Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Chroniques 36.10
Bible en Swahili de l’est


Règnes de Joachaz, Jojakim et Jojakin

1 Watu wa nchi wakamtwaa Yehoahazi mwana wa Yosia, wakamtawaza awe mfalme katika Yerusalemu badala ya babaye.
Jérémie 22.11 1 Chroniques 3.15 2 Rois 23.30-23.37 2 Chroniques 26.1 2 Chroniques 33.25
2 Yehoahazi alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitatu alipoanza kutawala; akatawala huko Yerusalemu miezi mitatu.
3 Naye mfalme wa Misri akamwondoa katika Yerusalemu, akaitoza nchi talanta mia za fedha, na talanta moja ya dhahabu.
2 Rois 23.33
4 Mfalme wa Misri akamtawaza Eliakimu nduguye awe mfalme juu ya Yuda na Yerusalemu, akambadilisha jina lake kuwa Yehoyakimu. Neko akamtwaa Yehoahazi nduguye, akamchukua mpaka Misri.
Jérémie 22.10-22.12 1 Chroniques 3.15 2 Rois 23.34-23.35 Ezéchiel 19.3-19.4
5 Yehoyakimu alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala; akatawala katika Yerusalemu miaka kumi na mmoja; akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, Mungu wake.
2 Rois 23.36-23.37 Jérémie 22.13-22.19 Jérémie 26.1 Jérémie 35.1 Jérémie 36.27-36.32
6 Juu yake akakwea Nebukadreza,
2 Chroniques 33.11 Ezéchiel 19.5-19.9 Habakuk 1.5-1.10 2 Rois 24.13-24.20 Daniel 1.1-1.2
7 Nebukadreza akachukua baadhi ya vyombo vya nyumba ya Bwana mpaka Babeli, akavitia katika hekalu lake huko Babeli.
2 Rois 24.13 Jérémie 27.16-27.18 Daniel 5.2-5.4 Jérémie 28.3 Daniel 1.2
8 Basi mambo yote ya Yehoyakimu yaliyosalia, na machukizo yake aliyoyafanya, nayo yaliyoonekana kwake, tazama, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda; na Yekonia
2 Rois 24.5-24.6 Jérémie 22.24 Jérémie 22.28 1 Chroniques 3.16-3.17 Matthieu 1.11-1.12
9 Yekonia alikuwa na umri wa miaka kumi na minane alipoanza kutawala; akatawala katika Yerusalemu miezi mitatu na siku kumi; akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana.
2 Rois 24.8-24.17
10 Mwaka ulipokwisha, Nebukadreza akatuma wajumbe, akamchukua mpaka Babeli; pamoja na vyombo vya thamani vya nyumba ya Bwana; akamtawaza Sedekia nduguye awe mfalme juu ya Yuda na Yerusalemu.
Jérémie 37.1 2 Chroniques 36.7 Daniel 5.23 2 Rois 25.27-25.30 Daniel 1.1-1.2

Règne de Sédécias

11 Sedekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja, alipoanza kutawala; akatawala katika Yerusalemu miaka kumi na mmoja;
2 Rois 24.18-24.20 Jérémie 27.1 Jérémie 28.1 Jérémie 52.1-52.3
12 akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, Mungu wake; wala hakujinyenyekesha mbele ya Yeremia nabii aliponena kwa kinywa cha Bwana.
2 Chroniques 33.23 Jérémie 37.2-37.21 Jérémie 38.14-38.28 1 Pierre 5.6 Daniel 5.22-5.23
13 Tena akamwasi mfalme Nebukadreza, aliyemwapisha kwa Mungu; lakini akajifanyia shingo ngumu, akajitia moyo nguvu asimgeukie Bwana, Mungu wa Israeli.
2 Chroniques 30.8 Jérémie 52.2-52.3 Josué 9.15 Esaïe 48.4 Romains 2.4-2.5
14 Na zaidi ya hayo wakuu wote wa makuhani, na watu, wakakosa mno sawasawa na machukizo yote ya mataifa; wakainajisi nyumba ya Bwana aliyoitakasa katika Yerusalemu.
Michée 3.1-3.4 2 Chroniques 33.9 Daniel 9.6 Jérémie 37.13-37.15 Jérémie 5.5
15 Naye Bwana, Mungu wa baba zao, akatuma kwao kwa mikono ya wajumbe wake, akiondoka mapema, na kutuma; kwa sababu aliwahurumia watu wake, na makao yake;
Jérémie 25.3-25.4 Jérémie 35.15 Jérémie 44.4-44.5 Jérémie 7.25 Jérémie 7.13
16 lakini waliwadhihaki wajumbe wa Mungu, na kuyadharau maneno yake, na kuwacheka manabii wake, hata ilipozidi ghadhabu ya Bwana juu ya watu wake, hata kusiwe na kuponya.
2 Chroniques 30.10 Proverbes 29.1 Jérémie 5.12-5.13 Psaumes 74.1 Luc 22.63-22.64
17 Kwa hiyo akaleta juu yao mfalme wa Wakaldayo, aliyewaua vijana wao kwa upanga nyumbani mwa patakatifu pao, asiwahurumie kijana wala mwanamwali, mzee wala mkongwe; akawatia wote mkononi mwake.
Psaumes 74.20 Esdras 9.7 Deutéronome 31.16-31.18 2 Chroniques 33.11 2 Rois 25.1-25.30
18 Na vyombo vyote vya nyumba ya Mungu, vikubwa kwa vidogo, na hazina za nyumba ya Bwana, na hazina za mfalme, na za wakuu wake; vyote pia akavileta Babeli.
2 Chroniques 36.10 2 Chroniques 36.7 Jérémie 52.17-52.23 2 Rois 25.13-25.17 Zacharie 1.6
19 Wakaiteketeza nyumba ya Mungu, wakaubomoa ukuta wa Yerusalemu, wakayateketeza kwa moto majumba yake yote, wakaviharibu vyombo vyake vyote vya thamani.
Psaumes 79.1 2 Rois 25.9-25.11 Psaumes 79.7 Jérémie 52.13-52.15 Jérémie 7.14
20 Na wale waliookoka na upanga akawachukua mpaka Babeli; wakamtumikia yeye na wanawe hata kulipoingia milki ya Uajemi;
Jérémie 27.7 Deutéronome 28.47-28.48 2 Rois 25.11 Esdras 1.1-1.11 2 Chroniques 36.22
21 ili kulitimiza neno la Bwana kwa kinywa cha Yeremia, hata nchi itakapofurahia sabato zake; kwa maana siku zote ilipokaa ukiwa ilishika sabato, kutimiza miaka sabini.
Jérémie 29.10 Lévitique 26.34-26.35 Daniel 9.2 Zacharie 1.12 Jérémie 26.6-26.7

Édit de Cyrus

22 Ikawa katika mwaka wa kwanza wa Koreshi, mfalme wa Uajemi, ili kwamba neno la Bwana alilolisema kwa kinywa cha Yeremia lipate kutimizwa, Bwana akamwamsha roho yake Koreshi, mfalme wa Uajemi, hata akapiga mbiu katika ufalme wake wote, akaiandika pia, akisema,
Jérémie 25.12 Jérémie 29.10 Esdras 1.1-1.3 Daniel 10.1 Jérémie 32.42-32.44
23 Koreshi, mfalme wa Uajemi asema hivi; Bwana, Mungu wa mbinguni, amenipa falme zote za dunia; naye ameniagiza nimjengee nyumba katika Yerusalemu, ulioko Yuda. Basi kila mtu katika ninyi nyote mlio watu wake, Bwana, Mungu wake, na awe pamoja naye, na akwee.
Daniel 5.18 Psaumes 75.5-75.7 Esdras 7.13 Daniel 4.35 1 Chroniques 22.16

Cette Bible est dans le domaine public.