii; na mkate wa mazao ya nchi, nayo itasitawi na kuzaa tele; katika siku hiyo ng’ombe zako watakula katika malisho mapana.
Esaïe 32.20 1 Timothée 4.8 Zacharie 8.11-8.12 Psaumes 65.9-65.13 Psaumes 104.13-104.14
24 Ng’ombe pia na wana-punda wailimao nchi watakula chakula kilichokolea, kilichopepetwa kwa ungo na kwa pepeo.
Genèse 45.6 Matthieu 3.12 Luc 3.17 1 Corinthiens 9.9-9.10 1 Samuel 8.12
25 Na juu ya kila mlima mrefu, na juu ya kila kilima kilichoinuka, itakuwapo mito na vijito vya maji, katika siku ya machinjo makuu itakapoanguka minara.
Esaïe 43.19-43.20 Esaïe 35.6-35.7 Esaïe 41.18-41.19 Jean 7.38 2 Corinthiens 10.4
26 Na tena nuru ya mwezi itakuwa kama nuru ya jua, na nuru ya jua itaongezeka mara saba, kama nuru ya siku saba, katika siku ile Bwana atakapofunga mapigo ya watu wake, na kuliponya pigo la jeraha yao.
Deutéronome 32.39 Esaïe 60.19-60.20 Job 5.18 Apocalypse 22.5 Esaïe 24.23

Jugement des Assyriens

27 Tazama, jina la Bwana linakuja kutoka mbali sana, linawaka kwa hasira yake, kwa moshi mwingi sana unaopaa juu; midomo yake imejaa ghadhabu, na ulimi wake ni moto ulao;
Esaïe 10.5 Deutéronome 33.2 Esaïe 59.19 Nahum 1.5-1.6 Sophonie 3.8
28 na pumzi yake ni kijito kifurikacho, kifikacho hata shingoni, kupepeta mataifa kwa ungo wa ubatili; na lijamu ikoseshayo itakuwa katika taya za watu.
Esaïe 37.29 2 Thessaloniciens 2.8 Esaïe 8.8 Esaïe 11.4 Amos 9.9
29 Mtakuwa na wimbo kama vile wakati wa usiku, ishikwapo sikukuu takatifu, mtakuwa na furaha ya moyo kama vile mtu aendapo na filimbi katika mlima wa Bwana, aliye Mwamba wa Israeli.
Psaumes 42.4 Esaïe 26.4 Esaïe 2.3 Deutéronome 16.6 Psaumes 32.7
30 Naye Bwana atawasikizisha watu sauti yake ya utukufu, naye atawaonyesha jinsi mkono wake ushukavyo, na ghadhabu ya hasira yake, na mwako wa moto ulao, pamoja na dhoruba, na tufani, na mvua ya mawe ya barafu.
Psaumes 18.13-18.14 Josué 10.11 Esaïe 28.2 Esaïe 29.6 Exode 15.16
31 Maana kwa sauti ya Bwana, Mwashuri atavunjika-vunjika, yeye apigaye kwa bakora.
Esaïe 11.4 Esaïe 9.4 Esaïe 10.5 Esaïe 10.24 Esaïe 30.30
32 Na kila pigo la fimbo iliyoamriwa, ambayo Bwana ataliweka juu yake, litakuwa pamoja na matari na vinanda, na kwa mapigano yenye kutikisa atapigana nao.
Esaïe 11.15 Esaïe 19.16 Esaïe 2.19 1 Samuel 10.5 Esaïe 30.29
33 Maana Tofethi imewekwa tayari tokea zamani, naam, imewekwa tayari kwa mfalme huyo; ameifanya kubwa, inakwenda chini sana; tanuru yake ni moto na kuni nyingi; pumzi ya Bwana, kama mto wa kiberiti, huiwasha.
2 Rois 23.10 Genèse 19.24 Jude 1.4 Jérémie 19.6 Esaïe 14.9-14.20

Cette Bible est dans le domaine public.