Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 56
Bible en Swahili de l’est


Confiance dans la détresse

1 Mungu, unirehemu, maana yuko atakaye kunimeza, Mchana kutwa ananionea akileta vita.
Psaumes 69.13-69.16 Psaumes 57.1-57.3 Psaumes 16.1 Psaumes 27.2 Psaumes 31.9
2 Adui zangu wanataka kunimeza mchana kutwa, Maana waletao vita juu yangu kwa kiburi ni wengi.
Psaumes 91.1 Psaumes 35.1 Actes 4.25-4.27 Psaumes 93.4 Psaumes 92.1
3 Siku ya hofu yangu nitakutumaini Wewe;
Psaumes 55.4-55.5 Psaumes 34.4 1 Samuel 30.6 1 Samuel 21.12 2 Corinthiens 7.5-7.6
4 Kwa msaada wa MUNGU nitalisifu neno lake. Nimemtumaini Mungu, sitaogopa; Mwenye mwili atanitenda nini?
Psaumes 118.6 Hébreux 13.6 Psaumes 27.1 Psaumes 56.10-56.11 Psaumes 119.160
5 Mchana kutwa wanapotosha maneno yangu, Mawazo yao yote ni juu yangu kunitakia mabaya.
2 Pierre 3.16 Jérémie 18.18 Psaumes 41.7 1 Samuel 18.29 Esaïe 29.20-29.21
6 Hukutanika, hujificha, huziangalia nyayo zangu, Kwa kuwa wameniotea nafsi yangu.
Psaumes 71.10 Psaumes 59.3 Psaumes 140.2 Daniel 6.4 Matthieu 26.3-26.4
7 Je! Wataokoka kwa uovu wao? Ee Mungu, uwaangamize kwa hasira yako.
Psaumes 55.23 Ecclésiaste 8.8 Jérémie 10.25 Esaïe 28.15 Jérémie 18.19-18.23
8 Umehesabu kutanga-tanga kwangu; Uyatie machozi yangu katika chupa yako; (Je! Hayamo katika kitabu chako?)
Psaumes 39.12 2 Rois 20.5 Malachie 3.16 Psaumes 139.16 Apocalypse 7.17
9 Ndipo adui zangu watarudi nyuma siku ile niitapo. Neno hili najua kuwa MUNGU yu upande wangu;
Romains 8.31 Psaumes 102.2 Psaumes 118.6 Psaumes 46.11 Jérémie 33.3
10 Kwa msaada wa MUNGU nitalisifu neno lake. Kwa msaada wa Bwana nitalisifu neno lake.
Genèse 32.11 Hébreux 6.18 2 Pierre 1.4 Matthieu 24.35 Psaumes 60.6
11 Nimemtumaini Mungu, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?
Esaïe 51.12-51.13 Psaumes 112.7-112.8 Esaïe 51.7-51.8 Psaumes 27.1
12 Ee Mungu, nadhiri zako zi juu yangu; Nitakutolea dhabihu za kushukuru.
Psaumes 9.1-9.3 Psaumes 50.14 Psaumes 66.13-66.14 Genèse 35.1-35.3 Genèse 28.20-28.22
13 Maana umeniponya nafsi yangu na mauti; Je! Hukuizuia miguu yangu isianguke? Ili nienende mbele za Mungu Katika nuru ya walio hai.
Job 33.30 Psaumes 116.8-116.9 Psaumes 49.15 Jean 12.35-12.36 Jean 8.12

Cette Bible est dans le domaine public.