Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 118.28
Bible en Swahili de l’est


Louange à Dieu pour sa bonté

1 Haleluya. Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele.
1 Chroniques 16.34 Psaumes 136.1 Psaumes 106.1 1 Chroniques 16.8 Psaumes 107.1
2 Israeli na aseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele.
Psaumes 115.9-115.11 Psaumes 135.19-135.20 1 Pierre 2.9-2.10 Galates 6.16 Hébreux 13.15
3 Mlango wa Haruni na waseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele.
Apocalypse 1.6 Apocalypse 5.8-5.10 Psaumes 134.1-134.3 1 Pierre 2.5 Apocalypse 4.7-4.11
4 Wamchao Bwana na waseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele.
Psaumes 22.23 Apocalypse 19.5
5 Katika shida yangu nalimwita Bwana; Bwana akanijibu akaniweka panapo nafasi.
Psaumes 18.19 Psaumes 40.1-40.3 Psaumes 18.6 Psaumes 120.1 Psaumes 116.3-116.4
6 Bwana yuko upande wangu, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?
Hébreux 13.6 Psaumes 56.4 Psaumes 56.9 Psaumes 56.11 Esaïe 51.12
7 Bwana yuko upande wangu, msaidizi wangu, Kwa hiyo nitawaona wanaonichukia wameshindwa.
Psaumes 54.4 Psaumes 59.10 Psaumes 54.7 Psaumes 92.11 Psaumes 112.8
8 Ni heri kumkimbilia Bwana Kuliko kuwatumainia wanadamu.
Psaumes 40.4 Jérémie 17.5-17.7 Psaumes 62.8-62.9 Michée 7.5-7.7
9 Ni heri kumkimbilia Bwana. Kuliko kuwatumainia wakuu.
Esaïe 30.2-30.3 Psaumes 146.3-146.5 Esaïe 31.1 Esaïe 30.15-30.17 Ezéchiel 29.7
10 Mataifa yote walinizunguka; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
Zacharie 14.1-14.3 2 Samuel 5.1-5.25 2 Samuel 8.1-8.18 Psaumes 18.40 Psaumes 88.17
11 Walinizunguka, naam, walinizunguka; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
Psaumes 88.17 Psaumes 22.12-22.16 1 Chroniques 19.10 1 Samuel 23.26
12 Walinizunguka kama nyuki, Walizimika kama moto wa miibani; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
Deutéronome 1.44 Esaïe 27.4 Psaumes 58.9 1 Samuel 17.45 Psaumes 20.5
13 Ulinisukuma sana ili nianguke; Lakini Bwana akanisaidia.
Psaumes 140.4 Psaumes 18.17-18.18 Psaumes 86.17 1 Samuel 25.29 2 Samuel 17.1-17.3
14 Bwana ni nguvu zangu na wimbo wangu, Naye amekuwa wokovu wangu.
Esaïe 12.2 Exode 15.2-15.6 Esaïe 45.17 Psaumes 18.2 Matthieu 1.21-1.23
15 Sauti ya furaha na wokovu Imo hemani mwao wenye haki; Mkono wa kuume wa Bwana hutenda makuu.
Psaumes 89.13 Psaumes 60.12 Actes 2.46-2.47 Psaumes 68.3 Psaumes 119.54
16 Mkono wa kuume wa Bwana umetukuzwa; Mkono wa kuume wa Bwana hutenda makuu.
Exode 15.6 Actes 2.32-2.36
17 Sitakufa bali nitaishi, Nami nitayasimulia matendo ya Bwana.
Psaumes 73.28 Psaumes 6.5 Psaumes 107.22 Habakuk 1.12 Esaïe 38.16-38.20
18 Bwana ameniadhibu sana, Lakini hakuniacha nife.
2 Corinthiens 6.9 1 Corinthiens 11.32 Job 5.17-5.18 2 Samuel 16.1-16.23 Psaumes 94.12-94.13
19 Nifungulieni malango ya haki, Nitaingia na kumshukuru Bwana.
Esaïe 26.2 Apocalypse 22.14 Psaumes 9.13-9.14 Psaumes 100.4 Esaïe 38.22
20 Lango hili ni la Bwana, Wenye haki ndio watakaoliingia.
Apocalypse 21.24-21.27 Esaïe 26.2 Psaumes 24.9 Apocalypse 22.14-22.15 Psaumes 24.3-24.4
21 Nitakushukuru kwa maana umenijibu, Nawe umekuwa wokovu wangu.
Psaumes 116.1 Esaïe 49.8 Psaumes 118.14 Esaïe 12.2 Psaumes 69.33-69.34
22 Jiwe walilolikataa waashi Limekuwa jiwe kuu la pembeni.
Luc 20.17 Matthieu 21.42 Actes 4.11 Ephésiens 2.20-2.22 1 Pierre 2.4-2.8
23 Neno hili limetoka kwa Bwana, Nalo ni ajabu machoni petu.
Actes 4.13 Job 5.9 Actes 13.41 Ephésiens 1.19-1.22 Actes 3.14-3.15
24 Siku hii ndiyo aliyoifanya Bwana, Tutashangilia na kuifurahia.
Psaumes 84.10 Esaïe 58.13 Zacharie 3.9 Néhémie 8.10 1 Rois 8.66
25 Ee Bwana, utuokoe, twakusihi; Ee Bwana, utufanikishe, twakusihi.
Psaumes 20.9 Psaumes 90.17 Psaumes 69.13 Psaumes 69.1 Psaumes 22.21
26 Na abarikiwe yeye ajaye kwa jina la Bwana; Tumewabarikia toka nyumbani mwa Bwana.
Matthieu 21.9 Luc 19.38 Jean 12.13 Psaumes 129.8 Matthieu 23.39
27 Bwana ndiye aliye Mungu, Naye ndiye aliyetupa nuru. Ifungeni dhabihu kwa kamba Pembeni mwa madhabahu.
Esther 8.16 1 Pierre 2.9 Psaumes 18.28 Exode 27.2 Hébreux 13.15
28 Ndiwe Mungu wangu, nami nitakushukuru, Ndiwe Mungu wangu, nami nitakutukuza.
Esaïe 25.1 Exode 15.2 Psaumes 146.2 Psaumes 145.1 Esaïe 12.2
29 Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Psaumes 118.1 Esaïe 63.7 Esdras 3.11 Psaumes 103.17

Cette Bible est dans le domaine public.