Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 26.3
Bible en Swahili de l’est


Prière de l’homme intègre

1 Ee Bwana, unihukumu mimi, Maana nimekwenda kwa ukamilifu wangu, Nami nimemtumaini Bwana bila wasiwasi.
Psaumes 7.8 Psaumes 28.7 Proverbes 20.7 2 Rois 20.3 1 Pierre 1.5
2 Ee Bwana, unijaribu na kunipima; Unisafishe mtima wangu na moyo wangu.
Psaumes 7.9 Psaumes 17.3 Job 13.23 Psaumes 66.10 Zacharie 13.9
3 Maana fadhili zako zi mbele ya macho yangu, Nami nimekwenda katika kweli yako.
2 Rois 20.3 1 Jean 4.7-4.12 1 Jean 1.7 Ephésiens 4.20-4.25 Psaumes 86.11
4 Sikuketi pamoja na watu wa ubatili, Wala sitaingia mnamo wanafiki.
Psaumes 1.1 Jérémie 15.17 Psaumes 119.115 1 Corinthiens 15.33 Psaumes 119.63
5 Nimelichukia kusanyiko la watenda mabaya, Wala sitaketi pamoja na watu waovu.
Psaumes 31.6 Psaumes 139.21-139.22 1 Corinthiens 5.9-5.11 Psaumes 1.1 Psaumes 101.3-101.8
6 Nitanawa mikono yangu kwa kutokuwa na hatia, Na kuizunguka madhabahu yako, Ee Bwana
Psaumes 73.13 Psaumes 43.4 Exode 30.19-30.20 Psaumes 24.4 1 Timothée 2.8
7 Ili niitangaze sauti ya kushukuru, Na kuzisimulia kazi zako za ajabu.
Psaumes 9.1 Psaumes 71.17-71.19 Psaumes 145.5 Luc 19.37-19.40 1 Samuel 1.24
8 Bwana, nimependa makao ya nyumba yako, Na mahali pa maskani ya utukufu wako.
Luc 2.49 Jean 2.14-2.17 Psaumes 27.4-27.6 Psaumes 63.2-63.3 2 Samuel 15.25
9 Usiiondoe nafsi yangu pamoja na wakosaji, Wala uhai wangu pamoja na watu wa damu.
Psaumes 139.19 Matthieu 24.51 Matthieu 25.46 Psaumes 51.14 Psaumes 55.23
10 Mikononi mwao mna madhara, Na mkono wao wa kuume umejaa rushwa.
Deutéronome 16.19 1 Samuel 8.3 Exode 23.8 Psaumes 10.14 Michée 2.1-2.3
11 Ila mimi nitakwenda kwa ukamilifu wangu; Unikomboe, unifanyie fadhili.
Psaumes 69.18 Psaumes 26.1 1 Samuel 12.2-12.5 Néhémie 5.15 Esaïe 38.3
12 Mguu wangu umesimama palipo sawa; Katika makusanyiko nitamhimidi Bwana.
Psaumes 27.11 Psaumes 40.2 Psaumes 111.1 Proverbes 10.9 Psaumes 26.7

Cette Bible est dans le domaine public.