Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Exode 2.15
Bible en Swahili de l’est


Naissance et fuite de Moïse

1 Mtu mmoja wa nyumba ya Lawi akaondoka akaoa binti mmoja wa Lawi.
Nombres 26.59 1 Chroniques 6.1-6.3 Exode 6.16-6.20 1 Chroniques 23.12-23.14
2 Yule mwanamke akachukua mimba akazaa mwana, na alipoona ya kuwa ni mtoto mzuri akamficha miezi mitatu.
Actes 7.20 Hébreux 11.23 Psaumes 112.5
3 Na alipokuwa hawezi kumficha tena, akampatia kisafina cha manyasi akakipaka sifa na lami, akamtia mtoto ndani yake, akakiweka katika majani kando ya mto.
Esaïe 18.2 Esaïe 19.6 Genèse 11.3 Genèse 6.14 Matthieu 2.16
4 Umbu lake mtoto akasimama mbali ili ajue yatakayompata.
Exode 15.20 Nombres 26.59 Nombres 20.1 Nombres 12.1-12.15 Michée 6.4
5 Basi binti Farao akashuka, aoge mtoni, na vijakazi wake wakatembea kando ya mto; naye akakiona kile kisafina katika majani, akamtuma kijakazi wake kwenda kukileta.
Actes 7.21 Psaumes 12.5 Exode 7.15 Exode 8.20 Psaumes 9.9
6 Akakifungua, akamwona mtoto, na tazama, mtoto yule analia. Basi akamhurumia, akasema, Huyu ni mmojawapo wa watoto wa Waebrania.
1 Pierre 3.8 Actes 7.21 Néhémie 1.11 Proverbes 21.1 1 Rois 8.50
7 Basi umbu lake mtoto akamwambia binti Farao, Je! Niende nikamwite mlezi katika wanawake wa Kiebrania, aje kwako, akunyonyeshee mtoto huyu?
Nombres 12.1 Exode 15.20 Nombres 26.59 Exode 2.4
8 Binti Farao akamwambia, Haya! Enenda. Yule kijana akaenda akamwita mama yake yule mtoto.
Exode 6.20 Psaumes 27.10 Esaïe 46.3-46.4 Ezéchiel 16.8
9 Binti Farao akamwambia, Mchukue mtoto huyu, ukaninyonyeshee, nami nitakupa mshahara wako. Yule mwanamke akamtwaa mtoto, akamnyonyesha.
10 Mtoto akakua, naye akamleta kwa binti Farao, akawa mwanawe. Akamwita jina lake Musa, akasema, Ni kwa sababu nalimtoa majini.
1 Jean 3.1 Galates 4.5 Hébreux 11.24 Matthieu 1.21 1 Samuel 1.20
11 Hata siku zile, Musa alipokuwa mtu mzima, akatoka kuwaendea ndugu zake, akatazama mizigo yao. Akamwona Mmisri anampiga Mwebrania, mmojawapo wa ndugu zake.
Hébreux 11.24-11.26 Exode 1.11 Matthieu 11.28 Exode 5.14 Exode 5.9
12 Basi akatazama huko na huko, na alipoona ya kuwa hapana mtu, akampiga Mmisri yule, akamficha ndani ya mchanga.
Actes 7.24-7.26
13 Akatoka siku ya pili, na tazama, watu wawili wa Waebrania walikuwa wakipigana. Akamwambia yule aliyemdhulumu mwenzake, Mbona unampiga mwenzako?
1 Corinthiens 6.7-6.8 Actes 7.26-7.28
14 Yule akasema, Ni nani aliyekuweka wewe kuwa mkuu wetu, na mwamuzi juu yetu? Je! Wataka kuniua mimi kama ulivyomwua yule Mmisri? Musa akaogopa, akasema, Kumbe! Jambo lile limejulikana.
Luc 12.14 Genèse 19.9 Matthieu 21.23 Luc 19.14 Nombres 16.13
15 Basi Farao alipopata habari, akataka kumwua Musa; lakini Musa akakimbia mbele ya Farao, akakaa katika nchi ya Midiani; akaketi karibu na kisima.
Actes 7.29 Hébreux 11.27 Genèse 24.11 Genèse 29.2 Proverbes 22.3
16 Basi kuhani wa Midiani alikuwa na binti saba, nao wakaja wakateka maji, wakazijaza birika maji, wapate kunywesha kundi la baba yao.
Exode 3.1 Genèse 24.11 1 Samuel 9.11 Genèse 24.14-24.20 Genèse 41.45
17 Wachungaji wakaja wakawafukuza; lakini Musa akasimama, akawasaidia, akalinywesha kundi lao.
Genèse 29.10 Genèse 21.25 Exode 2.12 Genèse 26.15-26.22
18 Walipofika kwa Reueli baba yao, akasema, Imekuwaje hata mkarejea mapema leo?
Exode 3.1 Nombres 10.29 Exode 4.18 Nombres 19.20 Exode 18.1-18.12
19 Wakasema, Mmisri mmoja alituokoa katika mikono ya wachungaji, tena zaidi ya hayo, akatutekea maji, akalinywesha kundi.
Genèse 29.10 Genèse 50.11
20 Akawaambia binti zake, Yuko wapi basi? Mbona mmemwacha mtu huyo? Mwiteni, ale chakula.
Genèse 31.54 Genèse 43.25 Genèse 24.31-24.33 Genèse 18.5 Job 31.32
21 Musa akawa radhi kukaa kwake mtu yule, naye akampa Musa binti yake, Sipora.
1 Timothée 6.6 Jacques 1.10 Nombres 12.1 Exode 2.10 Hébreux 13.5
22 Huyo akamzalia mwana, akamwita jina lake Gershomu, maana alisema, Nimekuwa mgeni katika nchi ya ugeni.
Hébreux 11.13-11.14 Actes 7.29 Exode 22.21 1 Chroniques 29.15 1 Chroniques 16.20

Appel de Moïse

23 Hata baada ya siku zile nyingi mfalme wa Misri akafa; wana wa Israeli wakaugua kwa sababu ya ule utumwa, wakalia; kilio chao kikafika juu kwa Mungu kwa sababu ya ule utumwa.
Jacques 5.4 Actes 7.30 Genèse 18.20-18.21 Actes 12.23-12.24 Deutéronome 26.6-26.7
24 Mungu akasikia kuugua kwao, Mungu akakumbuka agano lake alilolifanya na Ibrahimu na Isaka na Yakobo.
Psaumes 105.42 Exode 6.5 Genèse 26.3 Psaumes 106.45 Psaumes 102.20
25 Mungu akawaona wana wa Israeli, na Mungu akawaangalia.
Exode 4.31 Exode 3.7-3.8 Luc 1.25 2 Samuel 16.12 1 Samuel 1.11

Cette Bible est dans le domaine public.