Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Proverbes 24.14
Bible en Swahili de l’est


1 Usiwahusudu watu waovu, Wala usitamani kuwa pamoja nao;
Psaumes 37.1 Proverbes 23.17 Proverbes 3.31 Psaumes 73.3 Proverbes 24.19
2 Kwa maana moyo wao hufikiri dhuluma, Na midomo yao huongea madhara.
Psaumes 10.7 Psaumes 28.3 Psaumes 7.14 Job 15.35 Esaïe 59.4
3 Nyumba hujengwa kwa hekima, Na kwa ufahamu huthibitika,
Proverbes 14.1 Jérémie 10.12 Proverbes 9.1 Colossiens 2.7 1 Corinthiens 3.9
4 Na kwa maarifa vyumba vyake hujazwa Vitu vyote vya thamani na vya kupendeza.
Proverbes 21.20 Proverbes 15.6 Néhémie 10.39 Proverbes 20.15 Néhémie 13.5-13.13
5 Mtu mwenye hekima ana nguvu; Naam, mtu wa maarifa huongeza uwezo;
Proverbes 21.22 Colossiens 1.11 Ecclésiaste 7.19 Proverbes 8.14 Esaïe 40.31
6 Maana kwa mashauri ya akili utafanya vita; Na kwa wingi wa washauri huja wokovu.
Proverbes 11.14 Proverbes 20.18 Luc 14.31 Proverbes 15.22 Ephésiens 6.10-6.20
7 Kwa mpumbavu hekima haipatikani; Hafumbui kinywa chake langoni.
Proverbes 14.6 Psaumes 10.5 1 Corinthiens 2.14 Proverbes 17.24 Psaumes 92.5-92.6
8 Mtu afikiriye kutenda maovu, Watu watamwita mtundu;
Romains 1.30 Proverbes 6.14 Proverbes 14.22 Psaumes 21.11 Esaïe 32.7
9 Fikira za mpumbavu ni dhambi, Na mwenye mzaha huwachukiza watu.
Matthieu 15.19 Actes 8.22 Proverbes 29.8 2 Corinthiens 10.5 Genèse 6.5
10 Ukizimia siku ya taabu, Nguvu zako ni chache.
Esaïe 40.28-40.31 Job 4.5 Ephésiens 3.13 1 Samuel 27.1 Jérémie 51.46

Appel à la justice

11 Uwaokoe wanaochukuliwa ili wauawe; Nao walio tayari kuchinjwa uwaopoe.
Esaïe 58.6-58.7 Psaumes 82.4 Actes 23.10 Actes 18.17 1 Samuel 26.8-26.9
12 Ukisema, Sisi hatukujua hayo; Je! Yeye aipimaye mioyo siye afahamuye? Naye ailindaye nafsi yako siye ajuaye? Je! Hatamlipa kila mtu sawasawa na kazi yake?
Job 34.11 Ecclésiaste 5.8 1 Samuel 16.7 Apocalypse 2.23 Psaumes 121.8
13 Mwanangu, ule asali, kwa maana ni njema, Na sega la asali lililo tamu ulionjapo.
Cantique 5.1 Proverbes 25.16 Esaïe 7.15 Matthieu 3.4 Proverbes 25.27
14 Basi utaijua hekima kuwa tamu kwa nafsi yako; Ikiwa umekwisha kuiona; Ndipo itakapofuata thawabu; Wala tumaini lako halitabatilika.
Proverbes 23.18 Proverbes 2.10 Jacques 1.25 Psaumes 119.103 Proverbes 3.13-3.18
15 Ewe mtu mbaya, usiyavizie makao yake mwenye haki; Wala usipaharibu mahali pake pa kupumzika;
Psaumes 10.8-10.10 1 Samuel 9.11 Psaumes 56.6 Actes 25.3 Psaumes 140.5
16 Kwa maana mwenye haki huanguka mara saba akaondoka tena; Bali wasio haki hukwazwa na mabaya.
Psaumes 37.24 Michée 7.8-7.10 Job 5.19 Psaumes 34.19 2 Corinthiens 4.8-4.12
17 Usifurahi, adui yako aangukapo; Wala moyo wako usishangilie ajikwaapo;
Job 31.29 Proverbes 17.5 Abdias 1.12 1 Corinthiens 13.6-13.7 Psaumes 35.15
18 Bwana asije akaliona hilo, likamkasirisha; Akageuzia mbali naye hasira yake.
Zacharie 1.15-1.16 Lamentations 4.21-4.22
19 Usikasirike kwa sababu ya watenda mabaya; Wala usiwahusudu wabaya;
Psaumes 37.1 Proverbes 24.1 Proverbes 23.17 Psaumes 1.1 Proverbes 13.20
20 Kwa maana mtu mbaya hapati thawabu; Taa ya mtu mbaya itazimika.
Proverbes 13.9 Job 18.5-18.6 Proverbes 20.20 Job 21.17 Esaïe 3.11
21 Mwanangu, mche Bwana, na mfalme; Wala usishirikiane na wenye kigeugeu;
Romains 13.1-13.7 1 Pierre 2.13-2.17 Tite 3.1 1 Samuel 24.6 Matthieu 22.21
22 Maana msiba wao utatokea kwa ghafula; Tena ni nani aujuaye uharibifu wa miaka yao.
Nombres 16.31-16.35 Osée 5.11 Osée 13.10-13.11 Proverbes 16.14 2 Chroniques 13.16-13.17
23 Haya nayo pia ni maneno ya wenye akili. Kupendelea watu katika hukumu si kwema.
Proverbes 28.21 Proverbes 18.5 Lévitique 19.15 Proverbes 1.6 Psaumes 107.43
24 Amwambiaye mtu mwovu, Wewe una haki; Kabila za watu watamlaani, taifa watamchukia.
Proverbes 17.15 Proverbes 11.26 Esaïe 5.23 Esaïe 66.24 Exode 23.6-23.7
25 Bali kwao wakemeao furaha itakuwako; Na baraka ya kufanikiwa itawajilia.
Proverbes 28.23 Néhémie 13.17 1 Rois 21.19-21.20 1 Timothée 5.20 Tite 2.15
26 Aibusu midomo atoaye jawabu la haki.
Proverbes 25.11-25.12 Daniel 2.46-2.48 Genèse 41.38-41.57 Marc 12.32-12.34 Proverbes 15.23
27 Tengeneza kazi yako huko nje, Jifanyizie kazi yako tayari shambani, Ukiisha, jenga nyumba yako.
Luc 14.28-14.30 1 Rois 6.7 1 Rois 5.17-5.18
28 Usimshuhudie jirani yako pasipo sababu, Wala usidanganye kwa midomo yako.
Ephésiens 4.25 Proverbes 25.18 Psaumes 35.7 Exode 20.16 Proverbes 21.28
29 Usiseme, Nitamtenda kama alivyonitenda mimi; Nitamlipa mtu huyo sawasawa na tendo lake.
Proverbes 20.22 1 Thessaloniciens 5.15 Romains 12.17-12.21 2 Samuel 13.22-13.28 Juges 15.11
30 Nalipita karibu na shamba la mvivu, Na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili.
Job 15.17 Job 4.8 Job 5.27 Ecclésiaste 8.9-8.11 Ecclésiaste 4.1-4.8
31 Kumbe! Lote pia limemea miiba; Uso wake ulifunikwa kwa viwawi; Na ukuta wake wa mawe umebomoka.
Job 31.40 Proverbes 19.23 Ecclésiaste 10.18 Jérémie 4.3 Matthieu 13.22
32 Ndipo nilipoangalia na kufikiri sana; Naliona, nikapata mafundisho.
Job 7.17 Deutéronome 21.21 Deutéronome 32.29 Deutéronome 13.11 Jude 1.5-1.7
33 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, Bado kukunja mikono upate usingizi!
1 Thessaloniciens 5.6-5.8 Romains 13.11 Ephésiens 5.14 Proverbes 6.4-6.11
34 Hivyo, umaskini wako huja kama mnyang’anyi, Na uhitaji wako kama mtu mwenye silaha.
Proverbes 10.4 Proverbes 13.4

Cette Bible est dans le domaine public.