Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 56.8
Bible en Swahili de l’est


Confiance dans la détresse

1 Mungu, unirehemu, maana yuko atakaye kunimeza, Mchana kutwa ananionea akileta vita.
Psaumes 69.13-69.16 Psaumes 57.1-57.3 Psaumes 16.1 Psaumes 27.2 Psaumes 136.10
2 Adui zangu wanataka kunimeza mchana kutwa, Maana waletao vita juu yangu kwa kiburi ni wengi.
Psaumes 93.4 Psaumes 92.1 Psaumes 54.5 Psaumes 9.2 Psaumes 3.1
3 Siku ya hofu yangu nitakutumaini Wewe;
Psaumes 34.4 Psaumes 55.4-55.5 1 Samuel 30.6 Psaumes 11.1 1 Samuel 21.10
4 Kwa msaada wa MUNGU nitalisifu neno lake. Nimemtumaini Mungu, sitaogopa; Mwenye mwili atanitenda nini?
Psaumes 118.6 Hébreux 13.6 Psaumes 56.10-56.11 Psaumes 119.160 Psaumes 27.1
5 Mchana kutwa wanapotosha maneno yangu, Mawazo yao yote ni juu yangu kunitakia mabaya.
2 Pierre 3.16 1 Samuel 18.29 Esaïe 29.20-29.21 1 Samuel 20.7 Matthieu 22.15
6 Hukutanika, hujificha, huziangalia nyayo zangu, Kwa kuwa wameniotea nafsi yangu.
Psaumes 59.3 Psaumes 71.10 Psaumes 140.2 Actes 23.12-23.14 Esaïe 54.15
7 Je! Wataokoka kwa uovu wao? Ee Mungu, uwaangamize kwa hasira yako.
Psaumes 55.23 Jérémie 18.19-18.23 Psaumes 55.15 Psaumes 94.20-94.21 Jérémie 7.10
8 Umehesabu kutanga-tanga kwangu; Uyatie machozi yangu katika chupa yako; (Je! Hayamo katika kitabu chako?)
Psaumes 39.12 2 Rois 20.5 Malachie 3.16 Matthieu 10.30 Psaumes 139.16
9 Ndipo adui zangu watarudi nyuma siku ile niitapo. Neno hili najua kuwa MUNGU yu upande wangu;
Romains 8.31 Psaumes 118.6 Psaumes 102.2 Psaumes 18.38-18.42 Exode 17.9-17.11
10 Kwa msaada wa MUNGU nitalisifu neno lake. Kwa msaada wa Bwana nitalisifu neno lake.
Matthieu 24.35 Psaumes 60.6 Psaumes 56.4 Genèse 32.11 Hébreux 6.18
11 Nimemtumaini Mungu, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?
Esaïe 51.12-51.13 Psaumes 112.7-112.8 Esaïe 51.7-51.8 Psaumes 27.1
12 Ee Mungu, nadhiri zako zi juu yangu; Nitakutolea dhabihu za kushukuru.
Psaumes 9.1-9.3 Psaumes 50.14 1 Samuel 1.24-1.28 Esaïe 12.1 Psaumes 116.14-116.19
13 Maana umeniponya nafsi yangu na mauti; Je! Hukuizuia miguu yangu isianguke? Ili nienende mbele za Mungu Katika nuru ya walio hai.
Job 33.30 Psaumes 116.8-116.9 Psaumes 145.14 Ephésiens 5.8-5.14 Esaïe 2.5

Cette Bible est dans le domaine public.