Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Exode 17.15
Bible en Swahili de l’est


L’eau jaillie du rocher à Horeb

1 Mkutano wote wa wana wa Israeli ukasafiri, kutoka bara ya Sini kwa safari zao, kama Bwana alivyowaagiza, wakatua Refidimu; napo hapakuwa na maji, watu wanywe.
Exode 19.2 Exode 16.1 Exode 17.8 Nombres 33.12-33.14
2 Kwa hiyo hao watu wakateta na Musa, wakasema, Tupe maji tunywe. Musa akawaambia, Kwani kuteta na mimi? Mbona mnamjaribu Bwana?
Psaumes 78.41 Deutéronome 6.16 Psaumes 78.18 Matthieu 4.7 1 Corinthiens 10.9
3 Watu wakawa na kiu huko; nao wakamnung’unikia Musa, wakasema, Mbona umetupandisha kutoka Misri, kutuua sisi na watoto wetu na wanyama wetu kwa kiu?
Exode 16.2-16.3 Exode 15.24
4 Musa akamlilia Bwana, akisema, Niwatendee nini watu hawa? Bado kidogo nao watanipiga kwa mawe.
Nombres 14.10 1 Samuel 30.6 Actes 14.19 Jean 10.31 Jean 8.59
5 Bwana akamwambia Musa, Pita mbele ya watu, ukawachukue baadhi ya wazee wa Israeli pamoja nawe; na ile fimbo yako ambayo uliupiga mto kwayo, uitwae mkononi mwako, ukaende.
Nombres 20.8-20.11 Ezéchiel 2.6 Actes 20.23-20.24 Exode 7.19-7.20
6 Tazama, nitasimama mbele yako huko, juu ya lile jabali katika Horebu; nawe utalipiga jabali, na maji yatatoka, watu wapate kunywa. Musa akafanya hivyo mbele ya wazee wa Israeli.
1 Corinthiens 10.4 Psaumes 114.8 Psaumes 105.41 Deutéronome 8.15 Nombres 20.9-20.11
7 Akapaita mahali pale jina lake Masa, na Meriba; kwa sababu ya mateto ya wana wa Israeli, na kwa sababu walimjaribu Bwana, wakisema, Je! Bwana yu kati yetu au sivyo?
Psaumes 81.7 Psaumes 95.8 Nombres 20.13 Deutéronome 9.22 Hébreux 3.8-3.9

Victoire sur les Amalécites

8 Wakati huo Waamaleki wakatokea, wakapigana na Israeli huko Refidimu.
1 Samuel 15.2 1 Samuel 30.1 Genèse 36.12 Nombres 24.20 Deutéronome 25.17-25.19
9 Musa akamwambia Yoshua, Tuchagulie watu, ukatoke upigane na Waamaleki; kesho nitasimama juu ya kilele kile, na ile fimbo ya Mungu nitakuwa nayo mkononi mwangu.
Exode 24.13 Exode 4.20 Exode 4.2 Deutéronome 32.44 Nombres 11.28
10 Basi Yoshua akafanya kama Musa alivyomwambia, akapigana na Amaleki; na Musa na Haruni na Huri wakapanda juu ya kile kilima.
Exode 24.14 Jean 15.14 Exode 31.2 Matthieu 28.20 Jean 2.5
11 Ikawa, Musa alipouinua mkono wake, Israeli walishinda; na alipoushusha mkono wake, Amaleki walishinda.
1 Timothée 2.8 Jacques 5.16 Luc 18.1 Psaumes 56.9
12 Lakini mikono ya Musa ilikuwa mizito; basi wakatwaa jiwe, wakaliweka chini yake akalikalia. Haruni na Huri wakaitegemeza mikono yake, mmoja upande huu na mmoja upande huu; mikono yake ikathibitika hata jua lilipokuchwa.
Esaïe 35.3 1 Thessaloniciens 5.25 2 Corinthiens 1.11 Philippiens 1.19 Colossiens 4.2
13 Yoshua akawaangamiza Amaleki na watu wake kwa ukali wa upanga.
Josué 11.12 Josué 10.28 Josué 10.37 Josué 10.32 Josué 10.42
14 Bwana akamwambia Musa, Andika habari hii katika kitabu iwe ukumbusho, kisha ihubiri masikioni mwa Yoshua; ya kuwa nitaufuta ukumbusho wa Amaleki kabisa, usiwe tena chini ya mbingu.
1 Samuel 30.17 Exode 34.27 Nombres 24.20 2 Samuel 8.12 1 Samuel 30.1
15 Musa akajenga madhabahu, akaiita jina lake Yehova-nisi;
Genèse 22.14 Psaumes 60.4 Juges 6.24 Genèse 33.20
16 akasema, Bwana ameapa; Bwana atakuwa na vita na Amaleki kizazi baada ya kizazi.
Psaumes 21.8-21.11 Actes 7.49 Esaïe 66.1

Cette Bible est dans le domaine public.