Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Exode 13.2
Bible en Swahili de l’est


Consécration des premiers-nés à l’Éternel

1 Bwana akasema na Musa, akamwambia,
2 Nitakasie mimi wazaliwa wa kwanza wote, kila afunguaye tumbo katika wana wa Israeli, wa binadamu na wa mnyama; ni wangu huyo.
Luc 2.23 Deutéronome 15.19 Nombres 3.13 Lévitique 27.26 Nombres 18.15
3 Musa akawaambia hao watu, Kumbukeni siku hii, mliyotoka nchi ya Misri, kutoka nyumba ya utumwa; kwa kuwa Bwana aliwatoa mahali hapa kwa nguvu za mkono wake; na usiliwe mkate uliochachwa.
Deutéronome 16.3 Exode 6.1 Exode 12.8 Exode 12.42 Exode 20.8
4 Ninyi mwatoka leo katika mwezi wa Abibu.
Exode 23.15 Exode 34.18 Exode 12.2 Deutéronome 16.1-16.3
5 Itakuwa hapo Bwana atakapowaleta mpaka nchi ya Wakanaani, na Wahiti, na Waamori, na Wahivi, na Wayebusi, nchi hiyo aliyowaapia baba zako kwamba atakupa wewe, ni nchi imiminikayo maziwa na asali, ndipo mtakapoushika utumishi huu katika mwezi huu.
Exode 3.8 Exode 6.8 Josué 24.11 Exode 12.25-12.26 Exode 34.11
6 Mtakula mikate isiyochachwa muda wa siku saba, nayo siku ya saba itakuwa ni sikukuu ya Bwana.
Exode 12.15-12.20 Exode 34.18 Lévitique 23.8
7 Mikate isiyochachwa italiwa katika hizo siku saba; mkate uliotiwa chachu usionekane kwako, wala chachu isionekane kwako, ndani ya mipaka yako yote.
Exode 12.19 Matthieu 16.6
8 Nawe utamwambia mwanao siku hiyo, ukisema, Ni kwa sababu ya hayo Bwana aliyonifanyia hapo nilipotoka Misri.
Exode 13.14 Psaumes 44.1 Psaumes 78.3-78.8 Esaïe 38.19 Exode 12.26-12.27
9 Nayo itakuwa ishara kwako katika mkono wako, na kwa ukumbusho kati ya macho yako, ili kwamba sheria ya Bwana ipate kuwa kinywani mwako; kwani Bwana alikutoa utoke Misri kwa mkono wenye uwezo.
Deutéronome 6.8 Exode 13.16 Exode 12.14 Nombres 15.39 Matthieu 23.5
10 Kwa hiyo utaitunza amri hii kwa wakati wake mwaka baada ya mwaka.
Exode 12.14 Exode 12.24-12.25 Deutéronome 16.3-16.4 Exode 23.15 Lévitique 23.6
11 Itakuwa hapo Bwana atakapokuleta katika nchi ya Wakanaani, kama alivyokuapia wewe na baba zako, na kukupa,
Exode 13.5
12 ndipo utamwekea Bwana kila afunguaye tumbo, na kila mzaliwa wa kwanza uliye naye, azaliwaye na mnyama; hao waume watakuwa ni wa Bwana.
Nombres 18.15 Lévitique 27.26 Exode 34.19 Exode 13.2 Deutéronome 15.19
13 Kila mzaliwa wa kwanza wa punda utamkomboa kwa mwana-kondoo; na kwamba hutaki kumkomboa, utamvunja shingo; na kila mzaliwa wa kwanza wa binadamu katika wanao utamkomboa.
Exode 34.20 Nombres 18.15-18.17 Nombres 3.46-3.51 Apocalypse 14.4 Exode 12.21
14 Kisha itakuwa hapo mwanao atakapokuuliza keshoni, akisema, Ni nini hivi? Utamwambia, Bwana alimtoa Misri, kutoka ile nyumba ya utumwa, kwa uwezo wa mkono wake;
Exode 13.3 Josué 4.6 Deutéronome 6.20-6.24 Exode 12.26-12.27 Exode 10.2
15 basi ilikuwa hapo Farao alipojifanya kuwa mgumu ili asitupe ruhusa kuondoka, Bwana akawapiga wazaliwa wa kwanza wote waliokuwa katika nchi ya Misri, wa binadamu na wa mnyama; kwa ajili ya hayo namtolea Bwana wote wafunguao tumbo, wakiwa waume; lakini wazaliwa wa kwanza wote wa wana wangu nawakomboa.
Exode 12.29
16 Jambo hilo litakuwa ni ishara mkononi mwako, na utepe katikati ya macho yako; kwa kuwa Bwana alitutoa Misri kwa uwezo wa mkono wake.
Exode 13.9 Exode 13.14 Matthieu 23.5 Deutéronome 11.18 Deutéronome 26.8

Passage de la mer des Roseaux

17 Ilikuwa hapo Farao alipokwisha kuwaacha watu hao waende zao, Mungu hakuwaongoza kwa njia ya nchi ya Wafilisti, ijapokuwa ilikuwa ni ya karibu; maana Mungu alisema, Wasije wakaghairi watu hawa hapo watakapokutana na vita, na kurudi Misri;
Nombres 14.1-14.4 Exode 14.11-14.12 Deutéronome 17.16 Néhémie 9.17 Actes 15.38
18 lakini Mungu akawazungusha hao watu kwa njia ya bara kando ya Bahari ya Shamu; wana wa Israeli wakakwea kutoka nchi ya Misri hali wamevaa silaha.
Deutéronome 32.10 Nombres 33.6-33.8 Exode 14.2 Josué 1.14 Exode 12.51
19 Musa akaichukua ile mifupa ya Yusufu pamoja naye; maana, alikuwa amewaapisha sana wana wa Israeli, akisema, Mungu hana budi atawajilia ninyi; nanyi mtaichukua mfupa yangu kutoka hapa pamoja nanyi.
Josué 24.32 Actes 7.16 Genèse 50.24-50.25 Luc 7.16 Luc 1.58
20 Nao wakasafiri kutoka Sukothi, wakapiga kambi Ethamu, kwenye mpaka wa ile jangwa.
Exode 12.37 Nombres 33.5-33.6
21 Bwana naye akawatangulia mchana ndani ya wingu mfano wa nguzo, ili awaongoze njia; na usiku, ndani ya moto mfano wa nguzo, ili kuwapa nuru; wapate kusafiri mchana na usiku;
Néhémie 9.12 Psaumes 105.39 Deutéronome 1.33 Nombres 9.15-9.23 Psaumes 99.7
22 ile nguzo ya wingu haikuondoka mchana, wala ile nguzo ya moto haikuondoka usiku, mbele ya hao watu.
Apocalypse 10.1 Psaumes 121.5-121.8

Cette Bible est dans le domaine public.