Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Chroniques 1.7
Bible en Swahili de l’est


Règne de Salomon

Accession de Salomon au trône

1 Basi Sulemani, mwana wa Daudi, alithibitishwa katika ufalme wake, naye Bwana, Mungu wake, alikuwa pamoja naye, akamtukuza mno.
1 Chroniques 29.25 1 Rois 2.46 1 Rois 2.12 Genèse 39.2 Genèse 21.22
2 Sulemani akasema na Israeli wote, na maakida wa maelfu, na wa mamia, na waamuzi, na kila shehe wa Israeli wote, wakuu wa nyumba za mababa.
1 Chroniques 28.1 1 Chroniques 27.1 2 Chroniques 30.2 1 Chroniques 24.31 1 Chroniques 29.1
3 Basi Sulemani akaenda mahali pa juu pa Gibeoni, na kusanyiko lote naye; kwani ndipo ilipokuwako hema ya kukutania ya Mungu, aliyoifanya Musa mtumishi wa Bwana jangwani.
1 Chroniques 16.39 1 Chroniques 21.29 Exode 40.34 Exode 36.8 Exode 40.2
4 Lakini sanduku la Mungu, Daudi alikuwa amelipandisha kutoka Kiriath-yearimu mpaka mahali Daudi alipolitengenezea; maana amelitandia hema katika Yerusalemu.
2 Samuel 6.2 2 Samuel 6.17 1 Chroniques 15.25-15.28 1 Chroniques 15.1 1 Chroniques 16.1
5 Tena madhabahu ya shaba, aliyoifanyiza Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, ilikuwako huko mbele ya maskani ya Bwana; Sulemani na kusanyiko wakaiendea.
Exode 31.2 Exode 38.1-38.7 1 Chroniques 13.3 1 Chroniques 2.19-2.20 Exode 27.1-27.8
6 Sulemani akaipandia huko madhabahu ya shaba mbele za Bwana, iliyokuwako hemani pa kukutania, akatoa sadaka elfu za kuteketezwa juu yake.
1 Rois 3.4 1 Rois 8.63 Esaïe 40.16 1 Chroniques 29.21
7 Usiku ule Mungu akamtokea Sulemani, akamwambia, Omba utakalo nikupe.
Marc 10.51 Matthieu 7.7-7.8 1 Jean 5.14-5.15 1 Rois 3.5-3.15 Jean 16.23
8 Sulemani akamwambia Mungu, Umemfanyia baba yangu Daudi fadhili kuu, nawe umenimilikisha mimi badala yake.
1 Chroniques 28.5 Psaumes 89.20-89.28 Psaumes 89.49 1 Chroniques 29.23 Esaïe 55.3
9 Basi sasa, Ee Bwana Mungu, na limyakinie baba yangu Daudi neno lako; maana umenitawaza niwe mfalme juu ya watu wengi kama mavumbi ya nchi.
Genèse 13.16 2 Samuel 7.12-7.16 Psaumes 89.35-89.37 Psaumes 132.11-132.12 Genèse 22.17
10 Basi sasa nipe hekima na maarifa, nijue kutoka na kuingia mbele ya watu hawa; kwa kuwa ni nani awezaye kuwahukumu watu wako hawa walio wengi?
Nombres 27.17 2 Samuel 5.2 Proverbes 2.2-2.6 1 Rois 3.9 2 Corinthiens 3.5
11 Naye Mungu akamwambia Sulemani, Kwa sababu neno hili lilikuwamo moyoni mwako, wala hukujitakia mali, wala utajiri, wala utukufu, wala maisha za wakuchukiao, wala hukujitakia maisha ya siku nyingi; bali umejitakia hekima na maarifa, upate kuwahukumu watu wangu, niliokutawaza juu yao;
Proverbes 23.7 1 Chroniques 29.17-29.18 1 Rois 8.18 1 Samuel 16.7 Hébreux 4.12
12 basi hekima na maarifa umepewa; nami nitakupa mali, na utajiri, na utukufu, kupita walivyokuwa navyo wafalme wote waliokuwa kabla yako, wala baada yako hapatakuwa na mtu atakayekuwa navyo.
2 Chroniques 9.22 1 Chroniques 29.25 Jacques 1.5 Matthieu 6.33 Ecclésiaste 2.9
13 Akaja Sulemani kutoka mahali pa juu pa Gibeoni, toka mbele ya hema ya kukutania, mpaka Yerusalemu; akatawala juu ya Israeli.
2 Chroniques 1.3 1 Rois 4.24-4.25
14 Sulemani akakusanya magari na wapandao farasi; naye alikuwa na magari elfu na mia nne, na wapandao farasi kumi na mbili elfu, aliowaweka katika miji ya magari, na pamoja na mfalme huko Yerusalemu.
1 Rois 4.26 1 Rois 10.26-10.29 2 Chroniques 9.25 1 Rois 9.19 1 Rois 10.16
15 Mfalme akafanya fedha na dhahabu kuwa kama mawe humo Yerusalemu, na mierezi akaifanya kuwa kama mikuyu iliyomo Shefela, kwa kuwa mingi.
2 Chroniques 9.27 Esaïe 60.17 Amos 7.14 Job 22.24-22.25 Esaïe 9.10
16 Nao farasi, aliokuwa nao Sulemani wakaletwa toka Misri; wakapewa wafanya biashara wake mfalme kwa makundi; kila kundi na thamani yake.
1 Rois 10.28-10.29 2 Chroniques 9.28
17 Nao hupandisha, na kuleta kutoka Misri gari kwa shekeli mia sita za fedha, na farasi kwa mia na hamsini, vivyo watu wakawaletea wafalme wote wa Wahiti, na wafalme wa Shamu, mikononi mwao.
2 Rois 10.29

Cette Bible est dans le domaine public.