Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Exode 20.16
Bible en Swahili de l’est


Les dix commandements

1 Mungu akanena maneno haya yote akasema,
Deutéronome 4.36 Deutéronome 5.22 Deutéronome 5.4 Actes 7.38 Deutéronome 4.33
2 Mimi ni Bwana, Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa.
Osée 13.4 Psaumes 81.10 Exode 13.3 Lévitique 19.36 Deutéronome 5.6
3 Usiwe na miungu mingine ila mimi.
Deutéronome 5.7 Deutéronome 6.14 Deutéronome 6.5 Psaumes 81.9 Jérémie 25.6
4 Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.
Lévitique 26.1 Deutéronome 4.15-4.19 Psaumes 97.7 Deutéronome 27.15 Lévitique 19.4
5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
Nombres 14.18 Exode 34.14 Nahum 1.2 Jérémie 32.18 Deutéronome 4.24
6 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu.
Deutéronome 7.9 Jérémie 32.39-32.40 Actes 2.39 Deutéronome 5.29 1 Jean 5.3
7 Usilitaje bure jina la Bwana, Mungu wako, maana Bwana hatamhesabia kuwa hana hatia mtu alitajaye jina lake bure.
Lévitique 19.12 Jacques 5.12 Lévitique 24.11-24.16 Psaumes 50.14-50.16 Hébreux 6.16-6.17
8 Ikumbuke siku ya Sabato uitakase.
Lévitique 19.3 Lévitique 26.2 Exode 31.13-31.16 Lévitique 19.30 Genèse 2.3
9 Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote;
Luc 13.14 Exode 34.21 Exode 23.12 Lévitique 23.3 Exode 35.2
10 lakini siku ya saba ni Sabato ya Bwana, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako.
Nombres 15.32-15.36 Exode 34.21 Deutéronome 5.14-5.15 Exode 16.27-16.28 Néhémie 13.15-13.21
11 Maana, kwa siku sita Bwana alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba; kwa hiyo Bwana akaibarikia siku ya Sabato akaitakasa.
Genèse 2.2-2.3 Exode 31.17 Genèse 1.1-1.2 Marc 2.27-2.28 Actes 20.7
12 Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na Bwana, Mungu wako.
Colossiens 3.20 Marc 7.10 Ephésiens 6.1-6.3 Lévitique 19.3 Exode 21.15
13 Usiue.
Romains 13.9 Genèse 9.5-9.6 Matthieu 5.21-5.22 Matthieu 19.18 Deutéronome 19.11-19.13
14 Usizini.
Lévitique 20.10 Lévitique 18.20 Hébreux 13.4 Jérémie 5.8-5.9 Apocalypse 21.8
15 Usiibe.
Ephésiens 4.28 Lévitique 19.11 Matthieu 19.18 Lévitique 19.13 Romains 13.9
16 Usimshuhudie jirani yako uongo.
Matthieu 19.18 Proverbes 19.5 Psaumes 15.3 Exode 23.1 Matthieu 26.59-26.60
17 Usiitamani nyumba ya jirani yako, usimtamani mke wa jirani yako; wala mtumwa wake, wala mjakazi wake, wala ng’ombe wake, wala punda wake, wala cho chote alicho nacho jirani yako.
Romains 13.9 Luc 12.15 Romains 7.7 Ephésiens 5.3 Matthieu 5.28
18 Watu wote wakaona umeme na ngurumo na sauti ya baragumu, na ule mlima kutoka moshi; na watu walipoona hayo wakatetemeka, wakasimama mbali.
Exode 19.16-19.18 Hébreux 12.18-12.19 Psaumes 139.7-139.8 Jérémie 23.23
19 Wakamwambia Musa, Sema nasi wewe, nasi tutasikia, bali Mungu asiseme nasi, tusije tukafa.
Deutéronome 18.16 Galates 3.19 Exode 33.20 Deutéronome 5.5 Genèse 32.30
20 Musa akawaambia watu, Msiogope, maana Mungu amekuja ili awajaribu, na utisho wake uwe mbele yenu, ili kwamba msifanye dhambi.
Deutéronome 13.3 Esaïe 8.13 Esaïe 41.10 Proverbes 3.7 1 Samuel 12.20
21 Basi hao watu wakasimama mbali, naye Musa akalikaribia lile giza kuu Mungu alipokuwapo.
1 Rois 8.12 Psaumes 97.2 Psaumes 18.9 Exode 19.16-19.17 Deutéronome 5.5
22 Bwana akamwambia Musa, Waambie wana wa Israeli hivi, Ninyi wenyewe mmeona ya kuwa nimenena nanyi kutoka mbinguni.
Néhémie 9.13 Deutéronome 4.36 Hébreux 12.25-12.26
23 Msifanye miungu mingine pamoja nami; miungu ya fedha, wala miungu ya dhahabu, msijifanyie.
Exode 20.3-20.5 Ezéchiel 20.39 Sophonie 1.5 2 Rois 17.33 1 Samuel 5.4-5.5
24 Utanifanyia madhabahu ya udongo, nawe utatoa dhabihu zako juu yake; sadaka za kuteketezwa, na sadaka za amani, kondoo zako, na ng’ombe zako, kila mahali nitakapotia ukumbusho wa jina langu, hapo ndipo nitakapokujilia na kukubarikia.
Deutéronome 12.5 2 Chroniques 6.6 Deutéronome 16.11 Deutéronome 26.2 1 Rois 8.29
25 Nawe ukinifanyia madhabahu ya mawe, hutaijenga ya mawe yaliyochongwa; kwa kuwa ukiwa wewe umetumia chombo chako katika kuichonga umeitia unajisi.
Josué 8.31 Deutéronome 27.5-27.6
26 Tena hutapanda kwenda madhabahuni kwangu kwa daraja, uchi wako usidhihirike juu yake.
1 Pierre 1.16 Lévitique 10.3 Psaumes 89.7 Hébreux 12.28-12.29 Ecclésiaste 5.1

Cette Bible est dans le domaine public.