Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Cantique 1.5
Bible en Swahili de l’est


1 Wimbo ulio bora, wa Sulemani. 2 Kubusu na anibusu kwa kinywa chake. Maana pambaja zako zapita divai;Cantique 1.4 Cantique 4.10 Psaumes 63.3-63.5 Esaïe 55.1-55.2 Cantique 7.12
3 Manukato yako yanukia vizuri; Jina lako ni kama marhamu iliyomiminwa; Kwa hiyo wanawali hukupenda.Ecclésiaste 7.1 Jean 12.3 Psaumes 45.14 Cantique 4.10 Exode 30.23-30.28
4 Nivute nyuma yako, na tukimbie; Mfalme ameniingiza vyumbani mwake. Tutafurahi na kukushangilia; Tutazinena pambaja zako kuliko divai; Ndiyo, ina haki wakupende.Jean 6.44 Psaumes 45.14-45.15 Psaumes 119.32 Jean 12.32 Osée 11.4
5 Mimi ni mweusi-mweusi, lakini ninao uzuri, Enyi binti za Yerusalemu, Mfano wa hema za Kedari, Kama mapazia yake Sulemani.Cantique 5.8 Psaumes 120.5 Cantique 4.3 Cantique 2.7 Cantique 2.14
6 Msinichunguze kwa kuwa ni mweusi-mweusi, Kwa sababu jua limeniunguza. Wana wa mamangu walinikasirikia, Waliniweka niwe mlinzi wa mashamba ya mizabibu; Bali shamba langu mwenyewe sikulilinda.Psaumes 69.8 Cantique 8.11-8.12 Matthieu 10.35-10.36 Jérémie 8.21 Matthieu 10.25
7 Nijulishe, ee mpendwa wa nafsi yangu, Ni wapi utakapolisha kundi lako, Ni wapi utakapolilaza adhuhuri. Kwa nini niwe kama aliyefungiwa kidoto, Karibu na makundi ya wenzako?Cantique 3.1-3.4 Esaïe 13.20 Psaumes 23.1-23.2 Cantique 6.3 1 Jean 2.19
8 Usipojua, wewe uliye mzuri katika wanawake, Shika njia uzifuate nyayo za kondoo, Na kuwalisha wana-mbuzi wako Karibu na hema za wachungaji.Cantique 6.1 Cantique 5.9 Hébreux 13.7 Jacques 5.10 Psaumes 16.3
9 Mpenzi wangu, nimekulinganisha Na farasi katika magari ya Farao.Cantique 2.10 Cantique 2.13 Cantique 2.2 Cantique 4.7 Jean 15.14-15.15
10 Mashavu yako ni mazuri kwa mashada, Shingo yako kwa mikufu ya vito.Ezéchiel 16.11-16.13 1 Pierre 3.4 Cantique 5.13 Genèse 24.47 Cantique 4.9
11 Tutakufanyizia mashada ya dhahabu, Yenye vifungo vya fedha.Philippiens 3.21 Psaumes 149.4 Cantique 8.9 Genèse 1.26 Ephésiens 5.25-5.27
12 Muda mfalme alipoketi juu ya matakia, Nardo yangu ilitoa harufu yake.Jean 12.3 Marc 14.3 Cantique 4.13-4.16 Matthieu 26.26-26.28 Matthieu 22.4
13 Mpendwa wangu ni kama mfuko wa manemane Ukilazwa usiku maziwani mwangu.Jean 19.39 Psaumes 45.8 Cantique 5.13 Genèse 43.11 Cantique 4.6
14 Mpendwa wangu ni kama kishada cha hina, Katika mizabibu huko Engedi.Cantique 1.13 1 Samuel 23.29-24.1 Josué 15.62 Cantique 2.3 Cantique 4.13-4.14
15 Tazama, u mzuri, mpenzi wangu, U mzuri, macho yako ni kama ya hua.Cantique 4.1 Cantique 5.12 Cantique 4.7 Cantique 7.6 2 Corinthiens 11.2-11.3
16 Tazama, u mzuri, mpendwa wangu, Wapendeza, na kitanda chetu ni majani;Cantique 2.3 Apocalypse 5.11-5.13 Psaumes 110.3 Zacharie 9.17 Cantique 5.10-5.16
17 Nguzo za nyumba yetu ni mierezi, Na viguzo vyetu ni miberoshi.1 Timothée 3.15-3.16 Ezéchiel 42.3 Psaumes 92.12 Ezéchiel 41.16 Hébreux 11.10

Cette Bible est dans le domaine public.