Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Exode 8.2
Bible en Swahili de l’est


1 Bwana akamwambia Musa, Ingia kwa Farao, ukamwambie, Bwana asema hivi, Wape watu wangu ruhusa, ili wapate kunitumikia.
Exode 3.18 Exode 3.12 Exode 5.1 Ezéchiel 2.6-2.7 Exode 7.16
2 Tena kama ukikataa kuwapa ruhusa, tazama, nitaipiga mipaka yako yote kwa kuleta vyura;
Exode 9.2 Exode 7.14 Apocalypse 16.13-16.14 Psaumes 78.45 Psaumes 105.30
3 na huo mto utafurika vyura, nao watakwea juu na kuingia ndani ya nyumba yako, na ndani ya chumba chako cha kulala, na juu ya kitanda chako, na ndani ya nyumba ya watumishi wako, na juu ya watu wako, na ndani ya meko yako, na ndani ya vyombo vyako vya kukandia unga.
Exode 12.34 Psaumes 105.30
4 Kisha hao vyura watakwea juu yako wewe, na juu ya watu wako, na juu ya watumishi wako wote.
Esaïe 19.22 Esaïe 19.11 Esaïe 23.9 Daniel 4.37 Actes 12.22-12.23
5 Bwana akamwambia Musa, Mwambie Haruni, Nyosha mkono wako na fimbo yako juu ya mito, juu ya vijito, na juu ya maziwa ya maji, ukawalete vyura waje juu ya nchi yote ya Misri.
Exode 7.19
6 Basi Haruni akaunyosha mkono wake juu ya maji yote ya Misri; na hao vyura wakakwea juu, wakaifunika nchi ya Misri.
Psaumes 78.45 Psaumes 105.30 Apocalypse 16.13 Lévitique 11.12
7 Waganga nao wakafanya mfano wa hayo kwa uganga wao; na kuwaleta vyura juu ya nchi ya Misri.
Exode 7.11 Exode 7.22 2 Thessaloniciens 2.9-2.11 Apocalypse 13.14 2 Timothée 3.8
8 Ndipo Farao akawaita Musa na Haruni na kuwaambia, Mwombeni Bwana, ili awaondoe vyura hawa kwangu mimi na kwa watu wangu; nami nitawapa watu ruhusa waende zao, ili wamtolee Bwana dhabihu.
Exode 10.17 Exode 9.28 1 Rois 13.6 Nombres 21.7 Exode 8.25-8.28
9 Musa akamwambia Farao, Haya, ujitukuze juu yangu katika jambo hili; sema ni lini unapotaka nikuombee wewe, na watumishi wako, na watu wako, ili hao vyura waangamizwe watoke kwako wewe na nyumba zako, wakae ndani ya mto tu.
1 Rois 18.25 Esaïe 10.15 Juges 7.2
10 Akamwambia, Kesho, Akasema, Na yawe kama neno lako; ili upate kujua ya kwamba hapana mwingine mfano wa Bwana, Mungu wetu.
2 Samuel 7.22 Psaumes 86.8 Esaïe 46.9 1 Chroniques 17.20 Exode 9.14
11 Hao vyura wataondoka kutoka kwako wewe na nyumba zako, na watumishi wako, na watu wako; watasalia mtoni tu.
Exode 8.9 Exode 8.3

Fléau n° 3 : les moustiques

12 Basi Musa na Haruni wakatoka kwa Farao; Musa akamlilia Bwana katika jambo la hao vyura aliokuwa amewaleta juu ya Farao.
Exode 8.8 Exode 32.11 Exode 8.30 Exode 9.33 Exode 10.18
13 Bwana akafanya sawasawa na neno la Musa; na hao vyura wakafa kutoka katika zile nyumba, na katika viwanja, na katika mashamba.
Deutéronome 34.10-34.12
14 Wakawakusanya chungu chungu; na nchi ikatoa uvundo.
Ezéchiel 39.11 Esaïe 34.2 Exode 7.21 Joël 2.20 Exode 8.24
15 Lakini Farao alipoona ya kuwa pana nafuu, akaufanya moyo wake kuwa mzito, asiwasikize; kama Bwana alivyonena.
Esaïe 26.10 Jérémie 34.7-34.11 Ecclésiaste 8.11 Exode 7.4 Exode 7.13-7.14

Fléau n° 4 : les mouches venimeuses

16 Bwana akamwambia Musa, Mwambie Haruni, Nyosha fimbo yako, ukayapige mavumbi ya nchi, ili kwamba yawe chawa katika nchi yote ya Misri.
Exode 8.17 Exode 8.5
17 Nao wakafanya; Haruni akaunyosha mkono wake na fimbo yake, na kuyapiga mavumbi ya nchi, nayo yakawa chawa juu ya wanadamu na juu ya wanyama; mavumbi yote ya nchi yakawa ni chawa katika nchi yote ya Misri.
Psaumes 105.31 Actes 12.23 Esaïe 23.9
18 Hao waganga nao wakafanya mfano wa hayo kwa uganga wao, ili kwamba walete chawa, lakini wasiweze; nako kulikuwa na chawa juu ya wanadamu, na juu ya wanyama.
Exode 7.11 Exode 9.11 Daniel 5.8 Esaïe 19.12 2 Timothée 3.8-3.9
19 Ndipo wale waganga wakamwambia Farao, Jambo hili ni chanda cha Mungu; na moyo wake Farao ukawa mgumu asiwasikize; vile vile kama Bwana alivyonena.
Psaumes 8.3 Luc 11.20 Actes 4.16 Daniel 2.10-2.11 1 Samuel 6.9
20 Bwana akamwambia Musa, Inuka asubuhi na mapema usimame mbele ya Farao; angalia! Atoka aende majini; kamwambie, Bwana asema, Wape watu wangu ruhusa waende zao, ili wanitumikie mimi.
Exode 7.15 Exode 9.13 Exode 8.1 Exode 3.18
21 Au kwamba huwapi ruhusa watu wangu, tazama, nitaleta wingi wa mainzi juu yako wewe, na juu ya watumishi wako, na juu ya watu wako, nao wataingia ndani ya nyumba zako; na nyumba za Wamisri zitajawa na wingi wa mainzi, na nchi nayo ambayo wa juu yake.
Esaïe 7.18 Psaumes 78.45 Psaumes 105.31
22 Nami siku hiyo nitatenga nchi ya Gosheni, watu wangu wanayokaa, ili hao mainzi wasiwe huko; ili kwamba upate kujua wewe ya kuwa mimi ndimi Bwana kati ya dunia.
Exode 9.4 Exode 10.23 Malachie 3.18 Exode 9.6 Exode 9.26
23 Nami nitatia mpaka kati ya watu wangu na watu wako; ishara hiyo italetwa kesho.
24 Bwana akafanya; wakaja wingi wa mainzi kwa uzito sana, wakaingia nyumbani mwa Farao, na katika nyumba za watumishi wake, tena katika nchi yote ya Misri; nayo nchi iliharibiwa kwa ajili ya wale mainzi.
Psaumes 105.31 Psaumes 78.45 Exode 8.21
25 Farao akawaita Musa na Haruni akawaambia, Endeni mkamtolee Mungu wenu dhabihu ndani ya nchi hii.
Exode 9.27 Exode 8.8 Exode 12.31 Exode 10.16 Apocalypse 3.9
26 Musa akasema, Haitupasi kufanya hivyo; kwa kuwa tutamchinjia sadaka Bwana, Mungu wetu, na hayo machukizo ya Wamisri; je! Tutachinja sadaka ya hayo machukizo ya Wamisri mbele ya macho yao, wasitupige kwa mawe?
Genèse 43.32 Genèse 46.34 Exode 3.18 Esaïe 44.19 Deutéronome 7.25-7.26
27 La, tutakwenda safari ya siku tatu jangwani, tumchinjie dhabihu Bwana, Mungu wetu, kama atakavyotuagiza.
Exode 3.18 Exode 3.12 Exode 34.11 Exode 5.1 Exode 10.26
28 Farao akasema, Mimi nitawapa ruhusa mwende, ili mmchinjie dhabihu Bwana, Mungu wenu, jangwani; lakini hamtakwenda mbali sana; haya niombeeni.
Exode 8.8 1 Rois 13.6 Exode 9.28 Exode 8.29 Osée 10.2
29 Musa akasema, Tazama, mimi natoka kwako, nami nitamwomba Bwana ili hao mainzi wamtoke Farao, na watumishi wake, na watu wake kesho; lakini Farao asitende kwa udanganyifu tena, kwa kutowaacha watu waende kumchinjia Bwana dhabihu.
Exode 8.15 Exode 8.8 Jérémie 42.20-42.21 Psaumes 66.3 Psaumes 78.34-78.37
30 Musa akatoka kwa Farao, akamwomba Bwana.
Exode 8.12 Jacques 5.16 Exode 9.33
31 Bwana akafanya kama neno la Musa, akawaondoa wale mainzi wabaya kwake Farao, na kwa watumishi wake, na watu wake; hakusalia hata mmoja.
32 Farao akaufanya moyo wake kuwa mzito mara hiyo nayo, wala hakuwapa ruhusa hao watu waende zao.
Exode 8.15 Exode 4.21 Romains 2.5 Exode 7.13-7.14 Jacques 1.13-1.14

Cette Bible est dans le domaine public.