Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 56.2
Bible en Swahili de l’est


Confiance dans la détresse

1 Mungu, unirehemu, maana yuko atakaye kunimeza, Mchana kutwa ananionea akileta vita.
Psaumes 16.1 Psaumes 27.2 Psaumes 69.13-69.16 Psaumes 57.1-57.3 Lamentations 2.5
2 Adui zangu wanataka kunimeza mchana kutwa, Maana waletao vita juu yangu kwa kiburi ni wengi.
Psaumes 118.10-118.12 Daniel 5.18 Esaïe 57.15 Michée 6.6 Psaumes 92.8
3 Siku ya hofu yangu nitakutumaini Wewe;
Psaumes 55.4-55.5 Psaumes 34.4 1 Samuel 30.6 1 Samuel 21.12 2 Corinthiens 7.5-7.6
4 Kwa msaada wa MUNGU nitalisifu neno lake. Nimemtumaini Mungu, sitaogopa; Mwenye mwili atanitenda nini?
Psaumes 118.6 Hébreux 13.6 Psaumes 56.10-56.11 Psaumes 119.160 Psaumes 27.1
5 Mchana kutwa wanapotosha maneno yangu, Mawazo yao yote ni juu yangu kunitakia mabaya.
2 Pierre 3.16 1 Samuel 18.17 Luc 22.3-22.6 Luc 11.54 Jean 2.19
6 Hukutanika, hujificha, huziangalia nyayo zangu, Kwa kuwa wameniotea nafsi yangu.
Psaumes 59.3 Psaumes 71.10 Psaumes 140.2 Matthieu 26.57 Psaumes 10.8-10.10
7 Je! Wataokoka kwa uovu wao? Ee Mungu, uwaangamize kwa hasira yako.
Psaumes 55.23 Psaumes 55.9 Psaumes 36.12 Ecclésiaste 8.8 Jérémie 10.25
8 Umehesabu kutanga-tanga kwangu; Uyatie machozi yangu katika chupa yako; (Je! Hayamo katika kitabu chako?)
Psaumes 39.12 2 Rois 20.5 Malachie 3.16 Matthieu 10.30 Psaumes 139.16
9 Ndipo adui zangu watarudi nyuma siku ile niitapo. Neno hili najua kuwa MUNGU yu upande wangu;
Romains 8.31 Psaumes 118.6 Psaumes 102.2 Esaïe 8.9-8.10 Psaumes 118.11-118.13
10 Kwa msaada wa MUNGU nitalisifu neno lake. Kwa msaada wa Bwana nitalisifu neno lake.
Psaumes 56.4 Genèse 32.11 Hébreux 6.18 2 Pierre 1.4 Matthieu 24.35
11 Nimemtumaini Mungu, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?
Esaïe 51.12-51.13 Psaumes 112.7-112.8 Esaïe 51.7-51.8 Psaumes 27.1
12 Ee Mungu, nadhiri zako zi juu yangu; Nitakutolea dhabihu za kushukuru.
Psaumes 50.14 Psaumes 9.1-9.3 Ecclésiaste 5.4-5.6 Nombres 30.2-30.16 Psaumes 59.16-59.17
13 Maana umeniponya nafsi yangu na mauti; Je! Hukuizuia miguu yangu isianguke? Ili nienende mbele za Mungu Katika nuru ya walio hai.
Psaumes 116.8-116.9 Job 33.30 1 Samuel 2.9 Apocalypse 21.23-21.24 Esaïe 38.3

Cette Bible est dans le domaine public.