Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 30.1
Bible en Swahili de l’est


Annonce de la punition de Juda

1 Ole wa watoto waasi; asema Bwana; watakao mashauri lakini hawayataki kwangu mimi; wajifunikao kifuniko lakini si cha roho yangu; wapate kuongeza dhambi juu ya dhambi;
Esaïe 1.2 Esaïe 29.15 Esaïe 30.9 Esaïe 65.2 Psaumes 61.4
2 waendao kutelemkia Misri wala hawakuuliza kinywani mwangu; ili wajitie nguvu kwa nguvu za Farao, na kutumainia kivuli cha Misri.
Esaïe 36.6 Nombres 27.21 Jérémie 43.7 Esaïe 31.1-31.3 Jérémie 42.2
3 Basi, nguvu za Farao zitakuwa aibu yenu, na kutumainia kivuli cha Misri kutakuwa kufadhaika kwenu.
Esaïe 20.5 Romains 10.11 Esaïe 30.5-30.7 Romains 5.5 Jérémie 37.5-37.10
4 Kwa maana wakuu wake wako Soani, na wajumbe wake wamefika Hanesi.
Esaïe 19.11 Jérémie 43.7 2 Rois 17.4 Osée 7.16 Ezéchiel 30.14
5 Wote watawaonea haya watu wasioweza kuwafaidia, wasio na msaada wala faida, bali ni aibu na sababu ya kushutumiwa.
Jérémie 2.36 Esaïe 30.7 Esaïe 30.16 Esaïe 20.5-20.6 Esaïe 31.1-31.3
6 Ufunuo juu ya hayawani wa Negebu. Katikati ya nchi ya taabu na dhiki, Ambayo hutoka huko simba jike na simba, Nyoka na joka la moto arukaye, Huchukua mali zao mabegani mwa punda wachanga, Na hazina zao juu ya nundu za ngamia Waende kwa watu ambao hawatawafaa kitu.
Deutéronome 8.15 Jérémie 11.4 Esaïe 46.1-46.2 1 Rois 10.2 Deutéronome 4.20
7 Kwa maana Misri huwasaidia bure, bila faida; Kwa hiyo nimemwita, Rahabu aketiye kimya.
Esaïe 7.4 Jérémie 37.7 Esaïe 51.9 Esaïe 2.22 Esaïe 31.1-31.5
8 Haya, enenda sasa, andika neno hili katika kibao mbele ya macho yao, lichore katika kitabu ili liwe kwa ajili ya majira yatakayokuja, kwa ushuhuda hata milele.
Habakuk 2.2 Esaïe 8.1 Deutéronome 31.19 1 Timothée 4.1 Deutéronome 31.29
9 Kwa maana watu hawa ni watu waasi, watoto wasemao uongo, watoto wasiotaka kuisikia sheria ya Bwana;
Esaïe 30.1 Deutéronome 31.27-31.29 Esaïe 28.15 Zacharie 7.11-7.12 Apocalypse 21.8
10 wawaambiao waonaji, Msione; na manabii, Msitoe unabii wa mambo ya haki, tuambieni maneno laini, hubirini maneno yadanganyayo;
Amos 7.13 Romains 16.18 Amos 2.12 Jérémie 11.21 Jérémie 23.17
11 tokeni katika njia, geukeni mtoke katika mapito; mkomesheni Mtakatifu wa Israeli mbele yetu.
Ephésiens 4.18 Romains 1.30 Job 21.14 Romains 1.28 Amos 7.13
12 Basi kwa ajili ya hayo Mtakatifu wa Israeli asema hivi, Kwa sababu mwalidharau neno hili, na kutumainia jeuri na ukaidi, na kuyategemea hayo;
Esaïe 5.24 Luc 10.16 Jérémie 13.25 2 Samuel 12.9-12.10 Esaïe 31.1-31.3
13 basi, uovu huu utakuwa kwenu kama mahali palipobomoka, palipo tayari kuanguka patokezapo katika ukuta mrefu, ambapo kuvunjika kwake huja ghafula kwa mara moja.
1 Rois 20.30 Esaïe 29.5 Psaumes 62.3 1 Thessaloniciens 5.1-5.3 Proverbes 29.1
14 Naye atapavunja kama chombo cha mfinyanzi kivunjwavyo, akikivunja-vunja asiache kukivunja, hata hakipatikani katika vipande vyake kigae kitoshacho kutwaa moto jikoni, au kuteka maji kisimani.
Psaumes 2.9 Jérémie 19.10-19.11 Romains 11.21 2 Pierre 2.4-2.5 Apocalypse 2.27
15 Kwa maana Bwana MUNGU, Mtakatifu wa Israeli, asema hivi, Kwa kurudi na kustarehe mtaokolewa; nguvu zenu zitakuwa katika kutulia na kutumaini; lakini hamkukubali.
Esaïe 32.17 Luc 13.34 Esaïe 26.3-26.4 Esaïe 7.4 Jean 5.40
16 Bali ninyi mlisema, La! Maana tutakimbia juu ya farasi; basi, ni kweli, mtakimbia; tena, Sisi tutakimbia juu ya wanyama waendao upesi; basi, wale watakaowafuatia watakuwa wepesi.
Esaïe 31.1 Esaïe 31.3 Esaïe 5.26-5.30 Habakuk 1.8 Esaïe 10.28-10.32
17 Elfu moja watakimbia kwa kukemewa na mtu mmoja; kwa kukemewa na watano mtakimbia; hata mtakapoachwa kama mlingoti juu ya kilele cha mlima, na kama bendera juu ya kilima.
Lévitique 26.36 Josué 23.10 Lévitique 26.8 Deutéronome 28.25 Deutéronome 32.30

Promesses pour l’avenir

18 Kwa ajili ya hayo Bwana atangoja, ili awaonee huruma, na kwa ajili ya hayo atatukuzwa, ili awarehemu; kwa maana Bwana ni Mungu wa hukumu; heri wote wamngojao.
Proverbes 16.20 2 Pierre 3.9 Esaïe 8.17 Esaïe 25.9 Luc 15.20
19 Kwa maana watu watakaa katika Sayuni huko Yerusalemu; wewe hutalia tena; hakika yake atakuonea rehema nyingi kwa sauti ya kilio chako; asikiapo ndipo atakapokujibu.
Esaïe 60.20 Esaïe 65.24 Psaumes 50.15 Matthieu 7.7-7.11 Esaïe 58.9
20 Na ingawa Bwana atawapeni chakula cha shida na maji ya msiba, lakini waalimu wako hawatafichwa tena, ila macho yako yatawaona waalimu wako;
1 Rois 22.27 Psaumes 74.9 Psaumes 80.5 Actes 14.22 Psaumes 127.2
21 na masikio yako yatasikia neno nyuma yako, likisema, Njia ni hii, ifuateni; mgeukapo kwenda mkono wa kulia, na mgeukapo kwenda mkono wa kushoto.
Psaumes 32.8 Proverbes 3.5-3.6 Esaïe 58.11 Esaïe 35.8-35.9 Esaïe 42.16
22 Nanyi mtakitia najisi kifuniko cha sanamu zenu za fedha zilizochongwa, na mabamba ya sanamu zenu za dhahabu zilizoyeyushwa; utazitupilia mbali kama kitu kilicho najisi; utasema, Haya, toka hapa.
Juges 17.3-17.4 Esaïe 46.6 Esaïe 31.7 Osée 14.8 2 Rois 23.4-23.20
23 Naye atatoa mvua juu ya mbegu zako, upate kuipanda nchi hii; na mkate wa mazao ya nchi, nayo itasitawi na kuzaa tele; katika siku hiyo ng’ombe zako watakula katika malisho mapana.
Esaïe 32.20 1 Timothée 4.8 Zacharie 8.11-8.12 Psaumes 65.9-65.13 Psaumes 104.13-104.14
24 Ng’ombe pia na wana-punda wailimao nchi watakula chakula kilichokolea, kilichopepetwa kwa ungo na kwa pepeo.
Genèse 45.6 Deutéronome 21.4 Exode 34.21 Matthieu 3.12 Luc 3.17
25 Na juu ya kila mlima mrefu, na juu ya kila kilima kilichoinuka, itakuwapo mito na vijito vya maji, katika siku ya machinjo makuu itakapoanguka minara.
Esaïe 35.6-35.7 Esaïe 43.19-43.20 Esaïe 34.2-34.10 Ezéchiel 34.26 Esaïe 63.1-63.6
26 Na tena nuru ya mwezi itakuwa kama nuru ya jua, na nuru ya jua itaongezeka mara saba, kama nuru ya siku saba, katika siku ile Bwana atakapofunga mapigo ya watu wake, na kuliponya pigo la jeraha yao.
Esaïe 60.19-60.20 Deutéronome 32.39 Apocalypse 22.5 Esaïe 24.23 Apocalypse 21.23

Jugement des Assyriens

27 Tazama, jina la Bwana linakuja kutoka mbali sana, linawaka kwa hasira yake, kwa moshi mwingi sana unaopaa juu; midomo yake imejaa ghadhabu, na ulimi wake ni moto ulao;
Daniel 7.9 Esaïe 33.12 Deutéronome 32.22 Hébreux 12.29 Psaumes 79.5
28 na pumzi yake ni kijito kifurikacho, kifikacho hata shingoni, kupepeta mataifa kwa ungo wa ubatili; na lijamu ikoseshayo itakuwa katika taya za watu.
Esaïe 37.29 Esaïe 8.8 Esaïe 11.4 2 Thessaloniciens 2.8 2 Rois 19.28
29 Mtakuwa na wimbo kama vile wakati wa usiku, ishikwapo sikukuu takatifu, mtakuwa na furaha ya moyo kama vile mtu aendapo na filimbi katika mlima wa Bwana, aliye Mwamba wa Israeli.
Psaumes 42.4 Esaïe 26.4 Esaïe 2.3 1 Chroniques 13.7-13.8 Jérémie 19.1-19.7
30 Naye Bwana atawasikizisha watu sauti yake ya utukufu, naye atawaonyesha jinsi mkono wake ushukavyo, na ghadhabu ya hasira yake, na mwako wa moto ulao, pamoja na dhoruba, na tufani, na mvua ya mawe ya barafu.
Psaumes 18.13-18.14 Esaïe 28.2 Esaïe 29.6 Josué 10.11 Apocalypse 16.18-16.21
31 Maana kwa sauti ya Bwana, Mwashuri atavunjika-vunjika, yeye apigaye kwa bakora.
Esaïe 10.5 Esaïe 11.4 Esaïe 9.4 Esaïe 37.32-37.38 Esaïe 10.15
32 Na kila pigo la fimbo iliyoamriwa, ambayo Bwana ataliweka juu yake, litakuwa pamoja na matari na vinanda, na kwa mapigano yenye kutikisa atapigana nao.
Esaïe 11.15 Esaïe 19.16 Esaïe 2.19 Job 21.11-21.12 Ezéchiel 32.10
33 Maana Tofethi imewekwa tayari tokea zamani, naam, imewekwa tayari kwa mfalme huyo; ameifanya kubwa, inakwenda chini sana; tanuru yake ni moto na kuni nyingi; pumzi ya Bwana, kama mto wa kiberiti, huiwasha.
2 Rois 23.10 Genèse 19.24 Jérémie 19.6 Jude 1.4 Hébreux 13.8

Cette Bible est dans le domaine public.