Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 118
Bible en Swahili de l’est


Louange à Dieu pour sa bonté

1 Haleluya. Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele.
1 Chroniques 16.8 1 Chroniques 16.34 Psaumes 136.1 Psaumes 106.1 Psaumes 100.5
2 Israeli na aseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele.
Psaumes 115.9-115.11 Psaumes 135.19-135.20 Psaumes 147.19-147.20 Psaumes 145.10 1 Pierre 2.9-2.10
3 Mlango wa Haruni na waseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele.
1 Pierre 2.5 Apocalypse 4.7-4.11 Apocalypse 1.6 Apocalypse 5.8-5.10 Psaumes 134.1-134.3
4 Wamchao Bwana na waseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele.
Psaumes 22.23 Apocalypse 19.5
5 Katika shida yangu nalimwita Bwana; Bwana akanijibu akaniweka panapo nafasi.
Psaumes 18.19 Psaumes 40.1-40.3 Psaumes 18.6 Psaumes 120.1 Psaumes 116.3-116.4
6 Bwana yuko upande wangu, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?
Hébreux 13.6 Psaumes 56.4 Psaumes 56.9 Psaumes 56.11 Esaïe 51.12
7 Bwana yuko upande wangu, msaidizi wangu, Kwa hiyo nitawaona wanaonichukia wameshindwa.
Psaumes 59.10 Psaumes 54.4 Psaumes 54.7 1 Chroniques 12.18 Psaumes 55.18
8 Ni heri kumkimbilia Bwana Kuliko kuwatumainia wanadamu.
Psaumes 40.4 Jérémie 17.5-17.7 Psaumes 62.8-62.9 Michée 7.5-7.7
9 Ni heri kumkimbilia Bwana. Kuliko kuwatumainia wakuu.
Esaïe 30.2-30.3 Psaumes 146.3-146.5 Esaïe 31.1 Ezéchiel 29.7 Esaïe 31.8
10 Mataifa yote walinizunguka; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
Zacharie 14.1-14.3 2 Samuel 10.1-10.19 Apocalypse 20.8-20.9 Apocalypse 19.19-19.21 2 Samuel 5.1-5.25
11 Walinizunguka, naam, walinizunguka; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
Psaumes 88.17 Psaumes 22.12-22.16 1 Samuel 23.26 1 Chroniques 19.10
12 Walinizunguka kama nyuki, Walizimika kama moto wa miibani; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
Deutéronome 1.44 Nahum 1.10 Esaïe 27.4 Psaumes 58.9 1 Samuel 17.45
13 Ulinisukuma sana ili nianguke; Lakini Bwana akanisaidia.
Psaumes 140.4 Psaumes 18.17-18.18 1 Samuel 20.3 Psaumes 86.17 1 Samuel 25.29
14 Bwana ni nguvu zangu na wimbo wangu, Naye amekuwa wokovu wangu.
Esaïe 12.2 Esaïe 45.22-45.25 Psaumes 27.1 Exode 15.2-15.6 Esaïe 45.17
15 Sauti ya furaha na wokovu Imo hemani mwao wenye haki; Mkono wa kuume wa Bwana hutenda makuu.
Psaumes 89.13 Actes 2.46-2.47 Psaumes 60.12 Apocalypse 19.1-19.5 Actes 16.34
16 Mkono wa kuume wa Bwana umetukuzwa; Mkono wa kuume wa Bwana hutenda makuu.
Exode 15.6 Actes 2.32-2.36
17 Sitakufa bali nitaishi, Nami nitayasimulia matendo ya Bwana.
Psaumes 73.28 Psaumes 6.5 Psaumes 107.22 Habakuk 1.12 Esaïe 38.16-38.20
18 Bwana ameniadhibu sana, Lakini hakuniacha nife.
2 Corinthiens 6.9 1 Corinthiens 11.32 Job 5.17-5.18 Psaumes 66.10-66.12 Job 33.16-33.30
19 Nifungulieni malango ya haki, Nitaingia na kumshukuru Bwana.
Esaïe 26.2 Apocalypse 22.14 Psaumes 100.4 Psaumes 9.13-9.14 Psaumes 116.18-116.19
20 Lango hili ni la Bwana, Wenye haki ndio watakaoliingia.
Apocalypse 21.24-21.27 Apocalypse 22.14-22.15 Psaumes 24.3-24.4 Psaumes 24.7 Esaïe 26.2
21 Nitakushukuru kwa maana umenijibu, Nawe umekuwa wokovu wangu.
Psaumes 116.1 Psaumes 118.14 Esaïe 49.8 Psaumes 22.23-22.24 Esaïe 12.2
22 Jiwe walilolikataa waashi Limekuwa jiwe kuu la pembeni.
Luc 20.17 Matthieu 21.42 Ephésiens 2.20-2.22 Actes 4.11 1 Pierre 2.4-2.8
23 Neno hili limetoka kwa Bwana, Nalo ni ajabu machoni petu.
Actes 13.41 Ephésiens 1.19-1.22 Actes 4.13 Job 5.9 Actes 5.31-5.32
24 Siku hii ndiyo aliyoifanya Bwana, Tutashangilia na kuifurahia.
Psaumes 84.10 Esaïe 58.13 Zacharie 3.9 Néhémie 8.10 1 Rois 8.66
25 Ee Bwana, utuokoe, twakusihi; Ee Bwana, utufanikishe, twakusihi.
Psaumes 90.17 Psaumes 20.9 Psaumes 22.21 Psaumes 69.13 Psaumes 69.1
26 Na abarikiwe yeye ajaye kwa jina la Bwana; Tumewabarikia toka nyumbani mwa Bwana.
Matthieu 21.9 Luc 19.38 Matthieu 23.39 Jean 12.13 Psaumes 129.8
27 Bwana ndiye aliye Mungu, Naye ndiye aliyetupa nuru. Ifungeni dhabihu kwa kamba Pembeni mwa madhabahu.
Esther 8.16 1 Pierre 2.9 Psaumes 18.28 Exode 27.2 Jean 8.12
28 Ndiwe Mungu wangu, nami nitakushukuru, Ndiwe Mungu wangu, nami nitakutukuza.
Exode 15.2 Esaïe 25.1 Esaïe 12.2 Esaïe 25.9 Psaumes 146.2
29 Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Psaumes 118.1 Psaumes 103.17 Esaïe 63.7 Esdras 3.11

Cette Bible est dans le domaine public.