Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 56.1
Bible en Swahili de l’est


Confiance dans la détresse

1 Mungu, unirehemu, maana yuko atakaye kunimeza, Mchana kutwa ananionea akileta vita.
Psaumes 69.13-69.16 Psaumes 57.1-57.3 Psaumes 16.1 Psaumes 27.2 1 Samuel 21.11-21.15
2 Adui zangu wanataka kunimeza mchana kutwa, Maana waletao vita juu yangu kwa kiburi ni wengi.
Psaumes 9.2 Psaumes 3.1 Psaumes 57.3 Psaumes 118.10-118.12 Daniel 5.18
3 Siku ya hofu yangu nitakutumaini Wewe;
Psaumes 55.4-55.5 Psaumes 34.4 1 Samuel 30.6 1 Samuel 21.10 1 Samuel 21.12
4 Kwa msaada wa MUNGU nitalisifu neno lake. Nimemtumaini Mungu, sitaogopa; Mwenye mwili atanitenda nini?
Psaumes 118.6 Hébreux 13.6 Psaumes 56.10-56.11 Psaumes 119.160 Psaumes 27.1
5 Mchana kutwa wanapotosha maneno yangu, Mawazo yao yote ni juu yangu kunitakia mabaya.
2 Pierre 3.16 Matthieu 22.15 Matthieu 26.61 1 Samuel 20.33 1 Samuel 18.17
6 Hukutanika, hujificha, huziangalia nyayo zangu, Kwa kuwa wameniotea nafsi yangu.
Psaumes 59.3 Psaumes 71.10 Psaumes 140.2 Job 14.16 Job 31.4
7 Je! Wataokoka kwa uovu wao? Ee Mungu, uwaangamize kwa hasira yako.
Psaumes 55.23 Psaumes 94.20-94.21 Jérémie 7.10 Habakuk 1.13 Psaumes 55.9
8 Umehesabu kutanga-tanga kwangu; Uyatie machozi yangu katika chupa yako; (Je! Hayamo katika kitabu chako?)
Psaumes 39.12 2 Rois 20.5 Malachie 3.16 Matthieu 10.30 Psaumes 139.16
9 Ndipo adui zangu watarudi nyuma siku ile niitapo. Neno hili najua kuwa MUNGU yu upande wangu;
Romains 8.31 Psaumes 118.6 Psaumes 102.2 Psaumes 27.2 Psaumes 46.7
10 Kwa msaada wa MUNGU nitalisifu neno lake. Kwa msaada wa Bwana nitalisifu neno lake.
Psaumes 56.4 Genèse 32.11 Hébreux 6.18 2 Pierre 1.4 Matthieu 24.35
11 Nimemtumaini Mungu, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?
Esaïe 51.12-51.13 Psaumes 112.7-112.8 Esaïe 51.7-51.8 Psaumes 27.1
12 Ee Mungu, nadhiri zako zi juu yangu; Nitakutolea dhabihu za kushukuru.
Psaumes 50.14 Psaumes 9.1-9.3 Psaumes 116.14-116.19 1 Samuel 1.11 Psaumes 119.106
13 Maana umeniponya nafsi yangu na mauti; Je! Hukuizuia miguu yangu isianguke? Ili nienende mbele za Mungu Katika nuru ya walio hai.
Psaumes 116.8-116.9 Job 33.30 Esaïe 2.5 Jacques 5.20 Psaumes 86.12-86.13

Cette Bible est dans le domaine public.