Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Exode 32.8
Bible en Swahili de l’est


Renouvellement de l’alliance

Fabrication du veau d’or

1 Hata watu walipoona ya kuwa Musa amekawia kushuka katika mlima, wakakusanyana wakamwendea Haruni, wakamwambia, Haya! Katufanyizie miungu itakayokwenda mbele yetu, kwa maana Musa huyo aliyetutoa katika nchi ya Misri hatujui yaliyompata.
Actes 7.40 Exode 24.18 Deutéronome 9.9 2 Pierre 3.4 Exode 13.21
2 Haruni akawaambia, Zivunjeni pete za dhahabu zilizo katika masikio ya wake zenu, na wana wenu, na binti zenu, mkaniletee.
Juges 8.24-8.27 Exode 12.35-12.36 Ezéchiel 16.17 Osée 2.8 Ezéchiel 16.11-16.12
3 Watu wote wakazivunja pete za dhahabu zilizo katika masikio yao, wakamletea Haruni.
Juges 17.3-17.4 Jérémie 10.9 Esaïe 46.6 Esaïe 40.19-40.20
4 Akaipokea mikononi mwao akaitengeneza kwa patasi, akaifanya iwe sanamu ya ndama kwa kuiyeyusha; nao wakasema, Hiyo ndiyo miungu yako, Ee Israeli, iliyokutoa katika nchi ya Misri.
Néhémie 9.18 Actes 7.41 Deutéronome 9.16 Exode 32.8 Juges 17.3-17.4
5 Naye Haruni alipoona jambo hili, akajenga madhabahu mbele yake; Haruni akatangaza akasema, Kesho itakuwa sikukuu kwa Bwana.
2 Rois 10.20 Lévitique 23.37 Lévitique 23.2 1 Corinthiens 5.8 1 Rois 12.32-12.33
6 Wakaondoka asubuhi na mapema, wakatoa dhabihu, wakaleta sadaka za amani, watu wakaketi kula na kunywa, wakaondoka wacheze.
1 Corinthiens 10.7 Nombres 25.2 Juges 16.23-16.25 Actes 7.41-7.42 Exode 32.17-32.19
7 Bwana akamwambia Musa, Haya! Shuka; kwa maana watu wako uliowatoa katika nchi ya Misri wamejiharibu nafsi zao,
Deutéronome 9.12 Exode 32.11 Juges 2.19 Genèse 6.11-6.12 Osée 9.9
8 wamepotoka upesi kuiacha ile njia niliyowaamuru, wamejifanyizia ndama ya kuyeyusha wakaiabudu na kuitolea dhabihu, wakasema, Hiyo ndiyo miungu yako, Ee Israeli, iliyokutoa katika nchi ya Misri.
Exode 20.23 Exode 20.3-20.4 1 Rois 12.28 Deutéronome 9.16 Juges 2.17
9 Tena Bwana akamwambia Musa, Mimi nimewaona watu hawa, na tazama, ni watu wenye shingo ngumu
Deutéronome 9.13 Esaïe 48.4 Exode 34.9 Exode 33.5 Exode 33.3
10 basi sasa niache, ili hasira zangu ziwake juu yao, niwaangamize, nami nitakufanya wewe uwe taifa kuu.
Deutéronome 9.14 Nombres 14.12 Deutéronome 9.19 Exode 22.24 Nombres 16.45-16.48
11 Musa akamsihi sana Bwana, Mungu wake, na kusema, Bwana, kwa nini hasira zako kuwaka juu ya watu wako uliowaleta kutoka nchi ya Misri kwa uweza mkuu, na kwa mkono wenye nguvu?
Deutéronome 9.18-9.20 Psaumes 106.23 Psaumes 74.1-74.2 Deutéronome 9.26-9.29 Nombres 16.22
12 Kwa nini Wamisri kunena, wakisema, Amewatoa kwa kuwatenda uovu, ili apate kuwaua milimani, na kuwaondoa watoke juu ya uso wa nchi? Geuka katika hasira yako kali, ughairi uovu huu ulio nao juu ya watu wako.
Nombres 14.13-14.16 Deutéronome 9.28 Exode 32.14 Josué 7.9 Psaumes 74.18
13 Mkumbuke Ibrahimu, na Isaka, na Israeli, watumishi wako, ambao uliwaapia kwa nafsi yako, na kuwaambia, Nitazidisha kizazi chenu mfano wa nyota za mbinguni; tena nchi hii yote niliyoinena nitakipa kizazi chenu nao watairithi milele.
Genèse 22.16 Hébreux 6.13 Genèse 12.7 Genèse 15.18 Genèse 15.5
14 Na Bwana akaughairi ule uovu aliosema ya kwamba atawatenda watu wake.
Psaumes 106.45 2 Samuel 24.16 Jonas 3.10 Jérémie 26.13 Jonas 4.2
15 Basi, Musa akageuka akashuka katika mlima, na zile mbao mbili za mawe mikononi mwake; mbao zilizoandikwa pande zote mbili, upande huu na upande huu ziliandikwa.
Deutéronome 9.15 Deutéronome 5.22 Exode 31.18 Apocalypse 5.1 Exode 16.34
16 Na zile mbao zilikuwa kazi ya Mungu nayo maandiko yalikuwa maandiko ya Mungu, yaliyochorwa katika zile mbao.
Exode 31.18 2 Corinthiens 3.3 Exode 34.4 Deutéronome 9.9-9.11 Deutéronome 10.1
17 Na Yoshua aliposikia kelele za watu walipokuwa wakipiga kelele, akamwambia Musa, Kuna kelele ya vita maragoni.
Exode 24.13 Exode 17.9 1 Samuel 17.20 Esdras 3.11-3.13 1 Samuel 4.5-4.6
18 Akasema, Hiyo si sauti ya watu wapigao kelele kwa sababu ya kushinda vitani, wala si sauti ya watu wapigao kelele kwa sababu ya kushindwa; bali kelele za watu waimbao ndizo ninazozisikia mimi.
Daniel 5.23 Daniel 5.4 Exode 15.1-15.18
19 Hata alipoyakaribia marago akaiona ile ndama, na ile michezo. Hasira ya Musa ikawaka, akazitupa zile mbao mikononi mwake, akazivunja chini ya mlima.
Deutéronome 9.16-9.17 Zacharie 11.10-11.11 Lamentations 5.15 Marc 10.14 Jérémie 31.32
20 Akaitwaa ile ndama waliyoifanya, akaichoma moto, akaisaga hata ikawa mavumbi, akainyunyiza juu ya maji, akawanywesha wana wa Israeli.
Deutéronome 9.21 Proverbes 14.14 Deutéronome 7.25 2 Rois 23.15 Deutéronome 7.5
21 Musa akamwambia Haruni Watu hawa wamekufanyani hata ukaleta dhambi hii kuu juu yao?
Genèse 20.9 Genèse 26.10 1 Rois 21.22 2 Rois 21.9-21.11 Josué 7.19-7.26
22 Haruni akasema, Hasira ya bwana wangu isiwake, wewe unawajua watu hawa, ya kuwa wamejielekeza kwa mabaya.
Deutéronome 9.24 Exode 14.11 1 Samuel 15.24 Exode 16.20 Exode 15.24
23 Maana waliniambia, Katufanyie miungu, itakayokwenda mbele yetu, kwa maana mtu huyo Musa, aliyetutoa katika nchi ya Misri, hatujui yaliyompata.
Exode 32.1-32.4 Exode 32.8
24 Nikawaambia, Mtu ye yote aliye na dhahabu na aivunje; basi wakanipa, nami nikaitupa ndani ya moto, akatoka ndama huyu.
Exode 32.4 Luc 10.29 Genèse 3.12-3.13 Romains 3.10
25 Basi Musa alipoona ya kuwa watu hawa wameasi, maana Haruni amewaacha waasi, ili wawe dhihaka kati ya adui zao,
Daniel 12.2 Apocalypse 3.17-3.18 Apocalypse 16.15 2 Chroniques 28.19 Esaïe 47.3
26 ndipo Musa akasimama katika mlango wa marago, akasema, Mtu awaye yote aliye upande wa Bwana, na aje kwangu. Wana wa Lawi wote wakamkusanyikia
2 Samuel 20.11 Josué 5.13 2 Rois 9.32 Matthieu 12.30
27 Akawaambia, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Kila mtu na ajifunge upanga wake pajani mwake, akapite huko na huko toka mlango hata mlango kati ya marago, mkamchinje kila mtu ndugu yake, na kila mtu mwenziwe na kila mtu jirani yake.
Nombres 25.5 2 Corinthiens 5.16 Deutéronome 33.8-33.9 Luc 14.26 Exode 32.29
28 Na hao wana wa Lawi wakafanya kama vile alivyosema Musa, wakaanguka siku ile kama watu elfu tatu.
Deutéronome 33.9 Nombres 16.32-16.35 Hébreux 2.2-2.3 1 Corinthiens 10.8 Malachie 2.4-2.6
29 Musa akasema, Jiwekeni wakfu kwa Bwana leo, naam, kila mtu juu ya mwanawe na juu ya ndugu yake; ili awape baraka leo.
Zacharie 13.3 Matthieu 10.37 Nombres 25.11-25.13 Joël 2.12-2.14 1 Samuel 15.18-15.22

Intercession de Moïse

30 Hata asubuhi yake Musa akawaambia watu, Mmetenda dhambi kuu; na sasa nitakwenda juu kwa Bwana, labda nitafanya upatanisho kwa ajili ya dhambi yenu.
1 Samuel 12.20 Nombres 25.13 2 Samuel 16.12 Amos 5.15 1 Samuel 12.23
31 Musa akarejea kwa Bwana akasema, Aa! Watu hawa wametenda dhambi kuu wamejifanyia miungu ya dhahabu.
Exode 20.23 Exode 32.30 Daniel 9.5 Exode 34.28 Daniel 9.8
32 Walakini sasa, ikiwa utawasamehe dhambi yao -- na kama sivyo, unifute, nakusihi, katika kitabu chako ulichoandika.
Psaumes 69.28 Apocalypse 21.27 Philippiens 4.3 Daniel 12.1 Romains 9.3
33 Bwana akamwambia Musa, Mtu ye yote aliyenitenda dhambi ndiye nitakayemfuta katika kitabu changu.
Ezéchiel 18.4 Psaumes 69.28 Lévitique 23.30 Psaumes 109.13-109.14 Apocalypse 20.12
34 Basi sasa uende ukawaongoze watu hawa mpaka mahali pale ambapo nimekwambia habari zake; tazama, malaika wangu atakutangulia; pamoja na hayo siku nitakayowajilia nitawapatiliza kwa ajili ya dhambi yao.
Exode 23.20 Deutéronome 32.35 Nombres 20.16 Psaumes 99.8 Nombres 14.27-14.30
35 Bwana akawapiga hao watu, kwa walivyoifanya ile ndama, ambayo Haruni aliifanya.
2 Samuel 12.9-12.10 Matthieu 27.3-27.7 Actes 7.41 Exode 32.25 Exode 32.4

Cette Bible est dans le domaine public.