Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 10.22
Bible en Swahili de l’est


1 Nafsi yangu inachoka na maisha yangu; Sitajizuia na kuugua kwangu; Nitanena kwa uchungu wa roho yangu.
Job 7.11 1 Rois 19.4 Job 9.21 Nombres 11.15 Job 6.8-6.9
2 Nitamwambia Mungu, Usinihukumie makosa; Nionyeshe sababu ya wewe kushindana nami.
Job 9.29 Psaumes 143.2 Psaumes 139.23-139.24 Job 34.31-34.32 Psaumes 109.21
3 Je! Ni vema kwako wewe kuonea, Na kuidharau kazi ya mikono yako, Na kuyaangazia mashauri ya waovu?
Esaïe 64.8 Job 14.15 Psaumes 138.8 Psaumes 69.33 Job 21.16
4 Je! Wewe una macho ya kimwili, Au je! Waona kama aonavyo binadamu?
1 Samuel 16.7 Job 9.32 Apocalypse 1.14 Luc 16.15
5 Je! Siku zako ni kama siku za mtu, Au je! Miaka yako ni kama siku za mtu,
2 Pierre 3.8 Hébreux 1.12 Psaumes 102.24-102.27 Psaumes 90.2-90.4 Job 36.26
6 Hata ukauliza-uliza habari za uovu wangu, Na kuitafuta dhambi yangu,
Job 14.16 1 Corinthiens 4.5 Psaumes 44.21 Psaumes 10.15 Job 10.14-10.17
7 Ujapojua ya kuwa mimi si mwovu; Wala hapana awezaye kuokoa na mkono wako?
Deutéronome 32.39 Job 23.13-23.14 Psaumes 1.6 Daniel 3.15 1 Thessaloniciens 2.10
8 Mikono yako imeniumba na kunifinyanga; Nawe utageuka na kuniangamiza?
Psaumes 119.73 Esaïe 43.7 Job 10.3 Genèse 6.6-6.7 Jérémie 18.3-18.10
9 Kumbuka, nakusihi ulivyonifinyanga kama vile udongo; Nawe, je! Utanirudisha uvumbini tena?
Genèse 2.7 Esaïe 64.8 Genèse 3.19 Ecclésiaste 12.7 Jérémie 18.6
10 Je! Wewe hukunimimina kama maziwa, Na kunigandisha mfano wa jibini?
Psaumes 139.14-139.16
11 Umenivika ngozi na nyama, Na kuniunga pamoja kwa mifupa na mishipa.
Ezéchiel 37.4-37.8 Job 40.17-40.18 Ephésiens 4.16 2 Corinthiens 5.2-5.3
12 Umenijazi uhai na upendeleo, Na maangalizi yako yameilinda roho yangu.
Actes 17.28 Job 33.4 Actes 17.25 Genèse 19.19 Matthieu 6.25
13 Lakini mambo haya uliyaficha moyoni mwako; Najua kuwa haya yamo nafsini mwako;
Job 23.13 Deutéronome 32.39 Job 23.9 Esaïe 45.15 Esaïe 46.9-46.11
14 Nikifanya dhambi, ndipo waniangalia, Wala hutaniachilia na uovu wangu.
Job 7.21 Psaumes 130.3 Nombres 14.18 Exode 34.7 Job 14.16
15 Mimi nikiwa mbaya, ole wangu! Nami nikiwa mwenye haki, walakini sitainua kichwa changu; Mimi nimejaa aibu Na kuyaangalia mateso yangu.
Esaïe 3.11 Job 9.15 Psaumes 25.18 Job 10.7 Job 9.20-9.21
16 Kichwa changu kikijiinua, waniwinda kama simba; Tena wajionyesha kwangu kuwa wa ajabu.
Esaïe 38.13 Lamentations 3.10 Job 5.9 Nombres 16.29-16.30 Amos 3.8
17 Wewe warejeza upya hao mashahidi yako juu yangu, Na kasirani yako waiongeza juu yangu; Jeshi kwa jeshi juu yangu.
Job 16.8 Ruth 1.21 Job 16.11-16.16 Job 19.6-19.11 Psaumes 55.19
18 Kwa nini basi kunitoa tumboni? Ningekata roho, lisinione jicho lo lote.
Jérémie 20.14-20.18 Matthieu 26.24 Job 14.10 Job 11.20 Jérémie 15.10
19 Ningalikuwa kama mtu asiyekuwapo; Ningalichukuliwa kaburini kutoka tumboni.
Psaumes 58.8
20 Je! Siku zangu si chache? Acha basi, Usinisumbue, nipate ngaa kutuzwa moyo kidogo.
Job 14.1 Psaumes 39.13 Job 7.16-7.21 Job 8.9 Job 9.25-9.26
21 Kabla sijaenda huko ambako sitarudi kutoka huko tena, Ni hiyo nchi ya giza, giza tupu;
Job 3.5 2 Samuel 12.23 Psaumes 23.4 Job 16.22 Job 14.10-14.14
22 Ni nchi ya giza kuu, kama giza lenyewe lilivyo; Ni nchi ya giza tupu, isiyo na matengezo ya mambo yo yote, Nchi ambayo nuru yake ni kama giza.
Psaumes 88.12 Job 34.22 Luc 16.26 Job 3.5 Psaumes 23.4

Cette Bible est dans le domaine public.