Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 23.1
Bible en Swahili de l’est


Prophétie sur Tyr

1 Ufunuo juu ya Tiro. Toeni sauti za uchungu, enyi merikebu za Tarshishi, kwa maana umeharibika kabisa, hata hapana nyumba, hapana mahali pa kuingia; toka nchi ya Kitimu wamefunuliwa habari.
Joël 3.4-3.8 Jérémie 47.4 Jérémie 25.22 Genèse 10.4 Esaïe 2.16
2 Tulieni, enyi mkaao kisiwani; wewe ambaye wafanya biashara wa Sidoni, wavukao bahari, walikujaza.
Esaïe 47.5 Psaumes 46.10 Ezéchiel 28.2 Habakuk 2.20 Ezéchiel 27.8-27.36
3 Vitu vilivyopandwa, vya Shihori, mavuno ya Nile, yaliyokuja juu ya maji mengi, ndiyo pato lake, naye alikuwa soko la mataifa.
Jérémie 2.18 1 Chroniques 13.5 Joël 3.5 Ezéchiel 28.4 Apocalypse 18.11-18.13
4 Tahayari, Ee Sidoni; kwa maana bahari imenena, hiyo ngome ya bahari ilisema, Sikuona utungu, wala sikuzaa, wala sikulea vijana, wala sikulea wanawali.
Apocalypse 18.23 Genèse 10.19 Jérémie 47.3-47.4 Genèse 10.15 Osée 9.11-9.14
5 Habari itakapofika Misri wataona uchungu sana kwa sababu ya habari ya Tiro.
Exode 15.14-15.16 Josué 2.9-2.11 Ezéchiel 27.29-27.36 Apocalypse 18.17-18.19 Ezéchiel 28.19
6 Piteni mpaka Tarshishi, enyi mkaao kisiwani, toeni sauti ya uchungu.
Esaïe 23.12 Esaïe 23.1-23.2 Esaïe 23.10 Esaïe 21.15 Esaïe 16.7
7 Je! Huu ndio mji wenu wa furaha, ambao mwanzo wake ulikuwako tangu siku za kale, ambao miguu yake ilimchukua akae mbali sana?
Esaïe 22.2 Esaïe 47.1-47.2 Josué 19.29 Esaïe 32.13 Ecclésiaste 10.7
8 Ni nani aliyefanya shauri hili juu ya Tiro, uliotia watu taji, ambao wafanya biashara wake walikuwa wana wa wafalme, na wachuuzi wake ni watu wakuu wa dunia?
Esaïe 36.9 Ezéchiel 28.2-28.6 Ezéchiel 28.12-28.18 Esaïe 10.8 Jérémie 50.44-50.45
9 Bwana wa majeshi ndiye aliyefanya shauri hili, ili kuharibu kiburi cha utukufu wote, na kuwaaibisha watu wa duniani wote pia.
Esaïe 13.11 Daniel 4.37 Esaïe 2.11 Job 40.11-40.12 Actes 4.28
10 Pita katika nchi yako, kama Nile, Ee binti wa Tarshishi, hapana tena mshipi wa kukuzuia.
Lamentations 1.6 Esaïe 23.14 Job 12.21 Romains 5.6 1 Samuel 28.20
11 Amenyosha mkono wake juu ya bahari, amezitikisa falme; Bwana ametoa amri katika habari za Kanaani, kuziangamiza ngome zake.
Zacharie 9.3-9.4 Exode 14.21 Esaïe 2.19 Exode 15.8-15.10 Genèse 9.25
12 Naye akasema, Usizidi kufurahi, ewe bikira uliyeaibishwa, binti wa Sidoni, haya, ondoka, uende hata Kitimu; huko nako hutapata raha.
Apocalypse 18.22 Esaïe 47.1 Ezéchiel 26.13-26.14 Esaïe 23.1-23.2 Jérémie 46.11
13 Tazama, nchi ya Wakaldayo; watu hao hawako tena; Mwashuri ameiweka tayari kwa hayawani wa jangwani; wamesimamisha buruji zao za vita, wameyaharibu majumba yake ya enzi, akaufanya kuwa uharibifu.
Esaïe 13.19 2 Chroniques 33.11 Esaïe 10.5 Genèse 2.14 Actes 7.4
14 Pigeni yowe, enyi merikebu za Tarshishi; maana ngome yenu imefanywa ukiwa.
Esaïe 23.1 Ezéchiel 27.25-27.30 Esaïe 2.16 Apocalypse 18.11-18.19 Esaïe 23.6
15 Basi, itakuwa katika siku ile, Tiro utasahauliwa miaka sabini, kadiri ya siku za mfalme mmoja; hata mwisho wa miaka sabini, Tiro utakuwa kama vile ulivyo wimbo wa kahaba.
Jérémie 25.22 Jérémie 25.9-25.11 Jérémie 29.10 Apocalypse 17.10 Jérémie 27.3-27.7
16 Twaa kinubi, tembea mjini, Ewe kahaba uliyesahauliwa; Piga vizuri, imba nyimbo nyingi, Upate kukumbukwa tena.
Proverbes 7.10-7.12 Jérémie 30.14
17 Hata itakuwa mwisho wa miaka sabini, Bwana ataizuru nchi ya Tiro, naye atarudi apate ujira wake, atafanya ukahaba pamoja na falme zote za ulimwengu juu ya uso wa dunia.
Nahum 3.4 Ezéchiel 27.6-27.36 Deutéronome 23.18 Michée 3.11 Apocalypse 19.2
18 Na biashara yake na ujira wake utakuwa wakfu kwa Bwana, hautawekwa hazinani wala hautawekwa akiba; bali mapato ya biashara yake yatakuwa mali zao wakaao mbele za Bwana, wapate kula na kushiba, na kuvaa mavazi ya fahari.
Psaumes 72.10 Matthieu 6.19-6.21 Actes 21.3-21.5 Matthieu 25.35-25.40 Actes 9.39

Cette Bible est dans le domaine public.