Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Chroniques 17.16
Bible en Swahili de l’est


Règne de Josaphat

1 Na Yehoshafati mwanawe akatawala mahali pake, akajitia nguvu juu ya Israeli.
1 Rois 15.24 2 Chroniques 32.5 Ephésiens 6.10 Matthieu 1.8 1 Samuel 23.16
2 Akaweka jeshi katika miji yote yenye maboma ya Yuda, akatia na askari walinzi katika nchi ya Yuda, na katika miji ya Efraimu, aliyoitwaa Asa babaye.
2 Chroniques 15.8 2 Chroniques 11.5 2 Chroniques 11.11-11.12
3 Naye Bwana alikuwa pamoja na Yehoshafati, kwa kuwa alikwenda katika njia za kwanza za Daudi babaye, asiyatafute mabaali;
Psaumes 46.11 Matthieu 28.20 Exode 4.12 Psaumes 46.7 Josué 1.9
4 lakini alimtafuta Mungu wa baba yake, akaenda katika amri zake, wala si katika matendo ya Israeli.
1 Rois 12.28 1 Thessaloniciens 2.12 2 Rois 17.19 1 Thessaloniciens 4.1 Osée 4.15
5 Kwa hiyo Bwana akauthibitisha ufalme mkononi mwake; Yehoshafati akaletewa zawadi na Yuda wote; basi akawa na mali na heshima tele.
2 Chroniques 18.1 2 Chroniques 32.23 Matthieu 2.11 1 Samuel 10.27 1 Pierre 5.10
6 Ukainuliwa moyo wake katika njia za Bwana; na zaidi ya hayo akapaondoa mahali pa juu, na maashera, katika Yuda.
2 Chroniques 15.17 2 Chroniques 20.33 1 Rois 22.43 2 Chroniques 19.3 Psaumes 119.1
7 Tena, katika mwaka wa tatu wa kutawala kwake, akawatuma wakuu wake, yaani, Ben-haili, na Obadia, na Zekaria, na Nethaneli, na Mikaya, ili kufundisha mijini mwa Yuda;
2 Chroniques 35.3 2 Chroniques 15.3 Ecclésiaste 1.12 Deutéronome 4.5 Néhémie 9.3
8 na pamoja nao Walawi, yaani, Shemaya, na Nethania, na Zebadia, na Asaheli, na Shemiramothi, na Yehonathani, na Adonia, na Tobia, na Tob-adonia, Walawi; na pamoja nao Elishama na Yehoramu, makuhani.
2 Chroniques 19.8 Esdras 7.1-7.6 Malachie 2.7
9 Wakafundisha katika Yuda, wenye kitabu cha torati ya Bwana; wakazunguka katika miji yote ya Yuda, wakafundisha kati ya watu.
Matthieu 10.23 Néhémie 8.7 Matthieu 28.19-28.20 Actes 28.23 Deutéronome 6.4-6.9
10 Hofu ya Bwana ikaziangukia falme za nchi zote zilizozunguka Yuda, wasipigane vita na Yehoshafati.
2 Chroniques 14.14 Genèse 35.5 Proverbes 16.7 Exode 34.24 Exode 15.14-15.16
11 Na baadhi ya Wafilisti walimletea Yehoshafati zawadi, na fedha ya kodi; Waarabu nao wakamletea makundi, kondoo waume saba elfu na mia saba, na mabeberu saba elfu na mia saba.
2 Chroniques 26.8 2 Chroniques 9.14 2 Samuel 8.2 2 Rois 3.4 2 Chroniques 17.5
12 Ukuu wake Yehoshafati ukazidi sana; akajenga katika Yuda ngome na miji ya hazina.
2 Chroniques 8.2-8.6 2 Chroniques 11.5-11.12 2 Chroniques 32.5 2 Chroniques 26.6-26.9 2 Chroniques 14.6-14.7
13 Naye alikuwa na kazi nyingi katika miji ya Yuda; na watu wa vita, watu mashujaa humo Yerusalemu.
1 Chroniques 27.25-27.31 2 Chroniques 26.10-26.15
14 Na hivi ndivyo walivyohesabiwa kwa mbari za baba zao; wa Yuda, maakida wa maelfu; Adna jemadari, na pamoja naye watu mashujaa mia tatu elfu;
2 Chroniques 26.13 Nombres 1.2 2 Chroniques 14.8 Genèse 15.5 Genèse 12.2
15 na wa pili wake Yehohanani akida, na pamoja naye mia mbili na themanini elfu;
16 na baada yake Amasia mwana wa Zikri, aliyejitoa kwa Bwana kwa moyo, na pamoja naye mia mbili elfu, watu mashujaa;
Juges 5.9 1 Chroniques 29.9 Juges 5.2 1 Chroniques 29.17 2 Corinthiens 8.3-8.5
17 na wa Benyamini; Eliada mtu shujaa, na pamoja naye mia mbili elfu wenye nyuta na ngao;
2 Chroniques 14.8 2 Samuel 1.21-1.22
18 na wa pili wake Yehozabadi, na pamoja naye mia na themanini elfu waliojiweka tayari kwa vita.
19 Hao ndio waliomngojea mfalme, zaidi ya hao mfalme aliowaweka katika miji yenye maboma katika Yuda yote.
2 Chroniques 17.2 2 Chroniques 11.12 2 Chroniques 11.23 2 Chroniques 17.12

Cette Bible est dans le domaine public.